Hakuna sehemu iliyo salama hapo kariakoo

Hakuna sehemu iliyo salama hapo kariakoo

DON YRN

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2019
Posts
606
Reaction score
1,453
Ni kweli tupo kwenye majonzi kama Taifa hivyo yatupasa kushikamana na kuondoa tofauti zetu na kuwa kitu kimoja katika kipindi hiki kigumu kama Taifa.

Nimesikia kauli ya mheshimiwa Rais kuwa serikali itabeba gharama zote za matibabu kwa waliojeruhiwa na kwamba baada ya zoezi la uokoaji kukamilika amemtaka Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, kuongoza timu ya wakaguzi majengo ili kukagua eneo lote la Kariakoo na kupata hali kamili ya majengo katika eneo hilo.
Ni jambo jambo jema sana.

Bila kufichana wala kupepesa macho, hapo kariakoo hakuna sehemu iliyo salama, pameharibika pote.
Leo hii ukaguzi ukifanyika, majengo hayatazidi 20 yaliyo salama mengine ni magumashi tu na hii yote ni RUSHWA iliyokithiri wanayopokea hao waliopewa dhamana ya kusimamia na pia wengi wao hawana weledi sababu ya kauli ya "huyu mtoto wa mjomba tumuweke hapa"

Leo hii ikatokea tetemeko la ardhi kama Japan, hakutakuwa na eneo lolote kukimbilia usalama sababu hakuna sehemu ya wazi. Kinachofanyika sasa kariakoo ni ujenzi holela wa majengo yenye kiwango cha chini kupitiliza

Pia soma: Live Updates Kuporomoka kwa Ghorofa Kariakoo Nov 16: Watu 7 wengine waokolewa

Kinachotakiwa kufanyika kwa sasa katika eneo la kariakoo ni Demolition kama inayofanyika Gaza kisha tuanze upya.
Mfano, leo hii nilikuwa hapo china plaza, lifti zote mbovu
 
Back
Top Bottom