Pre GE2025 Hakuna chama chochote cha siasa nchini Tanzania kilicho na sera Bora zaidi ya ACT Wazalendo

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Youda Fema

Member
Joined
Feb 2, 2024
Posts
70
Reaction score
63
Hakuna chama chochote Cha siasa nchini Tanzania kilicho na sera Bora zaidi ya ACT Wazalendo. Ndiyo chama pekee kilicho na sifa zifuatazo:

1. Kina azimio, linaloitwa Azimio La Tabora. CCM walikua na Azimio La Arusha, ila Sasa hawana.

2. Ndio chama pekee kinachoibua Changamoto za wananchi na kuzitolea Ufumbuzi wake.

3. Ni Chama pekee ambacho magufuli, alikisifia bungeni mwaka 2015 na 2020 kuwa viongozi wake hawana papara ya mambo, ila wanachakata mambo Kwa kina.

4. Ndio chama chenye mawaziri katika serikali Kwa 2020-2025 baada ya kuiondoa CUF katika nafasi yake, na chenyewe kushika hatamu Zanzibar.

5. ACT Wazalendo ni Chama kinachopokea wanachama wapya Kwa hoja, sio Kwa udanganyifu kama ilivyo chadema au Kwa ulaghai kama ilivyo CCM.

ACT Wazalendo; Taifa La Wote, Maslahi Kwa Wote, Mamlaka kamili.


 
Ni upuuzi tupu.

Tatizo lililopo Tanzania siyo vyama vya Siasa na Sera zao.
 
inawezekana vyama vyote vina wajususi wa ccm, maana ccm..
 
Hongera sana kwao, hawana propaganda, hawana kiki!!
 
Sera haiwezi kuwa bora kama haijawahi kutekelezwa. Huwezi kupima ubora kwenye maandishi.
Kimsingi CCM inashindwa kuwa na sera bora kwa sababu inachanganya sera za serikali na sera za chama. Huwezi kutenganisha sera za serikali na sera za CCM.
Ili CCM iwe na sera nzuri ambazo zinaweza kutuvusha, ni lazima waje na sera mbadala ambazo ni tofauti na zile za serikali. Hata kama zitakuwa zinaendana ila haziwezi kufanana kama kurwa na doto.
Kimsingi CCM haina sera bali inatumia sera za serikali kama sera za chama.
 
SHIDA nanyi mmekuwa kama wanafunzi mnategemea sana boom Toka serikalini nje na utaratibu pambaneni hata mikutano tu hakuna
 
Hili liko wazi na Kwa nini Iko hivi ni Kwa sababu ACT inatumia Wasomi wa Uchumi na pia kutafuta exposures ya wenye akili.

Huwa wanafanya Uchambuzi wa masuala Kwa undani na Kwa hoja zenyeashiko.
 
Ccmb
 
Wewe umesikia waapi ?
 
Shida siyo sera nzuri. Waongoza chama ni watu gani? Wote ni wasaliti ambao wanaweza change anytime dau likiwekwa mezani
 
Nimecheka sana baada ya kuona jina la mtoa uzi, kumbe Mzee wa miamala??
 
Shida siyo sera nzuri. Waongoza chama ni watu gani? Wote ni wasaliti ambao wanaweza change anytime dau likiwekwa mezani
Mbona kipindi zitto kabwe, anatoka chadema, CCM waliweka dau kubwa na wakamuahidi uwaziri mkuu, ila jamaa akachomoa ???
 
Nilipoona Jina lako tu nikaelewa uelekeo wa upeo wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…