Elections 2015 Hakuna kifungu cha sheria kinachomruhusu mpiga kura kukaa nje ya mita 200 toka kituoni akilinda kura


Jifunze kulewa sheria ya uchaguzi haimhitaji mtu kukaa na kufanya shughuli yoyote ikiwemo kuvaa alama yoyote inayotambulisha chama chochote cha siasa ndani ya meta 200 toka mahali au kwenye jengo ambalo Upigaji kura unafanyika

PART II
OTHER ELECTION OFFENCES

104.-(1) No person shall, within any buildings where; voting in an
election is in progress or at any place within the radius or two hundred
meters of any such building, wear or display any card, symbol, favour or
other emblem indicating support for a particular candidate in the election.

(2) Any person acting in contravention of this section shall be guilty
of an offence and shall be liable on conviction to a fine not exceeding two
hundred shillings.
 
Haina haja kutumia akili nyingi sana kwani sheria ipo wazi sana kwa umbali Wa mita mia mbili basi nitakesha hapo sheria inaniruhusu sasa ukinifuata kunipiga mabomu huo ni ugomvi usio isha kwa maneno
 

Sheria Hairuhusu Mkusanyiko Au Maandamano Yasiyoratibiwa Na Kupata Kibali,
 
nilidhani unaweka hapa hicho kifungu cha sheria tukijadili kumbe ni porojo tu...
 

asante kaka. ukawa wako sahihi....nje ya mita 200 watu wanaruhusiwa...
 
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Mwanasheria wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Mallya amesema wanaendelea kushikilia msimamo huo kwa kuzingatia Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2010 kupitia kifungu Na. 104.
Mallya amesema kifungu hicho kinakataza watu kuwepo kwenye kituo cha kupiga kura isipokuwa nje ya mita 200 ya kituo husika.
Rais Kikwete akihutubia wananchi katika sherehe za kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru, mjini Dodoma jana, alisema ni marufuku watu kukaa karibu na vituo na kuonya kuwa atakayevunja sheria hatovumiliwa ili kuepusha demokrasia kutekwa nyara.

Tamko la Rais Kikwete limeimarisha agizo la Tume ya Taifa ya Uchaguzi lililotaka watu waende nyumbani baada ya kupiga kura na agizo likatiliwa nguvu na Jeshi la Polisi lililokataza watu kuwepo kwenye maeneo ya vituo ili kuzuia uchochezi wa vurugu siku ya uchaguzi.

Lakini, katika kuonesha hofu inayojengwa na Serikali na Polisi kuhusu suala la wananchi kuwa macho dhidi ya wizi wa kura, Mallya amesema vitisho vya Rais Kikwete vipuuzwe kwa kuwa “yeye si kazi yake na wala hajui sheria za uchaguzi.”

“Tunaomba wananchi wote wapenda mabadiliko baada ya kupiga kura wasiondoke eneo la tukio. Sawa mawakala wanakazi yao, lakini pia wananchi wanaweza kutoa msaada wa kuripoti vitendo vyote viovu vitakavyofanyika baada ya upigaji kura,” amesema Mallya.
Amesema iwapo kutatokea vurugu nje ya vituo vya uchaguzi, Rais Kikwete atabeba dhamana kwa sababu, “wananchi wanayo haki ya kusimamia kura zao dhidi ya kuibwa kama inavyotokea katika uchaguzi ambapo wagombea wa CCM hutangazwa washindi kwa kura za wizi.”

Akasisitiza kwamba Rais na wakuu wa Polisi watawajibika pakitokea vurugu kwa sababu ya hatua ya wananchi kulinda kura zao.
“Vurugu zikitokea, ni wao pamoja na wasimamizi wa uchaguzi ndio watakaoshitakiwa katika Mahakama za Kimataifa hasa kwa vile waangalizi wa uchaguzi kutoka ndani ya nje wapo wanaona kila kitu,” amesema.

“Rais Kikwete hana haki wala nguvu ya kuingilia kazi za Tume ya Uchaguzi kwani hana uzoefu wa sheria, asitake kuvuruga amani ya wananchi wapenda maendeleo kwa kuwa anamaliza muda wake,” amesema Mallya ambaye alizungumza akiwa ukumbi wa mikutano Millenium Tower, Makumbusho jijini Dar es Salaam.

Source : Rais atulie, hajui sheria – Mallya | MwanaHALISI Online
 
Sheria Hairuhusu Mkusanyiko Au Maandamano Yasiyoratibiwa Na Kupata Kibali,

Umeelewa swali? kama hukuelewa nimerudia soma tena kisha weka kifungu.


Swali
kunakifungu cha sheria kinachomzuia mpiga kura kukaa nje ya mita 200?

Kama Kipo mleta hoja kiweke hapa.
 



Ukawa wapuuzi kweli
Sasa unalinda kura ukiwa nje wakati kura zinahesabiwa ndani
Upuuzi mtupu
Na uharo
Huu

Kwan hamna mawakala?

".......mtu akikuambia upige kura na ulinde kura ..mwambie mzee njoo tulinde wrote..."
Kanali kinana
 
Hy anayesema hakuna sheria,,hv anahic amesoma zaid ya wanasheria wa ukawa,,,elimu inahitajika sn,,,ungetuwekea vifungu vyako hapo juu lkn sio kukurupuka km mlevi hvyo
 


Mwisho hii ni Amri kutoka kwa Raisi wa JMTZ ambayo kwa kawaida haipaswi kupingwa na binadamu yoyote yule ndani ya TanZania na wewe unapaswa kutii tu bila shurti, ni rahisi kihivyo tu!
Kwa jambo ambalo lina muongozo wa kisheria hata rais hana mamlaka ya kutoa maagizo/amri kinyume na matakwa ya kisheria. Hivyo, amri ya kuwaambia wananchi wakishapiga kura waende majumbani haina mashiko.
Kwa mwananchi ambaye ana shughuli zake mita 200 toka kilipo kituo cha kura sheria ina mruhusu kuwepo eneo hilo na kufanya shughuli zake. Amri hii ya JK ni batili na kifupi hakuna atakayeitii. Vilevile, Tanzania ya leo sio ya kutishiana kibabe babe! Watu wanaelewa haki zao.
 
Hy anayesema hakuna sheria,,hv anahic amesoma zaid ya wanasheria wa ukawa,,,elimu inahitajika sn,,,ungetuwekea vifungu vyako hapo juu lkn sio kukurupuka km mlevi hvyo

Usiombe Unijue, Sikuweka Vifungu Ila Nimewaletea Kilichoandikwa Kwenye Vifungu, Sasa Unadhan Nan Mnyika Ndo Anaweza Kufika Hata Nusu Yangu? Mnyika Ambaye Hakumaliza Shule? Au Unamaanisha Mbatia Alodisco Akaenda Kupata Course Fupi Nje? Au Unaongelea Sugu Msomi Wa Mbeya? Labda Unamsema Makaidi? Mungu Amlaze Pema Peponi, Au Unamsema Mbowe Aliyegraduate Bill Canaz, Au Wamsema Nan? Lissu Anayedesa Kila Kitu, Hasa Utanilinganisha Na Nani Hapo Chadema? Au Hujajua Nani Kapost Hii? Ebu Uuliza KAOROGOMA ni nani, nenda oxford uliza jina ilo nimepataje
 

Acha ujinga jaribu kusoma, kusikiliza na kuelewa kinachoongelewa, Serikali imesema hairuhusiwi kukusanyika, wametumia neno ,,kukusanyika"!

isitoshe ni sheria gani ya nchi ambayo Raisi wa JMTZ ameivunja?
 

Kama huna unalojuwa kaa kimya.

Otherwise weka vifungu kusapoti hoja yako.
 
Acha ujinga jaribu kusoma, kusikiliza na kuelewa kinachoongelewa, Serikali imesema hairuhusiwi kukusanyika, wametumia neno ,,kukusanyika"!

isitoshe ni sheria gani ya nchi ambayo Raisi wa JMTZ ameivunja?

Sawa wametumia sheria ipi kuzuwia mikusanyiko? Kwa maana ya wapiga kura.

Ukituwekea vifungu halisi tutakuelewa.
 
Acha ujinga jaribu kusoma, kusikiliza na kuelewa kinachoongelewa, Serikali imesema hairuhusiwi kukusanyika, wametumia neno ,,kukusanyika"!

isitoshe ni sheria gani ya nchi ambayo Raisi wa JMTZ ameivunja?
Mjinga ni wewe ambaye unatishiwa kwenye haki yako na sheria ipo wazi. Nipo kwenye eneo langu la kazi mita 200 toka kituo cha kura, nimekusanyika? Nyoko wee!
 

Kwa post yako ni dhahiri rushwa kwenye uchaguzi IPO,, makamanda tutalinda kura, haijalishi ni mita ngap,, hizo million 10 starudi kwa walipa kodi,
#ccmout
 
1. ELIMU 2. ELIMU 3.ELIMU Ndugu yangu nxhi haingozwi na matakwa ya rais bali na katiba ambayo ndio sheria Mama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…