Hakuna mama mkwe anaempenda mkwe wake 100%

Hakuna mama mkwe anaempenda mkwe wake 100%

Its Pancho

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2018
Posts
15,966
Reaction score
26,404
Wakuu

Huwa sipendi kuficha

Kwenye ndoa zetu hizi mama mkwe kumpenda mkwewe asilimia mia ni kitu ambacho hakiwezekani. Huwa wanawapenda ki-uongo tu na ki-nje nje. Sababu kubwa ni kuwa kutokana na upendo wa mama kwa mwanae huona Kama mtoto wake anapoenda kuoa inamaana yeye (mama) ni kama anamkabidhi mwanae akatunzwe sasa na mwanamke mwengine..! Japo haiwezekani mama kuzuia hilo lazima protocol ziende kama zilivyo. Matokeo yake

Mama kama anakaa hapo kwa mwanae Visa vitaanza dhidi ya mkwewe kila kukicha visivyo na kichwa wala miguu. Na sisi watoto wa kiume tunajikuta tunamsikiliza mama zaidi kwenye utetezi wao wote wawili.

Kumbe tunawaumiza wake zetu sana na huenda wanatupenda sana na ndo maana wameamua kuishi na sisi majumbani na kuondoka kwao,
Kuchukua jina lako na kuacha la baba yake.

Nakumbuka nilipokuwa mdogo mama yangu aliteseka sana kutokana na usumbufu na ugomvi usiokwisha kila siku kutoka kwa bibi mzaa baba (alikuwa katoka musoma) .
Siku nyingine akisalimiwa haitiki usiposalimia anasema kwa baba kwamba mkewe (mama) ni jeuri.

Siku moja mama alikuwa anamwaga maji nje na bibi amekaa mbali kwenye mkeka ghafla akaanza kupiga kelele(bibi) huku akimuita baba
"mwenga amenimwagieko maji "

Kwamba mama amemwagia maji mguuni. Huku analia. Akaulizwa yako wapi uliyomwagiwa? Hakuna..! Kakazana tu anasema atamlaani baba kisha anatishia kubeba mizigo arudi musoma...! Visa vingine vingi.

Since kipindi hicho nimejifunza mke ukae nae wewe na mama yako asikae hapo mjengee nyumba jitahidi au kama ana kwake na baba waache wakae Wale uzee wao..

Usijaribu
 
Na huu ndo ukweli

Wanaume wanaposhindwa kuelewa ni kuwa wanawake wote wana vijitabia vinavyofanana regardless ni watu wazima au vijana! Awe mama yako, dada yako au mkeo kuna tabia tu wote wanazo especially kuzira au maneno mengi.

Sasa unapoamua kuwaweka watu hawa pamoja uwe makini haswa as unaeza mpoteza mmoja ukagain mmoja(hapa itategemea nani anamzidi mwenzake maneno)
 
Wakuu
Huwa sipendi kuficha
Kwenye ndoa zetu hizi mama mkwe kumpenda mkwewe asilimia mia ni kitu ambacho hakiwezekani. Huwa
Eeh mara mia mkapange kuliko kukaa na bi.Mkubwa mwenye itikadi za kishamba! Kama unamjua mama yako mtu wa kuongea ongea na kupenda attention jua atamchukia mkeo tu hata iweje 😂😂😂
 
Wakuu
Huwa sipendi kuficha
Kwenye ndoa zetu hizi mama mkwe kumpenda mkwewe asilimia mia ni kitu ambacho hakiwezekani. Huwa wanawapenda ki-uongo tu na ki-nje nje. Sababu kubwa ni kuwa kutokana na upendo wa mama kwa mwanae
TAFUTA PESA wewe boya!
 
Eeh mara mia mkapange kuliko kukaa na bi.Mkubwa mwenye itikadi za kishamba! Kama unamjua mama yako mtu wa kuongea ongea na kupenda attention jua atamchukia mkeo tu hata iweje 😂😂😂
Vinginevyo cha moto utakiona 😀😀
 
Mkeo anampenda mama mkwe 100%?

Dawa pekee ni kuhakikisha hawakai sehemu moja kwa muda mrefu.
Hilo siwezi jua kiufupi sijui kama wanapendana
Sasa hata kama hampendi utafanyeje zaidi ya kumuepusha na mama? Utanyandua wapi?
 
Na huu ndo ukweli
Wanaume wanaposhindwa kuelewa ni kuwa wanawake wote wana vijitabia vinavyofanana regardless ni watu wazima au vijana!awe mama yako,dada yako au mkeo kuna tabia tu wote wanazo especially kuzira au maneno mengi
Sasa unapoamua kuwaweka watu hawa pamoja uwe makini haswa as unaeza mpoteza mmoja ukagain mmoja(hapa itategemea nani anamzidi mwenzake maneno)
Asiyesikia na asiskie mkuu
 
Shida niionayo kwetu wanawake na mama wakwe zetu ni moja. Kutokutambua nafasi zetu na kutaka mashindano baina yetu. Yapasa mama mkwe ajue kua yeye ni mama wa mwanaume na wala hakuna wakumpindua na asilete ushindani na mke pia kujua yeye ni mke wa mwanaume husika kwa wakati huo kwa imani wanayo fungamana nayo.

Hivyo hakuna anaepaswa kushindana kuchukua nafasi ya mwenzie kwan hivi ndivyo Mungu alivyoamrisha. Mama ashike nafasi yake ya umama na mke ashike nafasi yake ya kuwa mke na mume awajibike kwa wote kwa kumtunza mama na mke na pia awe na msimamo la sivyp hyo ligi ya mama mkwe na mkwewe haitoisha kamwe
 
Back
Top Bottom