Hakuna aliye juu ya sheria

Hakuna aliye juu ya sheria

enk

Member
Joined
Jan 11, 2012
Posts
87
Reaction score
12
Ni msemo mzuri na wenye maana yake inayojipambanua. Lakini ktk uhalisia ni kwamba kuna watu wako juu ya sheria hasa hapa TZ.
Kwa namna walivyojipanga na kuzitafasiri sheria mbalimbali, wameifunika sentensi hiyo kwa manufaa yao hao wachache na wengine watakaokuwa karibu nao. Hawa hakika hawaguswi wala kuhojiwa utendaji wao. Wako juu zaidi ya mkuu wa nchi, ambaye anaweza kulalamikiwa hadharani na hata kushitakiwa akitoka madarakani. Wao hilo haliwagusi ni Miungu Watu hao. Ktk umri wangu sijawahi kusikia wameshitakiwa ndani na nje ya muda wao kazini. Ila wao wanaweza kushitaki ndanina nje ya muda wao kazini.

Miungu hawa wanao uwezo wa kuamua namna ya baadae ama hatima ya mtu, watu ama jamii fulani. Ni bora sana wangeyafanya haya ki uhalali, lakini tofauti ni kuwa usemi wa "SHERIA NI MSUMENO" HUTUMIKA KWA MANUFAA YA UPANDE MMOJA UTAKAOWAHI. Maamuzi hutolewa tena kwa mzunguko mreefu mwishoni kabisa MNYONGE INAKULA KWAKE.

Nafunguka kuwa miungu hawa ni MAJAJI. Na hii ipo hasa TZ. JAJI wa mahakama hapa kwetu ana nguvu ya kuipeleka kesi kwa kadri apendavyo yeye "binafsi" hakuna wa kumsukuma afanye kama ambavyo serikali yaweza sukumana kwa kushushiana nyundo na watu kuwajibishana na jambo likaenda.
Kwa majaji wetu hata kama kilichoko mbele yao kina hatari ya kuoza, hawajali, wanayo majibu tayari waliyoyahalarisha ya kutokufanyakazi.
Lakini kila kitu kina kinyume chake. Dharura za kuahirisha kesi zina nafasi kubwa sana kuliko nafasi za kusikiliza kesi.
Nawashukuru na kuwapongeza wale waliojitahidi kuwa kama PILATO, wao hunawa maji mapema na kujitoa kwenye zile zinazoashiria haki kupindwa kwa njia mbadala. Wapo waliojiweka kando na mambo haya na tangu kuwa Majaji hadi kustaafu hawakuwahi kutoa hukumu labda ya jopo. Na huo ndo ukweli! Kesi yoyote tangu inaanza viashiria vya ukweli wa jambo huwa vipo ila mahakama zetu hutoa nafasi ya muda watu kuzidiana ujanja na mara zote maskini ndo wanaoumia.
SIKUSEMA YOTE HAYA KAMA MUATHIRIKA ILA KWA MTAZAMO WANGU KWA YALE NIYAONAYO.
MAJAJI TANZANIA YETU NI MIUNGU NA WAKO JUU YA SHERIA. Mwenye ku oppose hili karibu
 
Ni msemo mzuri na wenye maana yake inayojipambanua. Lakini ktk uhalisia ni kwamba kuna watu wako juu ya sheria hasa hapa TZ.
Kwa namna walivyojipanga na kuzitafasiri sheria mbalimbali, wameifunika sentensi hiyo kwa manufaa yao hao wachache na wengine watakaokuwa karibu nao. Hawa hakika hawaguswi wala kuhojiwa utendaji wao. Wako juu zaidi ya mkuu wa nchi, ambaye anaweza kulalamikiwa hadharani na hata kushitakiwa akitoka madarakani. Wao hilo haliwagusi ni Miungu Watu hao. Ktk umri wangu sijawahi kusikia wameshitakiwa ndani na nje ya muda wao kazini. Ila wao wanaweza kushitaki ndanina nje ya muda wao kazini.

Miungu hawa wanao uwezo wa kuamua namna ya baadae ama hatima ya mtu, watu ama jamii fulani. Ni bora sana wangeyafanya haya ki uhalali, lakini tofauti ni kuwa usemi wa "SHERIA NI MSUMENO" HUTUMIKA KWA MANUFAA YA UPANDE MMOJA UTAKAOWAHI. Maamuzi hutolewa tena kwa mzunguko mreefu mwishoni kabisa MNYONGE INAKULA KWAKE.

Nafunguka kuwa miungu hawa ni MAJAJI. Na hii ipo hasa TZ. JAJI wa mahakama hapa kwetu ana nguvu ya kuipeleka kesi kwa kadri apendavyo yeye "binafsi" hakuna wa kumsukuma afanye kama ambavyo serikali yaweza sukumana kwa kushushiana nyundo na watu kuwajibishana na jambo likaenda.
Kwa majaji wetu hata kama kilichoko mbele yao kina hatari ya kuoza, hawajali, wanayo majibu tayari waliyoyahalarisha ya kutokufanyakazi.
Lakini kila kitu kina kinyume chake. Dharura za kuahirisha kesi zina nafasi kubwa sana kuliko nafasi za kusikiliza kesi.
Nawashukuru na kuwapongeza wale waliojitahidi kuwa kama PILATO, wao hunawa maji mapema na kujitoa kwenye zile zinazoashiria haki kupindwa kwa njia mbadala. Wapo waliojiweka kando na mambo haya na tangu kuwa Majaji hadi kustaafu hawakuwahi kutoa hukumu labda ya jopo. Na huo ndo ukweli! Kesi yoyote tangu inaanza viashiria vya ukweli wa jambo huwa vipo ila mahakama zetu hutoa nafasi ya muda watu kuzidiana ujanja na mara zote maskini ndo wanaoumia.
SIKUSEMA YOTE HAYA KAMA MUATHIRIKA ILA KWA MTAZAMO WANGU KWA YALE NIYAONAYO.
MAJAJI TANZANIA YETU NI MIUNGU NA WAKO JUU YA SHERIA. Mwenye ku oppose hili karibu
we umetumwa au wamekufunga, mbona una hasira sana?
 
pole sana rafiki yangu maana hujajua tu kuwa moja mihimili ya katiba yetu ni uhuru wa mahakama hivyo katika uhuru mahakama kuna kipengele kinachowapa kinga majaji kutoshitakiwa katika utendaji wa kazi zao na pia kutoingiliwa wakati wa kutimiza kazi zake.pia kumbuka kila sheria ina isipokuwa zake mfano wenye matatizo akili,watoto chini ya miaka 11,wanadiplomasia,rais wa nchi hao wote wamepewa kinga ya kutoshitakiwa
 
Back
Top Bottom