Haji Manara Awachokoza tena TFF

Haji Manara Awachokoza tena TFF

Shark

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2010
Posts
29,775
Reaction score
29,746
Shirikisho la Mpira Tanzania linatakiwa kuchukua hatua kali zaidi kwa @hajismanara kwasababu ameendelea kukiuka adhabu aliyopewa ya kufungiwa miaka miwili. Hii ni dhihaka kubwa kwa chombo chetu cha kusimamia mpira nchini na kwa Wizara ya Michezo kwa ujumla wake, lakini inavuka na kudhalilisha utawala wa kisheria nchini.

Manara amefanya tukio la uvunjifu siku ya Wananchi wiki mbili zilizopita, Wakati TFF ikiwa tayari imemfikisha upya kwenye kamati ya nidhamu kwa mara nyingine, jana pia amekiuka na kuendelea kuwa msemaji wa Yanga akiuzungumzia mkataba wa Yanga na Jackson Group.

Narudia tena kushauri mamlaka za soka nchini @tanfootball kwamba Mpira huu wasipodhibitiwa watu wahuni kama huyu Manara basi tusahau mageuzi na uwekezaji ulioanza kujitokeza sasa. Mpira ni biashara kubwa sasa, Ni sekta inayoajiri na kulipa vijana wengi zaidi na kwa haraka zaidi Tanzania na nje ya nchi.

Manara aondolewe kabisa katika mpira wa nchi hii kwakufungiwa maisha, Ni kijana anayekosa sifa za kuwepo mpirani, Michezo iko mingi Tanzania aende kwingine ambako hakuna kanuni na sheria.

TFF simamieni mpira, simamieni kanuni.

Credit,
YN
 

Attachments

  • VID-1660982312946.mp4
    3.6 MB
Hili hata sijui niliweke vipi, jana au juzi nimemuona Shaffih Dauda akizungumzia utambulisho wa Diamond kwenye kudhamini mashindano yake ya Ndondo Cup.

Ikumbukwe Shaffih naye aliadhibiwa na Kamati ya Maadili asijihusishe na shughuli za michezo.
 
Hao TFF wangejikita kwenye issues nyingine za maendeleo huku kuvurugana na kupigishana kelele na watu / individuals ndio yale yale ya wrestling with the pig...., unashauriwa usifanye hivyo sababu nyote mtachafuka na mwenzako anafurahia.....
 
Hapo ni kutoa adhabu kwa aliyemuajiri.....Utopolo wapigwe faini wajue na wapate uchungu wa kuajiri huyo mtu.
Tukio kama la kwenye hii video ni kuwaonea Yanga, sababu ingawa kaiongelea Yanga but hakua klabuni, bali hotelini. Tukio la Yanga Day ni alikua kwenye shughuli ya Yanga.
 
Shirikisho la Mpira Tanzania linatakiwa kuchukua hatua kali zaidi kwa @hajismanara kwasababu ameendelea kukiuka adhabu aliyopewa ya kufungiwa miaka miwili. Hii ni dhihaka kubwa kwa chombo chetu cha kusimamia mpira nchini na kwa Wizara ya Michezo kwa ujumla wake, lakini inavuka na kudhalilisha utawala wa kisheria nchini.

Manara amefanya tukio la uvunjifu siku ya Wananchi wiki mbili zilizopita, Wakati TFF ikiwa tayari imemfikisha upya kwenye kamati ya nidhamu kwa mara nyingine, jana pia amekiuka na kuendelea kuwa msemaji wa Yanga akiuzungumzia mkataba wa Yanga na Jackson Group.

Narudia tena kushauri mamlaka za soka nchini @tanfootball kwamba Mpira huu wasipodhibitiwa watu wahuni kama huyu Manara basi tusahau mageuzi na uwekezaji ulioanza kujitokeza sasa. Mpira ni biashara kubwa sasa, Ni sekta inayoajiri na kulipa vijana wengi zaidi na kwa haraka zaidi Tanzania na nje ya nchi.

Manara aondolewe kabisa katika mpira wa nchi hii kwakufungiwa maisha, Ni kijana anayekosa sifa za kuwepo mpirani, Michezo iko mingi Tanzania aende kwingine ambako hakuna kanuni na sheria.

TFF simamieni mpira, simamieni kanuni.

Credit,
YN
Utakufa nacho kijiba cha roho.
 
Hili hata sijui niliweke vipi, jana au juzi nimemuona Shaffih Dauda akizungumzia utambulisho wa Diamond kwenye kudhamini mashindano yake ya Ndondo Cup.

Ikumbukwe Shaffih naye aliadhibiwa na Kamati ya Maadili asijihusishe na shughuli za michezo.
Dauda ameona hakuna kitu Haji amefanywa na ameendelea kuusemea mpira bila kujali! Pamoja na mapungufu ya viongozi wa TFF ( Kawaida kwa binadamu wote) lakini upo uwezekano wanasiasa wa juu wanaingilia haya mambo! Kiburi cha Haji si GSM tu, kuna sababu na hili sakata litakuja kuibua mengi.

Sasa TFF wamedharaulika na mpaka sasa hawajafanya lolote. Wengi tunasubiri kuona hili sakata litafia wapi. Tutawakumbusha hadi tuone mwisho.
 
Hivi lakinialichofanya sope kina tofauti gani na dauda, hii video mbona kaongea tu kama mwana utopolo?
 
Hili hata sijui niliweke vipi, jana au juzi nimemuona Shaffih Dauda akizungumzia utambulisho wa Diamond kwenye kudhamini mashindano yake ya Ndondo Cup.

Ikumbukwe Shaffih naye aliadhibiwa na Kamati ya Maadili asijihusishe na shughuli za michezo.

Sidhani kama hata ndondo ambayo anaandaa mwenyewe
 
Tff na Manara wote wapo sawa tuu...wamekuja na Ngao ya Hisani Timu ziwe nne wao kila kukicha hawajui wafanye nini toka walipokaa eti Timu iliyoshuka daraja inacheza tena play off na Timu iliyopanda daraja nikajua wahuni tumewapa kazi muhimu sana kimakosa..
 
Tff na Manara wote wapo sawa tuu...wamekuja na Ngao ya Hisani Timu ziwe nne wao kila kukicha hawajui wafanye nini toka walipokaa eti Timu iliyoshuka daraja inacheza tena play off na Timu iliyopanda daraja nikajua wahuni tumewapa kazi muhimu sana kimakosa..
 
Hivi lakinialichofanya sope kina tofauti gani na dauda, hii video mbona kaongea tu kama mwana utopolo?
Hivi tff wanaweza kumiliki hadi mdomo wa mtu?
Haji anaongelea mambo ya maendeleo ya timu yake tena anasimulia jinsi watakavyonufaika na sio anahamasisha au kutafuta wadau....acheni ufala
 
Back
Top Bottom