Hakuna Taifa lililoendelea kwa ziara za Rais Nje ya Nchi

Moja ya mada muhimu sana toka kwako, na kiujumla hapa JF.

Imewasilishwa vizuri, bila mihemko na unazi uliozoeleka toka kwako.

Lakini kidogo inachanganya. Unazungumzia "ziara" au "uwekezaji" (kufungua nchi)?

Uwekezaji toka nje ni muhimu, ninakubaliana kabisa na hilo, lakini kama ulivyoeleza, "ufunguaji wa nchi unafanyika kimakosa", kama ulivyoeleza, kwa vile tunafungua tu huku tukiwa hatuna uwezo wa kumiliki huo ufunguzi. Tunajiachia tu waje wafanye, huku sisi tukiwa tupotupo tu, wakati hatujui lolote. Huu ni upumbavu.

Jambo ambalo nami ningependa kulikazia hapa ni hii dhana potofu kabisa aliyo nayo Samia ya kudhani kwamba Tanzania itaendelea kwa vile watu wanakuja kuwekeza hapa bila ya mipango maalum. Hili litakuwa ni jalala la uchafu.
Maendeleo ya nchi hii yanawategemea waTanzania wenyewe kuyaleta. Juhudi kubwa zaidi zingeelekezwa huko kwa wananchi wenyewe. Wawekezaji muhimu kabisa katika maendeleo ya nchi hii ni waTanzania wenyewe.

Mama hili kalitupa mbali kabisa, anachojua yeye ni "kufungua tu nchi."

Mafuta ya kula, kwa mfano ya Alizeti, nayo mpaka tusubiri wawekezaji waje hapa ndio tuweze kutosheleza mahitaji yetu? Mifano ya aina hii ipo tele, na katika yote hiyo, hatuhitaji hata miaka mitano kujitegemea wenyewe katika mahitaji ya vitu hivyo na kuuza nje.

Tunafanya nini na elimu yetu, ili hao wawekezaji wanapokuja hapa tunafuzu kupata teknologia yao ambayo itabaki hapa hapa sisi tukiitumia kwa manufaa yetu.
Kuna hizi nyimbo zinaimbwa kila mara kwamba ni lazima wawepo waTanzania wanaoandaliwa kuchukua nafasi za wageni baada ya muda maalum. Huyu mama anajua kinachofanyika huko? Ameweka msisitizo wowote na ufuatiliaji kujua kuwa hili jambio muhimu linatimizwa? Yeye kazi kubwa aliyofanya hadi sasa ni "kufungua nchi tu", bila kujua anaifungua tupate faida ipi. Haandai mazingira ya kufaidika na ufunguzi huo.

Mama Samia ni lazima abadili mwelekeo, anakotupeleka siko kabisa.
 
Safari ya wiki mbili kwa ajili ya filamu kama Taifa kuna manufaa ya hili??
Bila shaka hii itakuwa imeweka rekodi ya dunia, kwa kiongozi wa nchi yeyote kuwahi kuwa nje ya nchi yake, bila ya dharura kwa muda mrefu kiasi hiki.

Kwani isingetosha kufanya ufunguzi mahali pamoja, na kurudi nyumbani, na huko kwingine wakaendelea wasaidizi wake?

Ina maana ofisini kwake hakuna kazi muhimu zaidi ya hii ya ufunguzi wa movie?

Very bad judgement on her part and that of her handlers.
 
Haya sasa. Unafungua nchi na hujui unaifungua ifanye nini wakati hukuweka maandalizi sahihi ya kufaidika na ufunguzi wenyewe!

Wawekezaji wanakuja hapa wanakwambia watu wako ni wabovu, hatuwezi kuwapa kazi, tunataka tulete wa kwetu. Badala ya kustuka na kuona tatizo lipo wapi ili ulirekebishe, wewe unakaza mwendo wa ufunguzi na bado unaamini utafaidika na ufunguzi huo!
 
Buni mbinu zako zinazo lingana na mahitaji na mazingira uliyomo na watu wako kwa kutumia akili zako zinavotenda kazi!!....hii kuiga iga ndo inazidi kuwafanya muwe wajinga wa kukaririr hovyo na maskini mpaka leo!
Ntakujibu hapa tu huko kwingine kote umebwabwaja.... UKISHASEMA BUNI MBINU ZAKO umerejea nilicho kiandika hapa full stop...

Sisi tunahitaji uchumi wa kisayansi ambao unahusisha elimu,tafiti, technolojia, uzalishaji rahisi wenye kuhususisha raslimali watu na muindo mbinu.

Technology ni uwezo, usanii, ufundi".

Teknolojia inaweza kumaanisha: vifaa na mashine zinazotumika katika matengenezo au uzalishaji wa vitu elimu ya matumizi yake pamoja na mbinu na maarifa jinsi ya kutumia sayansi uwezo wa kubadili malighafi asilia na kuwa bidhaa yenye thamani inayoweza kukidhi mahitaji ya binadamu.

Unamawazo ya drone, ya kale unaamini kwenye fikira kandamizi huna ubunifu, utakuta unamipango inayoanguka kila uchao. Tafuta watu wakusaidie kunyumbua fikira zako. Pata consultant wakusaidie.
 
Sasa kuna kampuni ilikuwa ina wageni 3 maana walibanwa awamu iliyopita kulocalise positions kama 7 na ajabu wazawa walikuwepo na wakapewa hizo kazi. Ajabu katikati mwaka jana wamewarudisha wageni speed ya 5G na sasa wazawa wale wameondolewa kupisha wageni. Je, kwenye practice ya localisation unaweza kureverse tena iwe foreignization.....???
 
Kaka hii nchi ina watu wenye vichwa vibovu sana tena haswa vijana. Yani wao hata kumbukumbu hawana, wao ni ushabiki tu wala hawatazami mambo kwa mapana. Yani hata katika mambo ya maendeleo wao ushangilia tu team zao kama kule ktk muziki team Kiba na team Diamond
 
Ntakujibu hapa tu huko kwingine kote umebwabwaja..
Hilo bado ni jibu rahisi kwa hoja nzito! huna uwezo nazo! bora umepita!
Sisi tunahitaji uchumi wa kisayansi ambao unahusisha elimu,tafiti, technolojia, uzalishaji rahisi wenye kuhususisha raslimali watu na muindo mbinu.
Ndo haya ya UPE .. hee! uzalishaji rahisi!! wapi na wapi!! yaani wenzako wanakimbia wewe unatembea??..utafika lini?? usitudanganye hakuna uzalishaji ambao hauhusishi watu! kasome tena uje.....

Kamwe hutokuwa na miundo mbinu Bora bila uchumi shirikishi unajidanganya kiujima Kwa kuwa Bongo siyo kisiwa!! bado tunawahitaji kama wao wanvyo tuhitaji! sana tu...kuna uchumi ambao si Elimu?? ivi umekula kweli dogo leo!
Unamawazo ya drone, ya kale unaamini kwenye fikira kandamizi huna ubunifu, utakuta unamipango inayoanguka kila uchao. Tafuta watu wakusaidie kunyumbua fikira zako. Pata consultant wakusaidie.
Hujui kuwa hujui ''Ya kale dhahabu!''umewahi jua hii?? .. Fikra kandamizi ni chachu ya Mafanikio kote Duniani! tizama ivi ''Bila Mataifa ya Ulaya kuwakandamiza weusi!!! weupe wasinge kuwa hapo walipo leo!

Angalia tu!! woote walio wakandamiza nyie weusi ndo super power leo! na bado mnakandamizwa barabara kwa fikra mfu km hizi zako!..... en' you are comfortable about it! Lamenting for nothin' gel up! stand up! meeen!
wa
Umetamka vyema ''Kuanguka'' jua ndo kusimama/kuelewa!! so! ni lazima!..... nasema binafsi lazima nianguke tu! ili nisi mame wima kamwe huwezi kusimama tu! kwa maneno mengine ni hivi kupotea njia ndo.......njia! ok! chukulia nadharia ya mtoto mdogo!

lazima atambae kwanza asimame aanguke mara kibao!! ndo ajue kutembea hiyo ni normal kwa binadamu..sasa wewe unataka utembee ghafla! hapa umeropoka Mkuu! kasome tena, then uje!!.......mjuvi wa mambo atafurahia kuanguka!

kwa taarifa yako ku/penda/taka/tamani kusaidiwa ni fikra tegemezi mnoo! km zako!......siyo ubunifu yakinifu! tulifundishwa kujitegemea shuleni na majumbani zamani hizo!...(rejea Elimu ya kujitegema!) natumai ulikuwa mtoro!

so! kuwa tegemezi si ujanja wala haijengi udadisi! ina maana pamoja na uzee wako huo hukuelewa sera mwanana za ''ujamaa na kujitegemea?? kuwa....... ''ndo njia pekee ya kujenga jamii iliyo sawa na huru??.. ....sasa huko shuleni ulisoma nini ndg??

Na hii Mwalimu Nyerere anaikumbusha kila siku mpaka leo palee TBC! Pugu road zamani! waombe wakusaidie! Mfuatilie upate japo Mwanga wa maisha ndo maana nikasema walimu wako wa UPE wamekuingiza mkenge Mzee Baba si wazuri hata kidogo!

lkn km ukiwa mtoto wa miaka 14-18 hivi!! mbona nakusamehe tu bure! najua unajifunza kwetu! sie dada zako ...lkn km ni zaidi ya hapo mweee!!..... bora ukae kimya! .......kaaa!!bisaa!...
 
Mama Samia anakutana na watu potential tu tangu aende MAREKANI...jamani kama inawezekana mama apige tena wiki 2 nyingine....hakuna haraka ya kurudi huku kwa sababu kama mvua zinanyesha na watu wanalima
 
Mama Samia anakutana na watu potential tu tangu aende MAREKANI...jamani kama inawezekana mama apige tena wiki 2 nyingine....hakuna haraka ya kurudi huku kwa sababu kama mvua zinanyesha na watu wanalima
Kweli anaupiga mwingi... hahahahha
 
Foreign Direct Investment ni muhimu katika kuzalisha ajira, hebu tuambie strategy gani wewe unaweza kuitumia kupromote ajira?

#Mama zunguka tuletee wawekezaji vijana wapate ajira,waoe wawe na familia na wao wawekeze waajiri wengine.
Mkuu, kazi ya kutoa ajira ni jukumu la serikali.
 
Malaya design yako dawa yao huwa nawatia mimba wanatulia.
Unanionea wivu! sifa ya Mimba angu!! mbona ndo zetu hatujuti sie!! njoo na weye upewe sina wivu mie! najua huwezi tia mimba ndo maana unaitamani! njoo nikufanyie mpango!
 
Zaidi sana, hakuna taifa , (hasa haya yaitwayo ya ulimwengu wa tatu) lililoendelea kwa viongozi wake kujifungia ndani.
 
Mama Samia anakutana na watu potential tu tangu aende MAREKANI...jamani kama inawezekana mama apige tena wiki 2 nyingine....hakuna haraka ya kurudi huku kwa sababu kama mvua zinanyesha na watu wanalima
Ikulu ihamie huko kabisa au sio sheikh.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…