Muarubaini
JF-Expert Member
- Apr 7, 2012
- 222
- 48
Mkurugenzi wa NSSF Dr Ramadhan Dau amesema Fao la kujitoa limeondolewa ili kuendana na mfumo wa kimataifa kwani duniani kote hakuna Fao la kujitoa.
Amesema hata Zanzibar na Kenya hakuna kitu kama hicho.
Mkurugenzi huyo alitoa tamko hilo alipokuwa akihojiwa na Kamati ya bunge ya mashirika ya umma inayoongozwa na Zitto Kabwe.
Source: ITV Habari
Jamani nna hasira sana na huyu jamaa anaitwa DAU
Jamani hivi mtu katoka mgodini(mwanafunzi), alikuwa anakatwa nssf naye asubiri miaka 60?
Mgodini wanafukuza na kuajiri kila siku,hao wachimbaji waliofukuzwa watapata lini mafao yao?
Je makampuni ya madini yana uwezekano wa kuendesha mgodi kwa miaka tajwa na nssf?
Kuna viongozi wanakuwa hawajui mazingira halisi ya wafanyakazi,na wakiendelea namsimamo wao ya RSA yatatokea TZ.
Mkurugenzi wa NSSF Dr Ramadhan Dau amesema Fao la kujitoa limeondolewa ili kuendana na mfumo wa kimataifa kwani duniani kote hakuna Fao la kujitoa.
Amesema hata Zanzibar na Kenya hakuna kitu kama hicho.
Mkurugenzi huyo alitoa tamko hilo alipokuwa akihojiwa na Kamati ya bunge ya mashirika ya umma inayoongozwa na Zitto Kabwe.
Source: ITV Habari
Huyu kilaza Dau ni janga sana kwa taifa letu na pia ana udini sana. Natamani 2015 ifike haraka ili tumuondoe hapo haraka sana.