Haki ya Kuishi ya Watanzania na Hofu Inayotanda

Haki ya Kuishi ya Watanzania na Hofu Inayotanda

Gellangi

JF-Expert Member
Joined
Apr 11, 2016
Posts
2,782
Reaction score
3,018
Ndugu zangu Watanzania wenzangu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,Nawasalimu kwa dhati.Pia nawapa pole wote waliotangulia mbele ya Muumba wao kwa vifo vya kinyama vilivyotokea.Mungu awape ujasiri wafiwa.

Pia bila kuwasahau wagonjwa, wafungwa & mahabusu (Hakuna aliye salama sana).

Nikirejea mada hapo juu; Ukisikiliza minong'ono na mijadala ya wazi au mitandaoni,unagundua kuwa vilio vimezidi.Mifano ipo mingi maana kuna vilio vya Uchumi mgumu,Tozo zilizokithiri,mauaji na utekaji wa Wananchi wenzetu.

Sakata la Serengeti limeniogopesha sana. Walianza na wanasiasa, wafanyabiashara, wasanii, Wamasai wa Ngorongoro na sasa ni zamu ya Panya Road, Majambazi na Udhalilishaji wa wanawake au wanaume.

Maovu haya yanaelekezwa zaidi kwa Serikali, POLISI na watawala wa CCM. Hofu ni kubwa mno.

Je, haya yamebarikiwa hapa Tanganyika? Je, nani wa kuwajibika kuhusu madhila haya?

Tudai Katiba Mpya ya Wananchi ili tuikomboe nchi yetu isiingie machafukoni.

Mwenye macho....
 
Je,shughuli za mahakama zitakuwa nini kama wahalifu au watuhumiwa watauliwa na POLISI?Je,kuna kipengele cha Sheria kinachoruhusu watuhumiwa kulawitiwa au kubakwa kama sehemu ya torture?Je,utesaji umeruhusiwa kwenye PGO ipi?
Watanzania wenye kuipenda nchi yetu tukatae na kupinga uonevu wa wananchi wenye nchi ndani ya nchi yao.
 
Ndugu zangu Watanzania wenzangu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar,Nawasalimu kwa dhati.Pia nawapa pole wote waliotangulia mbele ya Muumba wao kwa vifo vya kinyama vilivyotokea.Mungu awape ujasiri wafiwa.
Pia bila kuwasahau wagonjwa,wafungwa&mahabusu(Hakuna aliye salama sana).
Nikirejea mada hapo juu;
Ukisikiliza minong'ono na mijadala ya wazi au mitandaoni,unagundua kuwa vilio vimezidi.Mifano ipo mingi maana kuna vilio vya Uchumi mgumu,Tozo zilizokithiri,mauaji na utekaji wa Wananchi wenzetu.
Sakata la Serengeti limeniogopesha sana.Walianza na wanasiasa,wafanyabiashara,wasanii,Wamasai wa Ngorongoro na sasa ni zamu ya PanyaRoad,Majambazi na Udhalilishaji wa wanawake au wanaume.
Maovu haya yanaelekezwa zaidi kwa Serikali,POLISI na watawala wa CCM.
Hofu ni kubwa mno.
Je,haya yamebarikiwa hapa Tanganyika?Je,nani wa kuwajibika kuhusu madhila haya?
Tudai Katiba Mpya ya Wananchi ili tuikomboe nchi yetu isiingie machafukoni.
Mwenye macho....
Tanganyika ni nchi gani au wilaya?ukitaka Tanganyika irudi hamasisha wananchi wadai katiba yao na hasa vijana ambao mpaka sasa ndo tegemeo kisiasa,kiuchumi na kijamii.
 
Hivi ni kwa nini waliopewa jukumu la kuilinda Katiba wanaivunja?Je,ni ngumu kiasi gani kwa vyombo vya dola kutenda Haki,kujali Utu na kuhakikisha Sheria zinazingatiwa?
 
Tanganyika ni nchi gani au wilaya?ukitaka Tanganyika irudi hamasisha wananchi wadai katiba yao na hasa vijana ambao mpaka sasa ndo tegemeo kisiasa,kiuchumi na kijamii.
Umeuliza kama vile haufahamu jibu.Tanganyika ni nchi Huru iliyopata Uhuru toka Uingereza tarehe 09/12/1961.
Kuipa wilaya jina la nchi siyo tatizo lakini Tanganyika kupotezwa-HAPANA.
Hiyo Katiba Mpya tumeidai tokea 1990 hadi sasa.Wananchi wanataka Katiba Mpya ila CCM wanajidai hawataki na wanatuchelewesha.
Hakika nakualika kusherehekea Katiba Mpya punde.Haizuiliki tena,watakimbiana siyo muda mrefu ujao.
Ingelikuwa Bora kukubali ili tuwe nao pamoja kwenye Safina ya Tanganyika,Zanzibar na hatimaye tuingie Tanzania.Jiulize;nawe utakuwemo?
 
Watu wanauliwa,wanatekwa,wanalawitiwa au kubakwa na vyombo vya dola nasi tunadhani ni sawa?Tanzania ni kisiwa cha amani bado?
Huwa najiuliza;Nani hapa nchini akionewa,kunyanyaswa na au kudhalilishwa na waajiriwa wa wananchi ndipo tuamke usingizini?
Inasikitisha kuwa yanapokuwa masuala ya vyama na udaku server ingesheheni replies.Ila poa tu,mchumia juani....
 
Bado tupo nyuma sana, kama tunashangilia baadhi yetu kuporwa hakinzao za kuishi, maana yake tunajiandaa nasi kuporwa haki yetu ya kuishi pale muda wetu utakapofika.

Kwasababu hatuna uhakika kama hao wanaouliwa na polisi ni majambazi kweli au vinginevyo, basi tujiandae kuizoe tabia ya watuhumiwa kufia mikononi mwa polisi ambayo hatujui mwisho wake utakuwa upi kwa upande wetu.
 
Bado tupo nyuma sana, kama tunashangilia baadhi yetu kuporwa hakinzao za kuishi, maana yake tunajiandaa nasi kuporwa haki yetu ya kuishi pale muda wetu utakapofika.

Kwasababu hatuna uhakika kama hao wanaouliwa na polisi ni majambazi kweli au vinginevyo, basi tujiandae kuizoe tabia ya watuhumiwa kufia mikononi mwa polisi ambayo hatujui mwisho wake utakuwa upi kwa upande wetu.
Ahsante kwa kuliona hilo denooJ.Maajabu ya wenyenchi yao Watanganyika wamejisalimisha Haki zao za Kuishi,Kijamii,Kiuchumi,Kiraia na zingine zote kwa CCM na Serikali yake huku ushahidi wa wazi ni kuwa hao CCM wanajinufaisha peke yao(wameshindwa kula na kipofu) wanakomba chakula chote.
Ajabu nyingine ni hawa wenyenchi yao ya Tanganyika hawana uthubutu wa kudai Haki zao,wanawashangilia na kuwapongeza watesi wao.Tumesahau kuwa Haki haiombwi bali hupiganiwa na kutafutwa-Nothing is for granted.
Tudai na kuandika Katiba Mpya ya Wananchi wa Tanzania ya Tanganyika na Zanzibar sasa ili kuwanusuru wenyenchi Wananchi.
 
Haya wanaouuwa sasa hivi wanajulikana maana mlikuwa mnalalamika wasiojulikana.
 
Haya wanaouuwa sasa hivi wanajulikana maana mlikuwa mnalalamika wasiojulikana.
Hawakuwahi kutojulikana,wamejitahidi kuwaongopea wasioelewa ila kwa werevu walijulikana hata kabla ya kutenda.
Pembe la Ng'ombe....
 
Stop Police Brutality in Tanzania as soon as possible.
 
Back
Top Bottom