Haka kamjengo kanaweza kugharimu shilingi Ngapi?

Samahani wakuu, kwa wale wenye uzoefu na mambo ya ujenzi, je? Haka kamjengo kanaweza kugharimu sh. Ngapi hadi kanaisha?
View attachment 872767View attachment 872768

ukiweza kuweka vipimo ata roughly, wakuu wataweza kukadiria vizuri zaidi. na partitions za ndani zikoje?
japo kwa macho imekaa kama mita 6 kwa 3 jumla.. ujenzi halisi itakua kati ya 5-7mil. haiwezi kua chini ya 3. na ikizidi 8 umepigwa.
 
ukiweza kuweka vipimo ata roughly, wakuu wataweza kukadiria vizuri zaidi. na partitions za ndani zikoje?
japo kwa macho imekaa kama mita 6 kwa 3 jumla.. ujenzi halisi itakua kati ya 5-7mil. haiwezi kua chini ya 3. na ikizidi 8 umepigwa.
Mkuu tuchukulie ndani hakujasakafiwa wala rangi haijapigwa. Kifupi nataka nijenge kibanda cha kijana nitake muweka site mkuu
 
Mkuu umejibu ukiwa na usingizi
Yupo sahihi sana. Nimejenga kubwa ya hapo kwa 1.5m ila kuezeka nikapiga "slope" kama wengi wanavyoita ya mita 3x9. Makadirio mengi ya watu hapa ni nadharia tuu. Kwenye ujenzi unaweza tishwa hadi ukaogopa kuanza. Unamuuliza mtu nyumba yako hii umejenga kwa sh ngapi anakwambia million 150 kumbe hata 30m haifiki.
 
Ukisimamia ujenzi mwenyewe milion 3 zinatosha.

Kama unamtumia fundi pesa ananunua material yeye andaa miluon 4 mpaka 4.5
 
Kwa mwonekano wa hako kadirisha inaelekea kuna choo humo ndani... Afu umesahau nondo hapo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…