Haji Manara sijakuelewa

... Nilitegemea ungekuja ungeanza na tathmni ya mchezo uliopita, Kisha ukatuambia na Nini kifanyike katika mchezo ujao na As Vita,
Tathmini ya mchezo hutolewa na kocha au msaidizi wake. Tuheshimu taaluma za watu, Manara yupo sahihi kutozungumzia masuala ya kiufundi. Kuna timu moja kocha anaitisha mkutano wa agenda ya kukusanya mapato ya klabu, na anachukua na minutes za mkutano, sijui wakati huo Mwenyekiti wa klabu au Makamu wake wanakuwa na wajibu gani
 
Kwanini Simba ikishinda yeye km msemaji wa timu huwa anajitokeza na kuelezea? Lazima ifike mahali tuukubali ukweli, tuwe wawazi! Zama za kujisifia tunapofanya vizur na kukaa kimya tunapoboronga, haitujengi!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo ni sawa kabisa kiongozi, mimi nimeshangaa critic ya mchangiaji aliyempinga Haji kwa kumwita zeruzeru.

Vv

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Alaaa! Kumbe siku hizi mna vyeo kama vya CCM
Mbona unataka kutoka nje ya mada? Moja ya kazi ya Ofisa habari ni kuhamasisha watu wake waipende timu na kuipa sapoti, na hamasa ya mashabiki ndio inayovutia wawekezaji na wadhamini kujitokeza. Kampuni gani itapenda kuidhamini timu ambayo hakuna watu wanaohamasika kuitazama na hivyo kutazama matangazo ya biashara? Leo hata washabiki wa Yanga wanafuatilia kwa makini sana ligi ya mabingwa wa Afrika katika kundi la Simba, na wanaweza hata kukupangia msimamo wa kundi ulivyo kutoka kichwani. Yote hayo ni kwa sababu ya hamasa ya klabu. Unaweza ukajikuta hata wewe unamfuatilia Manara zaidi kuliko hata Dismas Ten!
 
Kwanini Simba ikishinda yeye km msemaji wa timu huwa anajitokeza na kuelezea? Lazima ifike mahali tuukubali ukweli, tuwe wawazi! Zama za kujisifia tunapofanya vizur na kukaa kimya tunapoboronga, haitujengi!
Ingekuwa vizuri kama ungeweka ushahidi kuwa alizungumzia masuala ya kiufundi siku fulani ambayo Simba ilishinda. Mfano labda Manara amesema Simba imeshinda kwa kuwa ilibadili mfumo na kuwa 3-5-2 kwa kujaza viungo wengi. Au labda Manara amesema Simba imeshinda kwa kuwa Okwi alielekezwa awe anashambulia kwa kutokea upande wa kushoto lakini akichezea zaidi upande wa chini kuja kupokea mipira ya Mkude na Kotei
 
Kweli kabisa, na ukiona club imeshinda utaona atakavyojitapa, lakini club ikifungwa, KIMYAAAAAAA
Katika hali ya kawaida, hivi mtu anawezaje kujitapa baada ya kufungwa? Mbona kama watu siku hizi hawaeleweki eleweki hivi humu?
 
Kwanza acha izo fikra potofu! Nawe unaweza ukazaa mtu wa aina hyo
Tatizo hujui Kiswahili wala Kingereza .
Albino ni Kingereza. Zeruzeru ni Kiswahili sanifu kabisa. Hatuna tusi, dharau au kejeli
 
Kwangu mimi Manara na Pierre wa Liquid Pub wanafanana tu. 5imba nayo ni sawa na Ndanda tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…