Haka kamjengo kanaweza kugharimu shilingi Ngapi?

Haka kamjengo kanaweza kugharimu shilingi Ngapi?

Umesahau lkumtajia bei ya kila kitu... nadhani umehofia kumkatisha tamaa... maana unaweza kuta labda alikuwa ma 1M akadhani itamtoa
Sijasahau ila unajua kila mtu na uwezo wake, wengine wa nanunua vitasa vya elfu sita wengine vya laki na nusu, kwahyo apige hesabu kwa level yake
 
Sijasahau ila unajua kila mtu na uwezo wake, wengine wa nanunua vitasa vya elfu sita wengine vya laki na nusu, kwahyo apige hesabu kwa level yake
Hapo sawa....

Ila kwa aina ya mjengo anaoutaka, ukiitathmini nyumba kwenye hiyo picha lazima atakuwa na uwezo wa kujenga mjengo wa kuungaunga...
 
Hapo ni chumba na sebule, max ni tofali 1000 kuanzia msingi hadi juu, bati sita kila upande jumla 12, milango miwili, madirisha mawili, mbao 4×2 sita na 2×2 nane, mchanga Lori na kokoto nusu lori, cement mifuko 20, vitasa viwili, komeo mbili za ndani, misumari ya bati kilo2 na ya 4" kilo2, bawaba za milango 6, mafuta gharama yà kila kimoja hapo jumlisha usisahau hela ya fundi sijui vinasimamia ngapi vitu hivyo
Chumba ni kipi na sebule ni ipi hapo? Maanake naona dirisha moja mbele,moja nyuma na kadirisha kamoja kadogo pembeni. Hako kadirisha kadogo ndio ka chumbani?
 
Chumba ni kipi na sebule ni ipi hapo? Maanake naona dirisha moja mbele,moja nyuma na kadirisha kamoja kadogo pembeni. Hako kadirisha kadogo ndio ka chumbani?
Itakuwa chumba na choo cha ndani
 
Laki 8 hadi chenchi inabaki sababu hako kanyumba hakazidi tofali 350 endapo utanunua tofali moja kwa 1500 hivyo kwa tofali 350 za block itakugharimu laki 5 na 25 elfu,bati 16 futi 3 ambapo kama ni Dar haizidi laki 2 ,mifuko ya sement 15 ambayo haizidi Sana laki 2, mbao 14 za kenchi Unaweza kutumia laki 1 na kidogo au chini ya laki moja misumali ya bati pamoja na kupigia Kenchi haizidi elfu 30,Madirisha ya kioo,rangi ya nyumba,mfumo wa maji na Umeme pamoja na malipo ya fundi angalau isipungue mil 2

Kama ni nyumba unayojenga kwaajili ya kuishi inabidi iwe imekamilika hata kama ni ndogo inachumba kimoja na choo yaani Umeijenga kama self contained hivyo haitakiwi kukosa vitu hivyo ili ufurahie japo kajumba ni kadogo.
 
Tatizo hujasema kama ni nyumba ya kuishi au Jiko au Stoo lakini kwa muonekano wa picha hiyo nyumba hiyo imetumia kati ya bati 8-10 ni ndogo kidogo labda umejenga kulingana na uwezo wako lakini ingefaa kama ungeongeza kidogo japo ingekuwa yenye bati kati ya 10-12 angalau iwe na size nzuri kidogo ninasema hivyo kwakua nimeona jamaa mmoja kajenga kanyumba Kenya ukubwa huo alafu ni self contained kaweka dirisha mmoja kubwa na chooni kuna dirisha lenye size nzuri,umeme maji na amekapiga rangi kanapendeza sana japo kwa haraka haraka unaweza kudhani ni Jiko la kisasa lakini mtu anaishi vizuri tu kama wew ni bachelor lakini
 
Naomba mchanganuo mkuu
acha uvivu
haya bana
  1. tofari 1200 -1300 kwa bei ya kununua 1200,000/- -1,300,000
  2. saruji ya kujengea matofari 50 kwa mfuko mifko 26 kama 390,000
  3. mabati 20 kila bati 15,000 jumla 300,000
  4. mailisha kama hayo 200,000/-
  5. mbao 150,000
  6. lipu saruji na fundi 400,000
  7. sakafu ya chini 300,000
  8. ufundi wote 700,000/-
  9. maji yote 120,000
  10. mlango na rangi 500,000
  11. usafiri na matumizi mengine 140,000
 
Yupo sahihi sana. Nimejenga kubwa ya hapo kwa 1.5m ila kuezeka nikapiga "slope" kama wengi wanavyoita ya mita 3x9. Makadirio mengi ya watu hapa ni nadharia tuu. Kwenye ujenzi unaweza tishwa hadi ukaogopa kuanza. Unamuuliza mtu nyumba yako hii umejenga kwa sh ngapi anakwambia million 150 kumbe hata 30m haifiki.
Hakuna asiyependa kuonekana ametumia gharama kubwa.
 
Back
Top Bottom