Haki yangu kikatiba ya kushawishi/hamasisha wamuongezee muda Rais Magufuli

Status
Not open for further replies.

JERUSALEM 2006

JF-Expert Member
Joined
Apr 23, 2012
Posts
527
Reaction score
596

1. Katiba ya Jamuhuri wa Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 na marekebisho yake ya 30th April 2000 yananipa haki zote kama raia halali wa Taifa la Tanzania kuwa na mawazo huru juu ya jambo lolote ambalo halivunji sheria za nchi yetu.

Mimi kama Mtanzania tarehe 16 Februari 2020 nilianzisha uzi unaosema "KARIBU TUJIUNGE NA KUNDI LA MAGUFULI TENA 2025" na mjadala katika kundi hili ulikuwa unaendelea. Kwa bahata mbaya sana.

2. Katiba ya jamhuri ya Tanzania ( 1977) kuanzia ibara ya18 (UHURU WA MAONI) , ibara ya19 ( UHURU WA MTU KUSHIRIKIANA NA MTU MWINGINE) kwa pamoja zinasema

Ibara 18.1 Bila kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake,na kutafuta,kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila kujali mipaka ya nchi, na pia ana uhuru mawasilano yake kutoingiliwa kati.

Naomba nielezee ibara hii ya 18.1; ni kwamba nina uhuru wa kutoa mawazo yangu yoyote, katika chombo chochote ikiwemo Jamii Forums, bila kuingiliwa na yeyote.

Ibara 20.1 Kila mtu anastahili kuwa Huru, bila ya kuathiri Sheria za Nchi, kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani, kuchanyika, na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo hadharani, na hasa zaidi kuanzisha au kujiunga na vyama au mashirika yaliyo anzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo.

Nia yangu ni thabiti, ni kuanzisha mchakato wa kubadirisha Katiba kwa kukusanya signatures zaidi ya million tano za wa Tanzania ili kuweza kukidhi matakwa ya kikatiba ya kumuongezea angalau muhala mwengine Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli,

KAULI MBIO YETU NI.

"H.E President Magufuli is too valuable to retire, Tanzanians needs him now more than ever" " Mhe, Rais Magufuli ni wathamani sana kustaafu, Watanzania wanamuhitaji sasa kuliko kipindi kingine chochote"

MWISHO

Kama nilivyo quote vipengele vya katiba, basi naomba mawazo yangu yaheshimiwe. Situkana, sijapanga kuua, wala sija panga kuvunja sheria za Nchi, ninafuata taratibu zote ili kubarisha vipengere vya Katiba ambayo siyo Msaafu wala siyo Bibilia.
 
Upvote 3

Sasa mimi nimesema Corona haipo nchini?

Cha msingi wewe jilindi uwezavyo.
 
Muarubaini wenu ni kuwa na utawala wa kimla , au?
 
Sasa mimi nimesema Corona haipo nchini?

Cha msingi wewe jilindi uwezavyo.
Nijilinde kwanini wakati corona haipo nchini? Mkuu acha kuchezea roho za watu, uhai wa mtu kitu muhimu kuliko hicho unacho kiabudu na kukilinda .

Ukiacha watu wakifa na kuteketea hata hizo barabara hazina faida .

Huo umeme unaosema wewe[emoji3] hauna faida

Uhai wa wanachi kwanza halafu ndio ndege na barabara pamoja kuabudu na kusifu kuendelee

Mungu ibariki tanzania Mungu ibariki Africa na Dunia kwa ujumla .
 
Umeeleweka
 

Wewe kwa maoni yako ungekuwa Rais ungechukua hatua gani ambazo ni bora zaidi ili kuokoa maisha ya watu.
 
Ukiona unapata hasira kwa mawazo mbadala ya mwenzako, sasa huo ndio ujinga wa kifikra.

Tunaita lack of political tolerance. Au political vandalism.
Basi waambie wenzio wamwachie askofu
 
Naona Wazi Wazi Wazi Wazi Wazi
Atatawala Milele
Ushauri Sasa Tafuteni Construction Company
Itengeneze Kiti Cha Zege, Ili Akikaa Ndiyo Hatoki
 
Katiba ya nchi inasemaje kuhusu ukomo wa urais?

Na kama unapingana na katiba huoni kama unavunja sheria?
Ndugu tanua akili yako usipende kupanua nanihii..
Si kweli kwamba kufanya mabadiliko ya baadhi ya vipengele vya katiba ni kuvunja katiba au kutoiheshimu katiba..
Katiba yenyewe imeruhusu kufanyiwa mabadiliko kama watu wameona kuna haja ya kufanya hivyo.. kikubwa taratibu zifuatwe.
Ni kwa msingi huohuo leo hii kuna vuguvugu kama;
1. Kudai tume huru
2. Matokeo ya Urais kuhojiwa mahakamani
3. Kumpunguzia Rais madaraka
4. Nk nk.
Mambo haya na MENGINE MENGI SANA yanayodaiwa kuathiri ustawi wa demokrasia uhuru na haki za raia mpaka leo yamo ndani ya katiba yetu inayotuongoza sasa. Na Baadhi ya Watanzania wanataka yafanyiwe marekebisho. Labda tungekubaliana hapa kwamba chochote kilichomo ndani ya Katiba kisiguswe abadani hivyo atakayedai tume huru haki ya kuhoji matokeo au kupunguza madaraka ya Rais ahesabiwe hajaiheshimu katiba iliyopo kama yule anayedai tuongeze au tuondoe ukomo wa Urais. SIMPLE.

Nafikiri tujenfe hoja kuhusu namna inakuwa Rahisi kufanya mabadiliko ya Katiba kwa mambo ambayo yana maslahi na viongozi waliopo na jinsi inakuwa vigumu kufanya hivyo kwa mambo ambayo yako kinyume nao.
 
Mkuu upo duniani ? Vp Corona ipo Tanzania au hamna ? Sitaki kubishana leo nakujulia hali tu ndugu yangu[emoji3][emoji3]
 
katoka nduki korona inatafuna inner circle ya mfale juha...
Watanzania ni wamoja , upendo kwetu ni asili ndio maana nikasema nimjulie hali ndugu yetu huyu, pamoja na mchalato wake wa kubadili katiba .

Hakujua kuna maswala ya muhimu kuzungumzia kuliko katiba katika kipindi hichi.
 
Watanzania ni wamoja , upendo kwetu ni asili ndio maana nikasema nimjulie hali ndugu yetu huyu, pamoja na mchalato wake wa kubadili katiba .

Hakujua kuna maswala ya muhimu kuzungumzia kuliko katiba katika kipindi hichi.

kabisa , me huwa nasema kitu kimoja yan kama nchi tunashindwa kuset priorities na mfumo hauruhusu mawazo mbadala, atakachosema mtu mmoja ndio sheria, hali ni mbaya sana
 
Naona Wazi Wazi Wazi Wazi Wazi
Atatawala Milele
Ushauri Sasa Tafuteni Construction Company
Itengeneze Kiti Cha Zege, Ili Akikaa Ndiyo Hatoki
Hizo kufuru zake zilimuudhi Mungu, akamtanguliza ahera. Shetani mkubwa Mwendazake
 
Mtoa mada japo alitumia haki yake kikatiba lakini alikuwa anawakilisha kundi la Watanzania wapumbavu sana.

Magufuli mwenywe alikuwa spanna mkononi ndiyo ulikuwa unataka aongezewe muda. Jitu linaumwa UKIMWI toka miaka ya 1990s, limewekewa betri kufuani, lina diabetes halafu ni Bipolar lisingeweza kukatiza kwenye upepo wa COVID19
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…