Hakuna kitu kibaya hapa duniani kama madeni

Hakuna kitu kibaya hapa duniani kama madeni

666 chata

JF-Expert Member
Joined
Mar 14, 2013
Posts
1,700
Reaction score
3,921
1. Wakati flani nikifanya shughuli za kisheria ktk taasisi flani niliwai kukutana na mzee mmoja ambae kwa wakati huo alikua ana lala stendi ya mabus ubungo terminal, baada ya kutolewa kwenye nyumba yake kinguvu na watu wa bank kisa alishindwa kurejesha marejesho yake kwa wakati ambapo mpaka anatolewa alikua amebakiza Tshs milion tano tu. Kwa aibu familia aliihamishia kijijini kwao huko kusini na yeye kubakia hapa dar anapambania haki yake na hakua na kazi yoyote ile isipokua hio nyumba ndio alikua ana frame ambalo ndio lilikua duka linalo endeshea familia na hata mkopo aliokopa ulitumika kuliendeleza ilo duka ila mwisho wa siku ikawa ndio ivyo. (Tulipambana sana tukashinda, ila mpaka leo kesi inaendelea kwenye rufaa jamaa walikata rufaa na mzee hana makazi maalum).

2. Rafiki angu mmoja alipata ajali ya gari mwaka 2021 akalazwa hospital karibu miezi sita, akiwa kitandani alikua ana letewa wito wa kulipa madeni na samani za mahakamani, alikua ana changanyikiwa ananiambia "kinachoniuma sasa iv sio haya maumivu ya ajali niliyopata ila ni haya madeni, nachelewa kupona sababu ya simu za wadeni wangu". Alipata ajali wakati anadaiwa na watu kama sita na hakuna aliekua ana muelewa wanaona ajali ni story ya kutunga, askari polisi wamewai kufika kitandani alipolazwa kama mara mbili na wakaondoka, alikua haponi na anazidi kukonda sababu ni bill za hospitali na madeni ya watu vinapishana mlangoni.

3. Wakati flani nikakutana na mama ambae alikua ana mtaji wa milion 100 uliisha kisa mapenzi anavyodai, na baadae aka kopa milion 50 bank moja hapo posta na dhamana ikiwa ni nyumba yake aliyoijenga yeye mwenyewe hapo ukonga, wakati anafanya biashara alikua na ujauzito, akapata matatizo ya miguu, biashara yake ya kuuza viatu hapo karume ikawa na changamoto sana, mwisho vijana wake wakauza mzigo wote kwa bei ya hasara wakakimbilia south, wiki moja baada ya kujifungua ile benk ikaja na mabaunsa na madocument ambayo yanaonesha mnada ulifanyika muda tu so atoke kama alivyo na kila kitu akiache, kilichotokea alihifadhiwa na jirani yake hapo na akaona familia nyingine imehamia kwenye hio hio nyumba na wanavaa hadi kanga zake na wanatumia kila kilichokua ndani.

Madeni hayazoeleki na madeni hayaendeki kwa waganga, kama kutakua na uwezekano usikope kabisa au kopa ukiwa na plan A,B,C mpaka Q.

Sijajua wewe utakua una visa vipi vya madeni? au ulikwepa vp madeni? Tuambie tujifunze na tuchukue taadhari.
 
Halafu utamsikia mchungaji sijui wanajiita wenyewe “mtumishi wa Mungu” anahubiri ameinua mkono juu anasema “wewe unaedaiwa madeni yako yanaenda kuisha sasa” jitu na akili zake linaitika amen ukimuuliza ile 700K ya jamaa uliyokopaga mpaka sasa umerudisha bei gani anakwambia sijarudisha hata mia.

Madeni ni mabaya kaka yangu 2012 hawa access bank waliuza nyumba yake pale Mburahati kwa deni la Tsh 1.7mill na jela wakataka kumtia.
 
Wazee wa kukopa salary advance uzi unawahusu?

Kuna mtu nilimkopesha hela, tokea January mpaka dk hii ni dana dana mwa mwiii mpkaa nimechoka.
Laki na nusu naanzaje tu kuipotezea? Kwa hela zipi nilizo nazo!! Nimempa last chance ya mwezi huu, nao unaelekea kuisha yuko kimya aibu haoni. Naumia basi tu 🥺🥺


Nyieee mkikope na mjue kulipa, nimejiambia mimi tena kukopesha? Labda nikuone hapo unaelekea kufariki
 
Wazee wa kukopa salary advance uzi unawahusu?

Kuna mtu nilimkopesha hela, tokea January mpaka dk hii ni dana dana mwa mwiii mpkaa nimechoka.
Laki na nusu naanzaje tu kuipotezea? Kwa hela zipi nilizo nazo!! Nimempa last chance ya mwezi huu, nao unaelekea kuisha yuko kimya aibu haoni. Naumia basi tu [emoji3064][emoji3064]


Nyieee mkikope na mjue kulipa, nimejiambia mimi tena kukopesha? Labda nikuone hapo unaelekea kufariki
Polesana
 
Wazee wa kukopa salary advance uzi unawahusu?

Kuna mtu nilimkopesha hela, tokea January mpaka dk hii ni dana dana mwa mwiii mpkaa nimechoka.
Laki na nusu naanzaje tu kuipotezea? Kwa hela zipi nilizo nazo!! Nimempa last chance ya mwezi huu, nao unaelekea kuisha yuko kimya aibu haoni. Naumia basi tu 🥺🥺


Nyieee mkikope na mjue kulipa, nimejiambia mimi tena kukopesha? Labda nikuone hapo unaelekea kufariki
Inaudhi kwa kweli. Wakija kukopa wanakuwa wapole mpaka wanatilisha huruma, na wanaahidi watarudisha on time. Wakishapata mkopo sasa... Weeee.. utawasikia kwenye redio za mbao tu. Ukja ipata hiyo pesa uliyomkopesha, shukuru Mungu. Sasa hivi mie nimejifunza. Sikopeshi mtu wala sikopi kwa mtu. Hata wanione mbaya vipi, halinihusu!!
 
Wazee wa kukopa salary advance uzi unawahusu?

Kuna mtu nilimkopesha hela, tokea January mpaka dk hii ni dana dana mwa mwiii mpkaa nimechoka.
Laki na nusu naanzaje tu kuipotezea? Kwa hela zipi nilizo nazo!! Nimempa last chance ya mwezi huu, nao unaelekea kuisha yuko kimya aibu haoni. Naumia basi tu 🥺🥺


Nyieee mkikope na mjue kulipa, nimejiambia mimi tena kukopesha? Labda nikuone hapo unaelekea kufariki
Tupo Tunapita Mbali, Huku Tunasonya Na Kutema Mate Mbali Sana


Haa
 
Stress za madeni hazipishani sana na zile stress za kusubiria majibu ya ngoma hali ya kua unajua ulicheza pekupeku na mtu anaetangaziwa kitaa kizima kua ni mgonjwa na lengo lake ni kusambaza upendo ili asiondoke peke yake.
 
Stress za madeni hazipishani sana na zile stress za kusubiria majibu ya ngoma hali ya kua unajua ulicheza pekupeku na mtu anaetangaziwa kitaa kizima kua ni mgonjwa na lengo lake ni kusambaza upendo ili asiondoke peke yake.
😂😂😂😂
 
Wazee wa kukopa salary advance uzi unawahusu?

Kuna mtu nilimkopesha hela, tokea January mpaka dk hii ni dana dana mwa mwiii mpkaa nimechoka.
Laki na nusu naanzaje tu kuipotezea? Kwa hela zipi nilizo nazo!! Nimempa last chance ya mwezi huu, nao unaelekea kuisha yuko kimya aibu haoni. Naumia basi tu 🥺🥺


Nyieee mkikope na mjue kulipa, nimejiambia mimi tena kukopesha? Labda nikuone hapo unaelekea kufariki
Haahhahaahha doooh pole mkuu.
 
Madeni upunguza kitambi na kuchangamsha akili
Kama una Nia ya kulipa lakini?

Uwe unaumia sana kushindwa kulipa.

Lakini kawaida ya Walivyo hapendi kulipa madeni, hata kama wakipata pesa.

Jitu unalidai lakini linanenepa tu na linakunywa BIA.
 
YONO auction ili ufanye kazi kwao sifa kuu uwe na roho mbaya!

Na hiyo Roho mbaya unatakiwa uithibitishe kwenye INTERVIEW!
unaweza kwenda na kuku ukamchana chana na mikono au unaweza kumkamata paka ukamla nyama mbichi...
Au unaweza piga kichwa ukutani, damu ikitoka unajilamba!

Baada ya hapo kituo kinachofuata ni kwa mteja ndipo atajua hajui

Kukopa sherehe kulipa msiba

Unachukua mkopo wa 100mil unanunulia nyumba au gari!
Wakija kuchukua nyumba yao sioni kama kuna tatizo MAANA ULIKUWA HUNA KITU ndo maana ukakopa,sasa wanachukua kukuacha ulivyokuwa sioni kama ni shida!
KOPA KUJAZIA PALIPOPELEA, SIYO UNAKOPA KWA KUDANGANYA VIELELEZO
 
YONO auction ili ufanye kwao sifa kuu uwe na roho mbaya!
Na hiyo Roho mbaya unatakiwa uithibitishe kwenye INTERVIEW!
unaweza kwenda na kuku ukamchana chana na mikono au unaweza kumkamata paka ukamla nyama mbichi...
Baada ya hapo kituo kinachofuata ni kwa mteja atajua hajui
Hahaaa, duh! Balaa
 
Majembe Auction Mart

YONO auction ili ufanye kwao sifa kuu uwe na roho mbaya!​

Na hiyo Roho mbaya unatakiwa uithibitishe kwenye INTERVIEW!
unaweza kwenda na kuku ukamchana chana na mikono au unaweza kumkamata paka ukamla nyama mbichi...
Baada ya hapo kituo kinachofuata ni kwa mteja atajua hajui
 
Back
Top Bottom