Hakuna mfanya biashara aliyeporwa fedha zake, kuwarudishia ni mbinu nyingine yenye ufisadi na viongozi kutengeneza biashara zao wenyewe!


[mention]Paulsylvester [/mention] Hoja Yako ina Mashiko Makubwa na Jicho Pevu Sana, hii ni kwa Big Thinkers tu ndio wataelewa.

Naamini mtoa maada bila shaka unatambua kuwa ni kweli Wapo walioumizwa kwa kuporwa Mali zao ndio wanaotakiwa kunufaika isipokuwa tu Wapitie utaratibu rasimi wa Kwenda Mahakamani na Mashauri yao yaamuriwe na Mahakama.

Kufanya hivyo itafahamika ni nani anayestahili kulipwa na nani hastahili , mbali na Hilo fedha zitakazotakiwa kulipwa kwa waasirika zitafahamika, na Sio tu Wahuni Vigogo Serikalini kujifanya Mahakimu na Kutaka Kulipa Mali ya Umma kwa Watu tu wanaosadikika kuwa waliporwa wakati ukweli haujafahamika publicaly.


Hapa Wasaka Tonge Wapo hewani Kupiga Dili, Time will Justify this
 
Hapo Serikali inakiri ujambazi wa marehemu, siyo Serikali. Pesa haikuporwa na Serikali, iliporwa na Magufuli, na wala haikupelekwa Serikalini.
 

Unafikiri ni Sahihi kuwa Mtu Ukimkosea Kwa Kumtukana nae Aje Alipize kwa Kukutukana, this is a bit terrible Lol,

Utawala wa Kisheria mbona hamtaki ufuatwe, Kufanya hivyo ni kuignoo Mahakama.

Hata kama Serikali ilipora hela za Watu bila Kushirikisha Mahakama, Lakini bado tu haiwezi kuwa Sahihi Watu Kurudishiwa wanachodai bila kushirikisha mahakama ambayo inamamlaka ya Kuamua yote hayo.

Utaratibu ufuatwe, sheria na Taratibu zipo ili zifuatwe.

Kufuata Utaratibu hela Nyingi za Walipa Kodi Zitaokolewa na Waasirika watapata haki zao.
 
Fisadi mkuu alikuwa ni Magufuli. Alisema anatumbua vyeti fake, mbona hakumtumbua Makonda, Mwigulu au Kigwangala, ambao wote mpaka leo wanatumia majina yasiyo yao?

Marehemu alikuwa ni mtu mnafiki mkubwa. Alikuwa kiongozi mwongo, laghai na mwizi (trilioni 1.5 mpaka leo haijulikani alipeleka wapi. Pesa aluziwapora aliowabambikia kesi za uhujumu uchumi, alizichukua yeye binafsi).
 
Pole ndugu yangu.

Utambue kuwa SHETANI ana mtiririko wa uongozi. Ule utawala ulikuwa utawala wa shetani. Yule alikuwa ni shetani katika umbile la mwanadamu. Na katika kutekeleza ule ushetani, ni lazima awe na wasaidizi, mmojawapo ni kama huyu mleta mada.

Aliyeondoka Duniani, niyeye pekee yake, wale mawakala wadogo wa shetani bado tunao, na wataendelea kufurukuta kwa kila namna, lakini Mungu hatoi nafasi mara mbili kwa shetani.
 
Siyo kila jambo huamliwa na mahakama. Kuna masuala mengine ni ya kiutawala, yanaamliwa kwa kupitia ofisi za kiutawala.

Na ndiyo maana hata kwenyr mikataba yote, utaona kuna kipengere kinasema, endapo kutatokea mgogoro, pande zinazohusika zitajitahidi kuumaliza mgogoro huo kimaelewano, na endapo njia zote za maelewano zitakuwa zimeshindikana, upande ambao haukuridhika utakwenda mahakamani.

Kama kila jambo maamuzi ni mahakamani tu, basi kusingekuwa na ofisi za utawala mahali popote. Kila suala ingeachiwa mahakama iamue.

Kama wahusika wakuu ambao ni Serikali na walioporwa pesa na marehemu wamekubaliana, tatizo liko wapi? Wewe kama mlipa kodi, kama hukuridhika na makubaliano kati ya Serikali na Walioporwa pesa na marehemu Magufuli, una uwezo wa kuishtaki Serikali na hao waliolipwa pesa yao.

Siku zote, kwenye suala madai, mahakamani huwa ni hatua ya mwisho baada ya pande zinazohusika kushindwa kukubaliana.
 

[mention]Bams [/mention] hakuna mtu anayebisha kuwa Watu hawakuporwa, Yawezekana hata wewe ulikuwa Muathirika pia na wote wanastahili kupewa haki zao na Ikibi na Faida juu.

Hoja ya Msingi hapa ni kwamba, isije ikatokea watu ambao hata Tsh 100 Hakuporwa ila kwa Sababu anamamlaka tu basi nayeye anapitishiamo Dili la Kupigia hela, [mention]Bams [/mention] lielewe hili, hamna anayepinga hoja yako Mkuu.
 
Hapo Serikali inakiri ujambazi wa marehemu, siyo Serikali. Pesa haikuporwa na Serikali, iliporwa na Magufuli, na wala haikupelekwa Serikalini.
Wanasemaga Rais wa Jamhuri ni icon ya Serikali. Tutatofautishaje?
 
Hivi nyinyi mnadhani Magufuli alivyokuwa anapora hela za watu ilikuwa siri ? Kwani aliokuwa anawatuma nao wamekufa ? si kafa yeye tu ! Ushahidi wa uchafu wake uko nje nje mbona !

Unawafahamu hawa hapa pichani , unajua hapa walikuwa wanafanya nini ?

Kama hukuwahi kunyang'anywa hela na Magufuli , Just Shut Up !

Philipo Mpango ndiye alikuwa Waziri wa fedha unadhani hakuyajua haya ?

 
Hivi unajua kwenda mahakamani nini kingetokea? Utalipa hiyo pesa pamoja na riba. Kama unajua umefanya kosa na huwezi shinda kesi, lipa hela za watu!
 

Kalale, hujui kuna gharama kuanzisha kesi
 
Asante mkuu, na ubarikiwe, hii nchi ni yetu sote, tulijiwekea sheria na taratibu, basi ni vema tukaifuata na sio kuzivunja na kutoheshimu mihimili mingine
 
Reactions: Ame
Lugha yako hii ya kijinga haikuondolei sifa zako za kufoji na kutumia majina ya watu ili hali wewe hata shule huna ni form four felia

Yaani serikali Iwe na dirisha la kulipa kila anayelalamika kuporwa fedha!

Tunaweza kujitahidi kuondoa maradhi na umasikini, ila ujinga!! Sielewi ikiwa kweli utawaisha wehu wa ccm
 
Kwani sasa bado hizo button zipo, si waende sasa?
 
Ukisemacho hiki, peleka mahakamani mkuu, acha kujifanya mjinga eti serikali ilipe kila anayelalamika kuibiwa
 
Serikali ikianza kulipa tu fidia kwa sabb kuna watu wamelalamika kuporwa na serikali hiyo, bila mlalamikaji kwenda mahakamani na mahakama ikajiridhisha, huo ni ufisadi tuu hakuna jina lingine zaidi ya hilo
Nitashangaa zaidi kama na Bunge nalo litakaa kimya haya yakifanyika
 
Kwa mfano kuna yule mhuni anadai alimpa sabaya rushwa eti ni moja wapo ya mambo alishitakiwa nayo sabaya.
Mtu kama alitoa rushwa wakati wa awamu ya 5 iweje yeye haonekani ni mkosaji ila sabaya ndio amebanwa kwa kuhongwa. Mambo ya uhuni tu.
Serikali hii inaweza kabisa kuja na wahuni wakidai warejeshewe hela eti walidhulumiw awamu ya 5 na kisha wakalipwa.
 
Kuna kichaka kitatumika kuiba pesa ya umma.Madai halali yatabaki halali iwapo mahakama imeyathibitisha .Mahakama kwa sasa iko huru zaidi ya wakati ule !
 
Hiyo inanisaidiaje Mimi common mwananchi naekosa Maji na umeme na gharama za maisha zikiwa juu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…