Haji Manara: Mimi na kocha Gamondi hatusalimiani, aliwahi kunipa tuhuma nzito kutaka yeye afukuzwe Yanga

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Wakuu msikie Manara huko!

Anasema katika kipindi cha kuelekea katika kilele cha wiki ya mwananchi mwezi Agosti mwaka huu 2024 wakati ameenda kambi ya Timu ya Yanga kuongea na wachezaji na bechi la ufundi ili kuwapa plan ya siku hiyo ya wiki ya mwananchi, lakini siku yake ikaharibiwa na kocha mkuu wa Yanga Miguel Gamond.

Kwa madai ya Manara anasema kocha Gamond alimwambia wewe Haji Manara nasikia ulipost Instagram kwamba mimi nifukuzwe unitaki niwepo Yanga. Manara alipigwa na mshangao baada kuyasikia hayo.

Na tangu hapo hawajawi kuongea na wala kusalimiana licha Manara anasema yeye anamkubali kocha na bado anastahili kuendelea kubaki Yanga zaidi.

Vipi hapo wadau huyu Manara alichesema

Your browser is not able to display this video.
 
Manara hana impact tena, sio simba wala yanga,,,,amebaki anabwabwaja tu ,,, ! Hapo yanga yupo tu kwa sababu ya GSM , kina Hersi walishamchoka ! Mtu mzima [anaelekea 50yrs au ameshafikisha] lakini akili kisoda ! Hajui nini ch kuzungumza na kipi kisizungumzwe
 
ndio maana baba yake toka chekechea aliona hasara akamtoa IST
 
“Kwasasa sina mahusiano yoyote na Engineer Hersi, tuna miezi mitatu nadhani hatujaongea, ni tofauti na hapo zamani nami sijamtafuta kuongea nae kwakuwa yeye si alisema Mimi ni Mwanachama tu sasa Mimi nimwambie nini yeye kila Mtu ana thamani yake ambayo anapaswa kuijua”

- Haji Sunday Manara kupitia AMPLIFAYA ya @cloudsfmtz
 
Niliwai kuweka hii hapa

 
 
Manara huenda ana tatizo la afya ya akili,achunguzwe!
Anajiona mkubwa sana na kiumbe wa aina yake,hii si kawaida.
 
Uzi uishie hapa tafadhali,huyu mtu muda wake umekwisha kwenye soka la Bongo,

The last kick of the dying Horse.
 
Ila huyu jamaa ana kihere here sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…