Hakuna haki bila wajibu! Haki sio hisani ni stahiki inayopaswa kutolewa. Haki ya kufanya mikutano na maandamano ni haki kakini pia watimize wajibu

Hakuna haki bila wajibu! Haki sio hisani ni stahiki inayopaswa kutolewa. Haki ya kufanya mikutano na maandamano ni haki kakini pia watimize wajibu

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Kama kawa,

Ukiangalia nguvu iliyotumika jana kuzuia maandamano ya Chadema, nguvu hiyo ingetumika kuyalinda maandamano hayo badala ya kuyazuia!

Mada ya leo ni kuhusu haki, hakuna haki bila wajibu!, haki sio hisani ni stahiki inayopaswa kutolewa bila kuombwa. Haki ya kufanya mikutano na maandamano ni haki ya msingi ya vyama vya siasa, lakini pia vyama vina wajibu wa kufanya mikutano kwa amani na utulivu, wajibu wa kuhakiki amani na utulivu unakuwepo ni wajibu wa jeshi la Polisi, ndio maana vyama vinatakiwa kuiraifu Polisi mikutano na maandamano na ni jukumu la polisi kulinda amani kwenye mikutano hiyo na maandamano hayo, kitu cha ajabu kwenye maandamano ya jana, nguvu iliyotumika kuyazuia maandamano hayo ni kubwa ambayo ingetosha kabisa kuyalinda na Chadema wakaandamana kwa amani.

Haki sio hisani ya serikali, au jeshi la Polisi, haki ni stakihiki inayopaswa kutolewa bila kuombwa!. Haki haipaswi kuombwa, bali inapaswa kutolewa tuu, na isipotolewa haipaswi kuombwa bali inadaiwa, na ni katika kuidai huku sometimes hlazimika kugharimiwa kwa gharama za machozi, jasho na damu!.

Haki ya vyama vya siasa kufanya mikutano na maandamano, ni haki ya msingi, iheshimiwe, waandamaji wana wajibu wa kuandamana kwa amani na kuitunza amani, utulivu na usalama, wakati huo huo, jeshi la Polisi lina wajibu wa kulinda amani, hivyo linapopata taarifa za kiiteligensia kuwa maandamano hayo yana malengo ya kificho ya "Samia Must Go", then jeshi la Polisi lina wajibu wa kuyazuia.

Leo naomba kurejejelea zile makala zangu za Ijue Katiba ya JMT kwa jicho la Mtunga Katiba, alidhamiria nini alipoweka kifungu fulani cha katiba. Ili tuweze kwenda sambasamba, naomba tukumbushane Katiba ni Nini?. Katiba ni kakitabu kadogo tuu chenye kurasa 113!. Kakitabu haka ndio kila kitu kuihusu Tanzania yetu, hakuna yeyote aliye juu ya Katiba.

Katiba ni ya Kazi Gani. Katiba ndio msingi Mkuu na muongozo wa uendeshaji wa nchi yetu, ambapo sheria zote, taratibu zote na kanuni zote, za kufanya kila jambo, lazima zitokane na katiba.

Misingi ya Katiba- Katiba yetu imeweka misingi mikuu 4 ya katiba ambayo ni uhuru, haki, udugu na amani. Misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu.

Hii maana yake, hii misingi mikuu 4 ya katiba yetu ambayo ni uhuru, haki, udugu na amani, Serikali, Bunge na Mahakama, zina wajibu wa kutekeleza, huu ni wajibu na sio hisani!. Tofauti ya wajibu na hisani, wajibu ni lazima utekelezwe, sio ombi, wakati hisani, ni huruma tuu unaweza ukatekeleza au usitekeleze kadri wewe unavyoona.

Turejee kwenye hii katiba, Katiba ni ya Nani? Katiba hii imetungwa na Bunge maalum kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia.

Hivyo kwa mujibu wa katiba hii, kitu muhimu kabisa kwa Taifa la Tanzania, ni watu!, Watanzania, hawa ndio wenye katiba!, katiba ni mali ya Watanzania. Ni watu hawa Watanzania, walioweka misingi mikuu minne ya katiba yetu, uhuru, haki, udugu na amani. Msingi mkuu wa kwanza wa katiba yetu ni uhuru, wa pili ni haki. Hivyo vitu vitu viwili vikuu vya katiba yetu ni uhuru na haki.

Katiba yetu ya mwaka 1977, unavyo vifungu kadhaa vya haki, kwenye vifungu hivyo, kunazo haki kuu za msingi. Haki kuu ni haki ya uraia, kuwa Mtanzania ndio haki kubwa kuliko zote, na Mtanzania ndicho kitu muhimu kuliko kitu chochochote ndani ya katiba yetu. Huyu mwananchi ndie mwenye nchi, mwenye katiba, anayemuajiri rais wa JMT kwa kura yake na kumlipa mshahara yeye na serikali yake, Bunge na Mahakama kwa kodi yake hivyo mwananchi ndie kila kitu!.

Kuanzia Ibara ya 5 hadi Ibara ya 30, haki mbalimbali zimetajwa na wajibu pia umetajwa, hapa nakutajia Ibara na haki yake

5. Haki ya kupiga kura.
11. Haki ya kufanya kazi, kupata elimu, na nyinginezo.
12. Usawa wa Binadamu. 13.Usawa mbele ya sheria.
14. Haki ya kuwa hai.
15.Haki ya uhuru wa mtu binafsi.
16. Haki ya faragha na ya usalama wa mtu.
17. Uhuru wa mtu kwenda atakako.
18.Uhuru wa maoni.

19. Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo.
20. Uhuru wa mtu kushirikiana na wengine.
21. Uhuru wa kushiriki shughuli za umma.
22. Haki ya kufanya kazi. 23.Haki ya kumiliki mali. 24.Haki ya kupata ujira wa haki.
Pia katiba imeweka wajibu
25. Wajibu wa kushiriki kazini.
26. Wajibu wa kutii sheria za nchi.
27. Kulinda mali ya Umma.
28. Ulinzi wa taifa.
29. Haki na wajibu muhimu.

30. Mipaka kwa haki, uhuru na hifadhi kwa haki na wajibu.


Baada ya haki hizo za msingi ndani ya katiba yetu, zikatungwa sheria na kutoa haki za mikusanyiko, haki za kufanya mikutano, haki za kuandamamana hadi haki za kufanya migomo.

Kufuatia vurugu za baadhi ya mikutano ya vyama, na maandamano kuleta taharuki kubwa nchini kutishia amani na utulivu, JPM, rais chuma wa Tanzania, bila kujali katiba inasema nini, alipiga marufuku mikutano ya siasa na maandamano kinyume cha katiba.

Rais Samia alipoingia, akaruhusu mikutano ya siasa, tukitaraji ni nderemo na vifijo nchi mzima!, kumbe sivyo , mikutano hii na maandamano imeanza tena kuleta tensions zisizo za lazima!, tusimfanya Rais Samia ajute kuruhusu mikutano na maandamano na wananchi waseme afadhali ya Magufuli.

Kwenye hili la kuzuiwa mikutano ya hadhara, kwa vyàma vya siasa kwa vile mikutano hiyo ya vyama vya siasa ni kitu ambacho kimeruhusiwa na katiba, kitendo kile cha kuzuia mikutano hii, hakikuwa sawa!, huu ilikuwa ni ukwiukwaji wa wazi kabisa wa katiba ya JMT mchana kweupe!.

Kufanya mikutano na maandamano ni miongoni mwa haki za vyama vya siasa zilizoainishwa na katiba, ila pia kwenye kila haki kuna wajibu!. hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu.

Kitu kama ni haki, then haki ni stahili sio hisani!, Je sisi Watanzania tutaendelèa kusubiri hadi lini wakati haki zetu na stahili zetu zikigeuzwa kuwa hisani?

Tena afadhali ya hili la haki ya mikutano ya siasa, limefanywa kwa utashi tuu kwa kutumia kauli tuu, yaani mikutano ilizuiliwa kwa kauli, na sasa imeruhusiwa kwa kauli, lakini kuna na haki nyingine mbili ambazo ndizo haki kuu za kiraia zilizotolewa na katiba yetu, haki za kuchagua na kuchaguliwa, nazo zimegeuzwa hisani!. Haki ya kuchagua yenyewe bado ipo, ila haki ya kuchaguliwa, haipo!, imenyofolewa na kufinyangwa finyangwa hivyo kuonekana kama ipo ila kiukweli ni haipo na mimi mwenyewe ni shahidi wa hili!

Watanzania tuendelee kuwa watu wa shukrani kwa kushukuru kwa yote, hata kama ni madogo ili tuweze kupatiwa makubwa, hivyo tuendelee kusema asante sana Mama Samia kwa a good political will la kuruhusu mikutano ya siasa, kwa utashi tuu hivyo vyama na Watanzania kukushukuru kwa hisani yako hii, tunakuomba tumia a political will kama hii hii kuwaruhusu Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa!

Haki ni stahiki sio hisani!, haki haiombwi na kutegemea hisani, wala haki haihitaji vikao, mikutano na majadiliano kuzijadili haki, na haki hauletewi kwenye kisahani cha chai kama hisani, fadhila au zawadi, haki ni stahiki inayopaswa kutolewa unconditional not as a favour, hisani au fadhila!

Haki is a right, inayopaswa kutolewa unconditional na isipotolewa, haiombwi, bali hudaiwa, na katika kuidai huku kukishindikana kuidai kwa amani na kisheria, ndipo nguvu hutumika kuipigania, but only pale inapobidi, na ni katika kuipigania huku sometimes machozi, jasho na damu huweza kumwagika!

Wito kwa vyama vya siasa, shime tufanye resiponsible politics, tufanye mikutano na maandamano responsibly kwa mujibu wa katiba, na serikali itemize wajibu wake responsibly kwa mujibu wa katiba. Nguvu iliyotumika kuyazuia maandamano ya juzi ya Chadema, ingeweza kutumika kuhakikisha wanaandamana kwa amani.

Mungu Mbariki Rais Samia aruhusu haki kama stahiki na sio haki kama hisani.

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali
 
Haki Sio Hisani, Ni Stakihiki Inayopaswa Kutolewa!, Haipaswi Kuombwa, Bali Inadaiwa!. Haki ya Vyama vya Siasa Kufanya Mikutano na Maandamano, Iheshimiwe, Wajibu wa Kutunza Amani na Usalama Uheshimiwe!. Rais Samia Atabarikiwa Sana!.

Leo naomba kurejejelea zile Makala zangu za Ijue Katiba ya JMT kwa jicho la Mtunga Katiba, alidhamiria nini alipoweka kifungu fulani cha katiba. Ili tuweze kwenda sambasamba, naomba tukumbushane Katiba ni Nini?. Katiba ni kakitabu kadogo tuu chenye kurasa 113!. Kakitabu haka ndio kila kitu kuihusu Tanzania yetu, hakuna yeyote aliye juu ya Katiba.

Katiba ni ya Kazi Gani. Katiba ndio msingi Mkuu na muongozo wa uendeshaji wa nchi yetu, ambapo sheria zote, taratibu zote na kanuni zote, za kufanya kila jambo, lazima zitokane na katiba.

Misingi ya Katiba- Katiba yetu imeweka misingi mikuu 4 ya katiba ambayo ni uhuru, haki, udugu na amani. Misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu.

Hii maana yake, hii misingi mikuu 4 ya katiba yetu ambayo ni uhuru, haki, udugu na amani, Serikali, Bunge na Mahakama, zina wajibu wa kutekeleza, huu ni wajibu na sio hisani!. Tofauti ya wajibu na hisani, wajibu ni lazima utekelezwe, sio ombi, wakati hisani, ni huruma tuu unaweza ukatekeleza au usitekeleze kadri wewe unavyoona.

Turejee kwenye hii katiba, Katiba ni ya Nani? Katiba hii imetungwa na Bunge maalum kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia.

Hivyo kwa mujibu wa katiba hii, kitu muhimu kabisa kwa Taifa la Tanzania, ni watu!, Watanzania, hawa ndio wenye katiba!, katiba ni mali ya Watanzania. Ni watu hawa Watanzania, walioweka misingi mikuu minne ya katiba yetu, uhuru, haki, udugu na amani. Msingi mkuu wa kwanza wa katiba yetu ni uhuru, wa pili ni haki. Hivyo vitu vitu viwili vikuu vya katiba yetu ni uhuru na haki.

Katiba yetu ya mwaka 1977, unavyo vifungu kadhaa vya haki, kwenye vifungu hivyo, kunazo haki kuu za msingi. Haki kuu ni haki ya uraia, kuwa Mtanzania ndio haki kubwa kuliko zote, na Mtanzania ndicho kitu muhimu kuliko kitu chochochote ndani ya katiba yetu. Huyu mwananchi ndie mwenye nchi, mwenye katiba, anayemuajiri rais wa JMT kwa kura yake na kumlipa mshahara yeye na serikali yake, Bunge na Mahakama kwa kodi yake hivyo mwananchi ndie kila kitu!.

Kuanzia Ibara ya 5 hadi Ibara ya 30, haki mbalimbali zimetajwa na wajibu pia umetajwa, hapa nakutajia Ibara na haki yake

5. Haki ya kupiga kura.
11.Haki ya kufanya kazi, kupata elimu, na nyinginezo.
12.Usawa wa Binadamu. 13.Usawa mbele ya sheria.
14.Haki ya kuwa hai.
15.Haki ya uhuru wa mtu binafsi.
16.Haki ya faragha na ya usalama wa mtu.
17.Uhuru wa mtu kwenda atakako.
18.Uhuru wa maoni.

19.Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo.
20.Uhuru wa mtu kushirikiana na wengine.
21.Uhuru wa kushiriki shughuli za umma.
22.Haki ya kufanya kazi. 23.Haki ya kumiliki mali. 24.Haki ya kupata ujira wa haki.
Pia katiba imeweka wajibu
25.Wajibu wa kushiriki kazini.
26.Wajibu wa kutii sheria za nchi.
27.Kulinda mali ya Umma.
28.Ulinzi wa taifa.
29.Haki na wajibu muhimu.

30.Mipaka kwa haki, uhuru na hifadhi kwa haki na wajibu.


Baada ya haki hizo za msingi ndani ya katiba yetu, zikatungwa sheria na kutoa haki za mikusanyiko, haki za kufanya mikutano, haki za kuandamamana hadi haki za kufanya migomo.

Kufuatia vurugu za baadhi ya mikutano ya vyama, na maandamano kuleta taharuki kubwa nchini kutishia amani na utulivu, JPM, rais chuma wa Tanzania, bila kujali katiba inasema nini, alipiga marufuku mikutano ya siasa na maandamano kinyume cha katiba.

Rais Samia alipoingia, akaruhusu mikutano ya siasa, tukitaraji ni nderemo na vifijo nchi mzima!, kumbe sivyo , mikutano hii na maandamano imeanza tena kuleta tensions zisizo za lazima!, tusimfanya Rais Samia ajute kuruhusu mikutano na maandamano na wananchi waseme afadhali ya Magufuli.

Kwenye hili la kuzuiwa mikutano ya hadhara, kwa vyàma vya siasa kwa vile mikutano hiyo ya vyama vya siasa ni kitu ambacho kimeruhusiwa na katiba, kitendo kile cha kuzuia mikutano hii, hakikuwa sawa!, huu ilikuwa ni ukwiukwaji wa wazi kabisa wa katiba ya JMT mchana kweupe!.

Kufanya mikutano na maandamano ni miongoni mwa haki za vyama vya siasa zilizoainishwa na katiba, ila pia kwenye kila haki kuna wajibu!. hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu.

Kitu kama ni haki, then haki ni stahili sio hisani!, Je sisi Watanzania tutaendelèa kusubiri hadi lini wakati haki zetu na stahili zetu zikigeuzwa kuwa hisani?.

Tena afadhali ya hili la haki ya mikutano ya siasa, limefanywa kwa utashi tuu kwa kutumia kauli tuu, yaani mikutano ilizuiliwa kwa kauli, na sasa imeruhusiwa kwa kauli, lakini kuna na haki nyingine mbili ambazo ndizo haki kuu za kiraia zilizotolewa na katiba yetu, haki za kuchagua na kuchaguliwa, nazo zimegeuzwa hisani!. Haki ya kuchagua yenyewe bado ipo, ila haki ya kuchaguliwa, haipo!, imenyofolewa na kufinyangwa finyangwa hivyo kuonekana kama ipo ila kiukweli ni haipo na mimi mwenyewe ni shahidi wa hili!.

Watanzania tuendelee kuwa watu wa shukrani kwa kushukuru kwa yote, hata kama ni madogo ili tuweze kupatiwa makubwa, hivyo tuendelee kusema asante sana Mama Samia kwa a good political will la kuruhusu mikutano ya siasa, kwa utashi tuu hivyo vyama na Watanzania kukushukuru kwa hisani yako hii, tunakuomba tumia a political will kama hii hii kuwaruhusu Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa!.

Haki ni stahiki sio hisani!, haki haiombwi na kutegemea hisani, wala haki haihitaji vikao, mikutano na majadiliano kuzijadili haki, na haki hauletewi kwenye kisahani cha chai kama hisani, fadhila au zawadi, haki ni stahiki inayopaswa kutolewa unconditional not as a favour, hisani au fadhila!. Haki is a right, inayopaswa kutolewa unconditional na isipotolewa, haiombwi, bali hudaiwa, na katika kuidai huku kukishindikana kuidai kwa amani na kisheria, ndipo nguvu hutumika kuipigania, but only pale inapobidi, na ni katika kuipigania huku sometimes machozi, jasho na damu huweza kumwagika!.

Wito kwa vyama vya siasa, shime tufanye resiponsible politics, tufanye mikutano na maandamano responsibly kwa mujibu wa katiba, na serikali itemize wajibu wake responsibly kwa mujibu wa katiba. Nguvu iliyotumika kuyazuia maandamano ya juzi ya Chadema, ingeweza kutumika kuhakikisha wanaandamana kwa amani.

Mungu Mbariki Rais Samia aruhusu haki kama stahiki na sio haki kama hisani.

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali
JPM: alikiuka katiba akapiga marafuku…..,
Dictator Samia: alirudisha kama inavyotakiwa na katiba… siyo hisani… ni katiba ndiyo ilimlazimisha… siyo matakwa yake

We didn’t beg
 
Wanabodi,
Kama kawa,
Ukiangalia nguvu iliyotumika jana kuzuia maandamano ya Chadema, nguvu hiyo ingetumika kuyalinda maandamano hayo badala ya kuyazuia!.

Mada ya leo ni kuhusu haki, hakuna haki bila wajibu!, haki sio hisani ni stahiki inayopaswa kutolewa bila kuombwa. Haki ya kufanya mikutano na maandamano ni haki ya msingi ya vyama vya siasa, lakini pia vyama vina wajibu wa kufanya mikutano kwa amani na utulivu, wajibu wa kuhakiki amani na utulivu unakuwepo ni wajibu wa jeshi la Polisi, ndio maana vyama vinatakiwa kuiraifu Polisi mikutano na maandamano na ni jukumu la polisi kulinda amani kwenye mikutano hiyo na maandamano hayo, kitu cha ajabu kwenye maandamano ya jana, nguvu iliyotumika kuyazuia maandamano hayo ni kubwa ambayo ingetosha kabisa kuyalinda na Chadema wakaandamana kwa amani.

Haki sio hisani ya serikali, au jeshi la Polisi, haki ni stakihiki inayopaswa kutolewa bila kuombwa!. Haki haipaswi kuombwa, bali inapaswa kutolewa tuu, na isipotolewa haipaswi kuombwa bali inadaiwa!.

Haki ya vyama vya siasa kufanya mikutano na maandamano, ni haki ya msingi, iheshimiwe, waandamaji wana wajibu wa kuandamana kwa amani na kuitunza amani, utulivu na usalama, wakati huo huo, jeshi la Polisi lina wajibu wa kulinda amani, hivyo linapopata taarifa za kiiteligensia kuwa maandamano hayo yana malengo ya kificho ya "Samia Must Go", then jeshi la Polisi lina wajibu wa kuyazuia.

Leo naomba kurejejelea zile makala zangu za Ijue Katiba ya JMT kwa jicho la Mtunga Katiba, alidhamiria nini alipoweka kifungu fulani cha katiba. Ili tuweze kwenda sambasamba, naomba tukumbushane Katiba ni Nini?. Katiba ni kakitabu kadogo tuu chenye kurasa 113!. Kakitabu haka ndio kila kitu kuihusu Tanzania yetu, hakuna yeyote aliye juu ya Katiba.

Katiba ni ya Kazi Gani. Katiba ndio msingi Mkuu na muongozo wa uendeshaji wa nchi yetu, ambapo sheria zote, taratibu zote na kanuni zote, za kufanya kila jambo, lazima zitokane na katiba.

Misingi ya Katiba- Katiba yetu imeweka misingi mikuu 4 ya katiba ambayo ni uhuru, haki, udugu na amani. Misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu.

Hii maana yake, hii misingi mikuu 4 ya katiba yetu ambayo ni uhuru, haki, udugu na amani, Serikali, Bunge na Mahakama, zina wajibu wa kutekeleza, huu ni wajibu na sio hisani!. Tofauti ya wajibu na hisani, wajibu ni lazima utekelezwe, sio ombi, wakati hisani, ni huruma tuu unaweza ukatekeleza au usitekeleze kadri wewe unavyoona.

Turejee kwenye hii katiba, Katiba ni ya Nani? Katiba hii imetungwa na Bunge maalum kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia.

Hivyo kwa mujibu wa katiba hii, kitu muhimu kabisa kwa Taifa la Tanzania, ni watu!, Watanzania, hawa ndio wenye katiba!, katiba ni mali ya Watanzania. Ni watu hawa Watanzania, walioweka misingi mikuu minne ya katiba yetu, uhuru, haki, udugu na amani. Msingi mkuu wa kwanza wa katiba yetu ni uhuru, wa pili ni haki. Hivyo vitu vitu viwili vikuu vya katiba yetu ni uhuru na haki.

Katiba yetu ya mwaka 1977, unavyo vifungu kadhaa vya haki, kwenye vifungu hivyo, kunazo haki kuu za msingi. Haki kuu ni haki ya uraia, kuwa Mtanzania ndio haki kubwa kuliko zote, na Mtanzania ndicho kitu muhimu kuliko kitu chochochote ndani ya katiba yetu. Huyu mwananchi ndie mwenye nchi, mwenye katiba, anayemuajiri rais wa JMT kwa kura yake na kumlipa mshahara yeye na serikali yake, Bunge na Mahakama kwa kodi yake hivyo mwananchi ndie kila kitu!.

Kuanzia Ibara ya 5 hadi Ibara ya 30, haki mbalimbali zimetajwa na wajibu pia umetajwa, hapa nakutajia Ibara na haki yake

5. Haki ya kupiga kura.
11.Haki ya kufanya kazi, kupata elimu, na nyinginezo.
12.Usawa wa Binadamu. 13.Usawa mbele ya sheria.
14.Haki ya kuwa hai.
15.Haki ya uhuru wa mtu binafsi.
16.Haki ya faragha na ya usalama wa mtu.
17.Uhuru wa mtu kwenda atakako.
18.Uhuru wa maoni.

19.Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo.
20.Uhuru wa mtu kushirikiana na wengine.
21.Uhuru wa kushiriki shughuli za umma.
22.Haki ya kufanya kazi. 23.Haki ya kumiliki mali. 24.Haki ya kupata ujira wa haki.
Pia katiba imeweka wajibu
25.Wajibu wa kushiriki kazini.
26.Wajibu wa kutii sheria za nchi.
27.Kulinda mali ya Umma.
28.Ulinzi wa taifa.
29.Haki na wajibu muhimu.

30.Mipaka kwa haki, uhuru na hifadhi kwa haki na wajibu.


Baada ya haki hizo za msingi ndani ya katiba yetu, zikatungwa sheria na kutoa haki za mikusanyiko, haki za kufanya mikutano, haki za kuandamamana hadi haki za kufanya migomo.

Kufuatia vurugu za baadhi ya mikutano ya vyama, na maandamano kuleta taharuki kubwa nchini kutishia amani na utulivu, JPM, rais chuma wa Tanzania, bila kujali katiba inasema nini, alipiga marufuku mikutano ya siasa na maandamano kinyume cha katiba.

Rais Samia alipoingia, akaruhusu mikutano ya siasa, tukitaraji ni nderemo na vifijo nchi mzima!, kumbe sivyo , mikutano hii na maandamano imeanza tena kuleta tensions zisizo za lazima!, tusimfanya Rais Samia ajute kuruhusu mikutano na maandamano na wananchi waseme afadhali ya Magufuli.

Kwenye hili la kuzuiwa mikutano ya hadhara, kwa vyàma vya siasa kwa vile mikutano hiyo ya vyama vya siasa ni kitu ambacho kimeruhusiwa na katiba, kitendo kile cha kuzuia mikutano hii, hakikuwa sawa!, huu ilikuwa ni ukwiukwaji wa wazi kabisa wa katiba ya JMT mchana kweupe!.

Kufanya mikutano na maandamano ni miongoni mwa haki za vyama vya siasa zilizoainishwa na katiba, ila pia kwenye kila haki kuna wajibu!. hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu.

Kitu kama ni haki, then haki ni stahili sio hisani!, Je sisi Watanzania tutaendelèa kusubiri hadi lini wakati haki zetu na stahili zetu zikigeuzwa kuwa hisani?.

Tena afadhali ya hili la haki ya mikutano ya siasa, limefanywa kwa utashi tuu kwa kutumia kauli tuu, yaani mikutano ilizuiliwa kwa kauli, na sasa imeruhusiwa kwa kauli, lakini kuna na haki nyingine mbili ambazo ndizo haki kuu za kiraia zilizotolewa na katiba yetu, haki za kuchagua na kuchaguliwa, nazo zimegeuzwa hisani!. Haki ya kuchagua yenyewe bado ipo, ila haki ya kuchaguliwa, haipo!, imenyofolewa na kufinyangwa finyangwa hivyo kuonekana kama ipo ila kiukweli ni haipo na mimi mwenyewe ni shahidi wa hili!.

Watanzania tuendelee kuwa watu wa shukrani kwa kushukuru kwa yote, hata kama ni madogo ili tuweze kupatiwa makubwa, hivyo tuendelee kusema asante sana Mama Samia kwa a good political will la kuruhusu mikutano ya siasa, kwa utashi tuu hivyo vyama na Watanzania kukushukuru kwa hisani yako hii, tunakuomba tumia a political will kama hii hii kuwaruhusu Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa!.

Haki ni stahiki sio hisani!, haki haiombwi na kutegemea hisani, wala haki haihitaji vikao, mikutano na majadiliano kuzijadili haki, na haki hauletewi kwenye kisahani cha chai kama hisani, fadhila au zawadi, haki ni stahiki inayopaswa kutolewa unconditional not as a favour, hisani au fadhila!. Haki is a right, inayopaswa kutolewa unconditional na isipotolewa, haiombwi, bali hudaiwa, na katika kuidai huku kukishindikana kuidai kwa amani na kisheria, ndipo nguvu hutumika kuipigania, but only pale inapobidi, na ni katika kuipigania huku sometimes machozi, jasho na damu huweza kumwagika!.

Wito kwa vyama vya siasa, shime tufanye resiponsible politics, tufanye mikutano na maandamano responsibly kwa mujibu wa katiba, na serikali itemize wajibu wake responsibly kwa mujibu wa katiba. Nguvu iliyotumika kuyazuia maandamano ya juzi ya Chadema, ingeweza kutumika kuhakikisha wanaandamana kwa amani.

Mungu Mbariki Rais Samia aruhusu haki kama stahiki na sio haki kama hisani.

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali
Kaka Paskali, binafsi kinachoniboa ni haya maneno ya kila wakati ya polisi;

1. Taarifa za kiintelijensia

2. Maagizo kutoka juu

3. Ukiliza kwanini upo under arrest, utasikia utaenda kujua kituoni

Haya mambo tajwa hapo juu, yanauwa kabisa dhan nzima ya haki kwenda na mwajibu, au wajibu kwenda na haki, iwe kwa pamoja au kimoja kitangulie.

Haya maneno yanatumika kuficha mambo mengi sana yahusuyo haki za raia
 
Haki na wajibu vinaenda both sides. Kwa watendaji na wananchi. Bahati mbaya mwananchi anatakiwa kufanya wajibu wake ila hapewi haki yake.

Ya jana ilikuwa haki ya msingi ya mwananchi, ila alinyimwa...na mengine mengi tu mwananchi ananyimwa.
 
Misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu.
Jee serikali ya TZ haina sifa hizi?
Haki ni stahiki sio hisani!, haki haiombwi na kutegemea hisani, wala haki haihitaji vikao, mikutano na majadiliano kuzijadili haki, na haki hauletewi kwenye kisahani cha chai kama hisani, fadhila au zawadi, haki ni stahiki inayopaswa kutolewa unconditional not as a favour, hisani au fadhila!

Ni kweli uliyoyasema. Jee hao waliodai haki jana na juzi na siku nyingine walionesha kwa vitendo haya uliyoyaandika?
Wito kwa vyama vya siasa, shime tufanye resiponsible politics, tufanye mikutano na maandamano responsibly kwa mujibu wa katiba, na serikali itemize wajibu wake responsibly kwa mujibu wa katiba. Nguvu iliyotumika kuyazuia maandamano ya juzi ya Chadema, ingeweza kutumika kuhakikisha wanaandamana kwa amani.
Haya uliyaandika hapa yalitekelezwa na vyama vya siasa?
Mungu Mbariki Rais Samia aruhusu haki kama stahiki na sio haki kama hisani.
Naomba nami iwe hivyo.

Naomba watu na wewe muelewe kwamba siku zote haki hailetwi kisahanini kama keki.

Waambie, nawe ujue, kwamba kwenye haki ukisema "nitafanya" lazima ufanye. Ukijitia uoga imekula kwako.

Siku zote ukimwambia mtu "nitakuua" naye atatafuta namna yackuhakikisha humuui. Ni juu yako kutekeleza. Ukimwacha usilalamike na matokeo yake. Huwezi kusema kwa maneno na mabango kwamba "Samia must go" halafu Samia akuambie "haya endelea". Ni juu yako kumuonesha kwa vitendo.


Nimevunjika moyo sana jana kwa waliojigamba wangeandamana lakini wakaufyata. Ni masikitiko lakini ndo mambo na hao ndo Wadanganyika.
 
Jeshi la polisi lilifanya vizuri sana kuwadhibiti .maana maandamano yenu tangia awali yalikuwa yana Lengo baya pale mlipokuwa mnasema kuwa Samia Must Go.
Unataka na sisi tumsifie kama vile kuna kitu cha maana kafanya? huyo nguvu waliyotumia jana kwanini wasiitumie kudhibiti matukio ya hovyo kama utekaji na mauaji?
 
Pamoja na kuundwa tume ya kuchunguza mambo ya haki jinai na kutoa mapendekezo, hali imekuwa mbaya zaidi..kulikuwa na maana gani kupoteza pesa kulipa watu kwa jambo ambalo muunda tume hana uwezo wa kubadilisha chochote? haya ndio mambo ya kuhoji pascal..
 
Wanabodi,

Kama kawa,

Ukiangalia nguvu iliyotumika jana kuzuia maandamano ya Chadema, nguvu hiyo ingetumika kuyalinda maandamano hayo badala ya kuyazuia!

Mada ya leo ni kuhusu haki, hakuna haki bila wajibu!, haki sio hisani ni stahiki inayopaswa kutolewa bila kuombwa. Haki ya kufanya mikutano na maandamano ni haki ya msingi ya vyama vya siasa, lakini pia vyama vina wajibu wa kufanya mikutano kwa amani na utulivu, wajibu wa kuhakiki amani na utulivu unakuwepo ni wajibu wa jeshi la Polisi, ndio maana vyama vinatakiwa kuiraifu Polisi mikutano na maandamano na ni jukumu la polisi kulinda amani kwenye mikutano hiyo na maandamano hayo, kitu cha ajabu kwenye maandamano ya jana, nguvu iliyotumika kuyazuia maandamano hayo ni kubwa ambayo ingetosha kabisa kuyalinda na Chadema wakaandamana kwa amani.

Haki sio hisani ya serikali, au jeshi la Polisi, haki ni stakihiki inayopaswa kutolewa bila kuombwa!. Haki haipaswi kuombwa, bali inapaswa kutolewa tuu, na isipotolewa haipaswi kuombwa bali inadaiwa, na ni katika kuidai huku sometimes hlazimika kugharimiwa kwa gharama za machozi, jasho na damu!.

Haki ya vyama vya siasa kufanya mikutano na maandamano, ni haki ya msingi, iheshimiwe, waandamaji wana wajibu wa kuandamana kwa amani na kuitunza amani, utulivu na usalama, wakati huo huo, jeshi la Polisi lina wajibu wa kulinda amani, hivyo linapopata taarifa za kiiteligensia kuwa maandamano hayo yana malengo ya kificho ya "Samia Must Go", then jeshi la Polisi lina wajibu wa kuyazuia.

Leo naomba kurejejelea zile makala zangu za Ijue Katiba ya JMT kwa jicho la Mtunga Katiba, alidhamiria nini alipoweka kifungu fulani cha katiba. Ili tuweze kwenda sambasamba, naomba tukumbushane Katiba ni Nini?. Katiba ni kakitabu kadogo tuu chenye kurasa 113!. Kakitabu haka ndio kila kitu kuihusu Tanzania yetu, hakuna yeyote aliye juu ya Katiba.

Katiba ni ya Kazi Gani. Katiba ndio msingi Mkuu na muongozo wa uendeshaji wa nchi yetu, ambapo sheria zote, taratibu zote na kanuni zote, za kufanya kila jambo, lazima zitokane na katiba.

Misingi ya Katiba- Katiba yetu imeweka misingi mikuu 4 ya katiba ambayo ni uhuru, haki, udugu na amani. Misingi hiyo yaweza tu kutekelezwa katika jamii yenye demokrasia ambayo serikali yake husimamiwa na Bunge lenye wajumbe waliochaguliwa na linalowawakilisha wananchi, na pia yenye Mahakama huru zinazotekeleza wajibu wa kutoa haki bila woga wala upendeleo wowote, na hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu.

Hii maana yake, hii misingi mikuu 4 ya katiba yetu ambayo ni uhuru, haki, udugu na amani, Serikali, Bunge na Mahakama, zina wajibu wa kutekeleza, huu ni wajibu na sio hisani!. Tofauti ya wajibu na hisani, wajibu ni lazima utekelezwe, sio ombi, wakati hisani, ni huruma tuu unaweza ukatekeleza au usitekeleze kadri wewe unavyoona.

Turejee kwenye hii katiba, Katiba ni ya Nani? Katiba hii imetungwa na Bunge maalum kwa niaba ya Wananchi, kwa madhumuni ya kujenga jamii kama hiyo, na pia kwa ajili ya kuhakikisha kwamba Tanzania inaongozwa na Serikali yenye kufuata misingi ya demokrasia.

Hivyo kwa mujibu wa katiba hii, kitu muhimu kabisa kwa Taifa la Tanzania, ni watu!, Watanzania, hawa ndio wenye katiba!, katiba ni mali ya Watanzania. Ni watu hawa Watanzania, walioweka misingi mikuu minne ya katiba yetu, uhuru, haki, udugu na amani. Msingi mkuu wa kwanza wa katiba yetu ni uhuru, wa pili ni haki. Hivyo vitu vitu viwili vikuu vya katiba yetu ni uhuru na haki.

Katiba yetu ya mwaka 1977, unavyo vifungu kadhaa vya haki, kwenye vifungu hivyo, kunazo haki kuu za msingi. Haki kuu ni haki ya uraia, kuwa Mtanzania ndio haki kubwa kuliko zote, na Mtanzania ndicho kitu muhimu kuliko kitu chochochote ndani ya katiba yetu. Huyu mwananchi ndie mwenye nchi, mwenye katiba, anayemuajiri rais wa JMT kwa kura yake na kumlipa mshahara yeye na serikali yake, Bunge na Mahakama kwa kodi yake hivyo mwananchi ndie kila kitu!.

Kuanzia Ibara ya 5 hadi Ibara ya 30, haki mbalimbali zimetajwa na wajibu pia umetajwa, hapa nakutajia Ibara na haki yake

5. Haki ya kupiga kura.
11. Haki ya kufanya kazi, kupata elimu, na nyinginezo.
12. Usawa wa Binadamu. 13.Usawa mbele ya sheria.
14. Haki ya kuwa hai.
15.Haki ya uhuru wa mtu binafsi.
16. Haki ya faragha na ya usalama wa mtu.
17. Uhuru wa mtu kwenda atakako.
18.Uhuru wa maoni.

19. Uhuru wa mtu kuamini dini atakayo.
20. Uhuru wa mtu kushirikiana na wengine.
21. Uhuru wa kushiriki shughuli za umma.
22. Haki ya kufanya kazi. 23.Haki ya kumiliki mali. 24.Haki ya kupata ujira wa haki.
Pia katiba imeweka wajibu
25. Wajibu wa kushiriki kazini.
26. Wajibu wa kutii sheria za nchi.
27. Kulinda mali ya Umma.
28. Ulinzi wa taifa.
29. Haki na wajibu muhimu.

30. Mipaka kwa haki, uhuru na hifadhi kwa haki na wajibu.


Baada ya haki hizo za msingi ndani ya katiba yetu, zikatungwa sheria na kutoa haki za mikusanyiko, haki za kufanya mikutano, haki za kuandamamana hadi haki za kufanya migomo.

Kufuatia vurugu za baadhi ya mikutano ya vyama, na maandamano kuleta taharuki kubwa nchini kutishia amani na utulivu, JPM, rais chuma wa Tanzania, bila kujali katiba inasema nini, alipiga marufuku mikutano ya siasa na maandamano kinyume cha katiba.

Rais Samia alipoingia, akaruhusu mikutano ya siasa, tukitaraji ni nderemo na vifijo nchi mzima!, kumbe sivyo , mikutano hii na maandamano imeanza tena kuleta tensions zisizo za lazima!, tusimfanya Rais Samia ajute kuruhusu mikutano na maandamano na wananchi waseme afadhali ya Magufuli.

Kwenye hili la kuzuiwa mikutano ya hadhara, kwa vyàma vya siasa kwa vile mikutano hiyo ya vyama vya siasa ni kitu ambacho kimeruhusiwa na katiba, kitendo kile cha kuzuia mikutano hii, hakikuwa sawa!, huu ilikuwa ni ukwiukwaji wa wazi kabisa wa katiba ya JMT mchana kweupe!.

Kufanya mikutano na maandamano ni miongoni mwa haki za vyama vya siasa zilizoainishwa na katiba, ila pia kwenye kila haki kuna wajibu!. hivyo kuhakikisha kwamba haki zote za binadamu zinadumishwa na kulindwa, na wajibu wa kila mtu unatekelezwa kwa uaminifu.

Kitu kama ni haki, then haki ni stahili sio hisani!, Je sisi Watanzania tutaendelèa kusubiri hadi lini wakati haki zetu na stahili zetu zikigeuzwa kuwa hisani?

Tena afadhali ya hili la haki ya mikutano ya siasa, limefanywa kwa utashi tuu kwa kutumia kauli tuu, yaani mikutano ilizuiliwa kwa kauli, na sasa imeruhusiwa kwa kauli, lakini kuna na haki nyingine mbili ambazo ndizo haki kuu za kiraia zilizotolewa na katiba yetu, haki za kuchagua na kuchaguliwa, nazo zimegeuzwa hisani!. Haki ya kuchagua yenyewe bado ipo, ila haki ya kuchaguliwa, haipo!, imenyofolewa na kufinyangwa finyangwa hivyo kuonekana kama ipo ila kiukweli ni haipo na mimi mwenyewe ni shahidi wa hili!

Watanzania tuendelee kuwa watu wa shukrani kwa kushukuru kwa yote, hata kama ni madogo ili tuweze kupatiwa makubwa, hivyo tuendelee kusema asante sana Mama Samia kwa a good political will la kuruhusu mikutano ya siasa, kwa utashi tuu hivyo vyama na Watanzania kukushukuru kwa hisani yako hii, tunakuomba tumia a political will kama hii hii kuwaruhusu Watanzania wote kuchagua na kuchaguliwa!

Haki ni stahiki sio hisani!, haki haiombwi na kutegemea hisani, wala haki haihitaji vikao, mikutano na majadiliano kuzijadili haki, na haki hauletewi kwenye kisahani cha chai kama hisani, fadhila au zawadi, haki ni stahiki inayopaswa kutolewa unconditional not as a favour, hisani au fadhila!

Haki is a right, inayopaswa kutolewa unconditional na isipotolewa, haiombwi, bali hudaiwa, na katika kuidai huku kukishindikana kuidai kwa amani na kisheria, ndipo nguvu hutumika kuipigania, but only pale inapobidi, na ni katika kuipigania huku sometimes machozi, jasho na damu huweza kumwagika!

Wito kwa vyama vya siasa, shime tufanye resiponsible politics, tufanye mikutano na maandamano responsibly kwa mujibu wa katiba, na serikali itemize wajibu wake responsibly kwa mujibu wa katiba. Nguvu iliyotumika kuyazuia maandamano ya juzi ya Chadema, ingeweza kutumika kuhakikisha wanaandamana kwa amani.

Mungu Mbariki Rais Samia aruhusu haki kama stahiki na sio haki kama hisani.

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali
Nadhani kuhusu suala la umoja, amani na utulivu wa wananchi Tanzania, liko wazi kabisa, na mkuu wa nchi alishasema bayana bila kubabaika wala kupepesa macho, kwa Taifa na dunia nzima ikaskia,

Kwamba kama Taifa, tutailinda usalama na amani ya Tanzania kwa nguvu zote na kwa gharama yoyote ile full stop. Hakuna mijadala kwenye hilo.

Ukiwa mjuaji sana, jeuri na kaidi, tafadhali, jitahidi sana kwenye maandamano haramu yaliyopigwa marufuku na polisi, ñjoo na katiba yako utaelekezwa vizuri sana kwa virungu na polisi, maana ya haki na wajibu wa kuandamana kwa amani kikatiba, ili ukawafundishe na kuwaeleza makaidi wengine ukiwa umevimba macho na kuteguka kiuno, kwamba Tanzania hakuna mzaha kwenye suala la Amani.

Friends, ladies and gentlemen,
Kwani kwenye yale maandamano ya June - august ya CHADEMA yaliyopita, kulikua na muujiza gani, hata pakawepo ulinzi mkali na mzito wa polisi namna ile, na maandamano yakawa ya amani vile?

Au ilikua ni makosa makubwa sana kwa Rais na kipenzi cha waTanzania Dr.Samia Suluhu Hassan kuondoa marufuku na katazo la mikutano ya hadharani na maandamano lililowekwa na mtangulizi wake?

Au ilikua ni kosa kubwa zaidi Rais Dr. Samia Suluhu Hassan kuruhusu maandamano yale ya chadema yaliyopita na sasa wakaamua kumdharau Rais na sasa wakaitisha maandamano ya Samia Must Go, maana yake lazima aondolewe madakani kwa nguvu apende asipende, right?

Hiyo ndiyo demokrasia mnapambania? Au hiyo ndio shukran ya punda, right?

Kwani dhamira, malengo na nia ya kufanyika kwa maandamano ya chadema ya August katika majiji ya Dar, Arusha, Meanza na Mbeya imemoptelea wapi kwa wanachadema, kwenye maandamano ya jana mpaka yawe ya shari na kufikia kuamua kuja na Samia Must Go hala usiku wa manane kubadisha yakawa sijui maandamano ya nini tena?

Kwamba chadema wanafanya Jokes kwenye amani ee? sijui wanaijaribu nchi au serikali itafanyaje, right?

Hivi mwalimu,
ni nini kingeweza kua matokeo ya maandamano ya Samia must go honestly?

Lakini mwalimu Pascal Mayalla, pia hivi kweli kwa darasa lako la leo ndio inafahamika kwamba maandamano ni haki ya kikatiba na sio hisani, hata kama yana kusudi la kulazimisha fujo uharibifu na pengine maafa?

Nilikuuliza jana, unaweza kufafanua kwa kiasi, nini hasa maana, dhamira, kusudi, nia na matokeo ya Samia Must go?

Kwa kiasi fulani kadiri unavyotoa masomo haya malimbali kwenye jukwaa hili,
somo la haki ya kuandamana kikatiba nadhani limeanza kueleweka vizuri.

Nashauri kwenye somo lijalo ukijaaliwa, msitizo uweke kwenye wajibu na dhamira ya anaekusudia kuandamana, itapendeza zaidi. Na inshallah tunaweza kuelewana na tukawa na uelekeo moja wa kimtazamo kuhusu amani ya kudumu kwa Taifa letu.

Hata hivyo ifahamike wazi umoja, amani na utulivu wa wananchi Tanzania, utalindwa kwa nguvu zote na kwa gharama yoyote ile, dhidi ya mtu au Taifa lolote litakalothubutu kuhatarisha au kuvuruga usalama wa waTanzania.🐒

Mungu Ibariki Tanzania
 
CHADEMA walitimiza wajibu wa kufuata taratibu kuandamana kwa kutoa taarifa za maandamano ya amani, lakini haki yao ikazuiliwa. Kulikuwa hamna viashiria vyovyote vya kuvunja amani na utulivu katika maandamano yao.
 
Nadhani kuhusu suala la umoja, amani na utulivu wa wananchi Tanzania, liko wazi kabisa, na mkuu wa nchi alishasema bayana bila kubabaika wala kupepesa macho, kwa Taifa na dunia nzima ikaskia,

Kwamba kama Taifa, tutailinda usalama na amani ya Tanzania kwa nguvu zote na kwa gharama yoyote ile full stop. Hakuna mijadala kwenye hilo.

Ukiwa mjuaji sana, jeuri na kaidi, tafadhali, jitahidi sana kwenye maandamano haramu yaliyopigwa marufuku na polisi, ñjoo na katiba yako utaelekezwa vizuri sana kwa virungu na polisi, maana ya haki na wajibu wa kuandamana kwa amani kikatiba, ili ukawafundishe na kuwaeleza makaidi wengine ukiwa umevimba macho na kuteguka kiuno, kwamba Tanzania hakuna mzaha kwenye suala la Amani.

Friends, ladies and gentlemen,
Kwani kwenye yale maandamano ya June - august ya CHADEMA yaliyopita, kulikua na muujiza gani, hata pakawepo ulinzi mkali na mzito wa polisi namna ile, na maandamano yakawa ya amani vile?

Au ilikua ni makosa makubwa sana kwa Rais na kipenzi cha waTanzania Dr.Samia Suluhu Hassan kuondoa marufuku na katazo la mikutano ya hadharani na maandamano lililowekwa na mtangulizi wake?

Au ilikua ni kosa kubwa zaidi Rais Dr. Samia Suluhu Hassan kuruhusu maandamano yale ya chadema yaliyopita na sasa wakaamua kumdharau Rais na sasa wakaitisha maandamano ya Samia Must Go, maana yake lazima aondolewe madakani kwa nguvu apende asipende, right?

Hiyo ndiyo demokrasia mnapambania? Au hiyo ndio shukran ya punda, right?

Kwani dhamira, malengo na nia ya kufanyika kwa maandamano ya chadema ya August katika majiji ya Dar, Arusha, Meanza na Mbeya imemoptelea wapi kwa wanachadema, kwenye maandamano ya jana mpaka yawe ya shari na kufikia kuamua kuja na Samia Must Go hala usiku wa manane kubadisha yakawa sijui maandamano ya nini tena?

Kwamba chadema wanafanya Jokes kwenye amani ee? sijui wanaijaribu nchi au serikali itafanyaje, right?

Hivi mwalimu,
ni nini kingeweza kua matokeo ya maandamano ya Samia must go honestly?

Lakini mwalimu Pascal Mayalla, pia hivi kweli kwa darasa lako la leo ndio inafahamika kwamba maandamano ni haki ya kikatiba na sio hisani, hata kama yana kusudi la kulazimisha fujo uharibifu na pengine maafa?

Nilikuuliza jana, unaweza kufafanua kwa kiasi, nini hasa maana, dhamira, kusudi, nia na matokeo ya Samia Must go?

Kwa kiasi fulani kadiri unavyotoa masomo haya malimbali kwenye jukwaa hili,
somo la haki ya kuandamana kikatiba nadhani limeanza kueleweka vizuri.

Nashauri kwenye somo lijalo ukijaaliwa, msitizo uweke kwenye wajibu na dhamira ya anaekusudia kuandamana, itapendeza zaidi. Na inshallah tunaweza kuelewana na tukawa na uelekeo moja wa kimtazamo kuhusu amani ya kudumu kwa Taifa letu.

Hata hivyo ifahamike wazi umoja, amani na utulivu wa wananchi Tanzania, utalindwa kwa nguvu zote na kwa gharama yoyote ile, dhidi ya mtu au Taifa lolote litakalothubutu kuhatarisha au kuvuruga usalama wa waTanzania.🐒

Mungu Ibariki Tanzania
Mkuu wewe umenena. Watakao kuelewa wataelewa.
 
Nadhani kuhusu suala la umoja, amani na utulivu wa wananchi Tanzania, liko wazi kabisa, na mkuu wa nchi alishasema bayana bila kubabaika wala kupepesa macho, kwa Taifa na dunia nzima ikaskia,

Kwamba kama Taifa, tutailinda usalama na amani ya Tanzania kwa nguvu zote na kwa gharama yoyote ile full stop. Hakuna mijadala kwenye hilo.

Ukiwa mjuaji sana, jeuri na kaidi, tafadhali, jitahidi sana kwenye maandamano haramu yaliyopigwa marufuku na polisi, ñjoo na katiba yako utaelekezwa vizuri sana kwa virungu na polisi, maana ya haki na wajibu wa kuandamana kwa amani kikatiba, ili ukawafundishe na kuwaeleza makaidi wengine ukiwa umevimba macho na kuteguka kiuno, kwamba Tanzania hakuna mzaha kwenye suala la Amani.

Friends, ladies and gentlemen,
Kwani kwenye yale maandamano ya June - august ya CHADEMA yaliyopita, kulikua na muujiza gani, hata pakawepo ulinzi mkali na mzito wa polisi namna ile, na maandamano yakawa ya amani vile?

Au ilikua ni makosa makubwa sana kwa Rais na kipenzi cha waTanzania Dr.Samia Suluhu Hassan kuondoa marufuku na katazo la mikutano ya hadharani na maandamano lililowekwa na mtangulizi wake?

Au ilikua ni kosa kubwa zaidi Rais Dr. Samia Suluhu Hassan kuruhusu maandamano yale ya chadema yaliyopita na sasa wakaamua kumdharau Rais na sasa wakaitisha maandamano ya Samia Must Go, maana yake lazima aondolewe madakani kwa nguvu apende asipende, right?

Hiyo ndiyo demokrasia mnapambania? Au hiyo ndio shukran ya punda, right?

Kwani dhamira, malengo na nia ya kufanyika kwa maandamano ya chadema ya August katika majiji ya Dar, Arusha, Meanza na Mbeya imemoptelea wapi kwa wanachadema, kwenye maandamano ya jana mpaka yawe ya shari na kufikia kuamua kuja na Samia Must Go hala usiku wa manane kubadisha yakawa sijui maandamano ya nini tena?

Kwamba chadema wanafanya Jokes kwenye amani ee? sijui wanaijaribu nchi au serikali itafanyaje, right?

Hivi mwalimu,
ni nini kingeweza kua matokeo ya maandamano ya Samia must go honestly?

Lakini mwalimu Pascal Mayalla, pia hivi kweli kwa darasa lako la leo ndio inafahamika kwamba maandamano ni haki ya kikatiba na sio hisani, hata kama yana kusudi la kulazimisha fujo uharibifu na pengine maafa?

Nilikuuliza jana, unaweza kufafanua kwa kiasi, nini hasa maana, dhamira, kusudi, nia na matokeo ya Samia Must go?

Kwa kiasi fulani kadiri unavyotoa masomo haya malimbali kwenye jukwaa hili,
somo la haki ya kuandamana kikatiba nadhani limeanza kueleweka vizuri.

Nashauri kwenye somo lijalo ukijaaliwa, msitizo uweke kwenye wajibu na dhamira ya anaekusudia kuandamana, itapendeza zaidi. Na inshallah tunaweza kuelewana na tukawa na uelekeo moja wa kimtazamo kuhusu amani ya kudumu kwa Taifa letu.

Hata hivyo ifahamike wazi umoja, amani na utulivu wa wananchi Tanzania, utalindwa kwa nguvu zote na kwa gharama yoyote ile, dhidi ya mtu au Taifa lolote litakalothubutu kuhatarisha au kuvuruga usalama wa waTanzania.🐒

Mungu Ibariki Tanzania
Mtu mwenye uwezo wa kufikiri kama kuku anaona maandamano kwa mtizamo huu..taja matishio ya usalama na amani unayoimba kila mara kwamba utalinda usalama na amani..unaaminishwa ujinga usiokuwepo kabisa..uhuru wa kujieleza kwa njia ya maandamano ni haki ya binadamu kimataifa, na huwezi kupangia mtu ajieleze kwa njia gani ili mradi havunji sheria..walioandaa maandamano wametaja sababu za kuandamana..kuhoji watu waliotekwa wako wapi na kupinga mauaji yanayotokana na utekaji! ajabu wewe unashikilia ishu ndogo ya samia must go..! kwa nini wenye dhamana ya kuwajibika hawatoi majibu ya yanayoulizwa na kulalamikiwa???
 
Yani watu walewale waliosema mtu yupo Arusha, mara waliweka kambi nje ya geti yake Dar, na walishangaa ameibuka eneo ya tukio, ni walewale wanamwambia mama yenu “hali ni shwari”? Na yeye anawaamini kabisa?
 
Mtu mwenye uwezo wa kufikiri kama kuku anaona maandamano kwa mtizamo huu..taja matishio ya usalama na amani unayoimba kila mara kwamba utalinda usalama na amani..unaaminishwa ujinga usiokuwepo kabisa..uhuru wa kujieleza kwa njia ya maandamano ni haki ya binadamu kimataifa, na huwezi kupangia mtu ajieleze kwa njia gani ili mradi havunji sheria..walioandaa maandamano wametaja sababu za kuandamana..kuhoji watu waliotekwa wako wapi na kupinga mauaji yanayotokana na utekaji! ajabu wewe unashikilia ishu ndogo ya samia must go..! kwa nini wenye dhamana ya kuwajibika hawatoi majibu ya yanayoulizwa na kulalamikiwa???
jambo hili ni rahisi sana tu, wala haihitaji mihemko, ghadhabu, hisia wala huruma..

kwanini nia na dhamira ya maandamano ya Samia must go ilibadilishwa usiku wa manane?🤣

au ndio kujaribu au kuinja sumu kwa ulimi?

Mlipewa ruhusa ya kuingiza pua, sasa mnataka kulazimisha kizembe kabisa kuingiza kichwa na kitambi kabisa🤣

mlipewa fursa ya kuungia sebuleni eti, kwa lazima mnataka muingie chumbani, na kumtoa mwenyewe chumba? Useless kabisa alaaa!!🤣

ng'weee ng'weee ng'weee eti haki ya kikatiba. sasa si ungekuja na hiyo katiba yako ya samai must go ili uelekezwe vizuri maana yake kwa virungu na polisi 🤣
 
Back
Top Bottom