King 999
JF-Expert Member
- Aug 15, 2019
- 5,872
- 8,374
lengo la kuleta huu uzi ni lipi?Zamani nilidanganywa kwa kuambiwa kuwa ukiwa na pesa utapata kila kitu, kweli nikapambana na nikafanikiwa kwa kiasi chake.
Ki ufupi nimewekeza kwenye biashara zisizofilisika. Na kwa siku napata laki nane hadi tisa (hiyo ni faida kwa kila siku).
Ila kinachonishangaza nimejikalia tuu nyumbani nacheza na kuku,mabata mzinga na kanga.
Kuna saa naweza kubeba milioni kama ishirini hivi nikazirusha zikasambaa chumbani ili angalau nipate kazi ya kuziokota na kuanza kuzihesabu tena.
Eti naweza kuwa nimelogwa? Au ni kawaida