Mwanasayansi Kalivubha
JF-Expert Member
- Feb 4, 2024
- 344
- 926
Maisha ya ajira yanafanana na ndoa , kwenye ndoa kila siku watu watu wanatamani kuingia huko mpaka kwenda kwa waganga ila wanasahau kitu kimoja ambacho ni kujiandaa kuishi ndani ya ndoa hiyo na kwenye ajira kila siku watu hutafuta kazi ila wanasahau kuwa kuna siku wataishi bila hiyo kazi.
Unapotafuta kazi usisahau pia kuna siku utaishi bila hiyo kazi hivyo hali uliyonayo kabla ya kupata kazi inaweza kujirudia siku utapoanza kuishi bila hiyo kazi kama tu utashindwa kujiandaa vizuri.
Yawezekana pasiwe na kanuni ya kuishi maisha ya ajira ila la msingi ukifika kwenye ajira hakikisha unatengeneza tena ajira nyingine itayokupa mshahara wa ziada na ukifanikisha hilo basi utakuwa na vigezo vyote vya kuitwa mstaafu atakayefurahia mapumziko yake.
Upo kwenye ajira kwa muda gani? Je mshahara ukisimama sasa utaweza kuishi kwa muda gani bila kuingia kwenye madeni?
Jitahidi uwe na uwezo wa kuishi miezi sita bila mshahara na usiathirike na hicho ndio kipimo kikubwa kuwa umejiandaa vyema kustaafu.
Unapotafuta kazi usisahau pia kuna siku utaishi bila hiyo kazi hivyo hali uliyonayo kabla ya kupata kazi inaweza kujirudia siku utapoanza kuishi bila hiyo kazi kama tu utashindwa kujiandaa vizuri.
Yawezekana pasiwe na kanuni ya kuishi maisha ya ajira ila la msingi ukifika kwenye ajira hakikisha unatengeneza tena ajira nyingine itayokupa mshahara wa ziada na ukifanikisha hilo basi utakuwa na vigezo vyote vya kuitwa mstaafu atakayefurahia mapumziko yake.
Upo kwenye ajira kwa muda gani? Je mshahara ukisimama sasa utaweza kuishi kwa muda gani bila kuingia kwenye madeni?
Jitahidi uwe na uwezo wa kuishi miezi sita bila mshahara na usiathirike na hicho ndio kipimo kikubwa kuwa umejiandaa vyema kustaafu.
Upvote
5