Haka kamjengo kanaweza kugharimu shilingi Ngapi?

Umesahau lkumtajia bei ya kila kitu... nadhani umehofia kumkatisha tamaa... maana unaweza kuta labda alikuwa ma 1M akadhani itamtoa
Sijasahau ila unajua kila mtu na uwezo wake, wengine wa nanunua vitasa vya elfu sita wengine vya laki na nusu, kwahyo apige hesabu kwa level yake
 
Sijasahau ila unajua kila mtu na uwezo wake, wengine wa nanunua vitasa vya elfu sita wengine vya laki na nusu, kwahyo apige hesabu kwa level yake
Hapo sawa....

Ila kwa aina ya mjengo anaoutaka, ukiitathmini nyumba kwenye hiyo picha lazima atakuwa na uwezo wa kujenga mjengo wa kuungaunga...
 
Chumba ni kipi na sebule ni ipi hapo? Maanake naona dirisha moja mbele,moja nyuma na kadirisha kamoja kadogo pembeni. Hako kadirisha kadogo ndio ka chumbani?
 
Chumba ni kipi na sebule ni ipi hapo? Maanake naona dirisha moja mbele,moja nyuma na kadirisha kamoja kadogo pembeni. Hako kadirisha kadogo ndio ka chumbani?
Itakuwa chumba na choo cha ndani
 
Laki 8 hadi chenchi inabaki sababu hako kanyumba hakazidi tofali 350 endapo utanunua tofali moja kwa 1500 hivyo kwa tofali 350 za block itakugharimu laki 5 na 25 elfu,bati 16 futi 3 ambapo kama ni Dar haizidi laki 2 ,mifuko ya sement 15 ambayo haizidi Sana laki 2, mbao 14 za kenchi Unaweza kutumia laki 1 na kidogo au chini ya laki moja misumali ya bati pamoja na kupigia Kenchi haizidi elfu 30,Madirisha ya kioo,rangi ya nyumba,mfumo wa maji na Umeme pamoja na malipo ya fundi angalau isipungue mil 2

Kama ni nyumba unayojenga kwaajili ya kuishi inabidi iwe imekamilika hata kama ni ndogo inachumba kimoja na choo yaani Umeijenga kama self contained hivyo haitakiwi kukosa vitu hivyo ili ufurahie japo kajumba ni kadogo.
 
Tatizo hujasema kama ni nyumba ya kuishi au Jiko au Stoo lakini kwa muonekano wa picha hiyo nyumba hiyo imetumia kati ya bati 8-10 ni ndogo kidogo labda umejenga kulingana na uwezo wako lakini ingefaa kama ungeongeza kidogo japo ingekuwa yenye bati kati ya 10-12 angalau iwe na size nzuri kidogo ninasema hivyo kwakua nimeona jamaa mmoja kajenga kanyumba Kenya ukubwa huo alafu ni self contained kaweka dirisha mmoja kubwa na chooni kuna dirisha lenye size nzuri,umeme maji na amekapiga rangi kanapendeza sana japo kwa haraka haraka unaweza kudhani ni Jiko la kisasa lakini mtu anaishi vizuri tu kama wew ni bachelor lakini
 
Naomba mchanganuo mkuu
acha uvivu
haya bana
  1. tofari 1200 -1300 kwa bei ya kununua 1200,000/- -1,300,000
  2. saruji ya kujengea matofari 50 kwa mfuko mifko 26 kama 390,000
  3. mabati 20 kila bati 15,000 jumla 300,000
  4. mailisha kama hayo 200,000/-
  5. mbao 150,000
  6. lipu saruji na fundi 400,000
  7. sakafu ya chini 300,000
  8. ufundi wote 700,000/-
  9. maji yote 120,000
  10. mlango na rangi 500,000
  11. usafiri na matumizi mengine 140,000
 
Hakuna asiyependa kuonekana ametumia gharama kubwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…