mkuu natambua sana unayoyasema yapo, lakini in general bongo ndoa ambazo watu wanapenda kujivunia ni zile rasmi za akanisani, shekh au mkuu wa wilaya
Mimi naangalia zaidi hizi ndoa "rasmi" kwanini zamani haikuwa hivi sana? yaani sasa hivi watu wanokimbilia uzeeni ndio utawakuta kwenye kumbi mbalimbali za sherehe za harusi kama maharusi
Ndoa ikishatambulika na wawili na kisheria ni "rasmi" tayari. Huna haki ya kusema walioamua kukaa katika "common law marriage" hawana ndoa rasmi. Hii ni stigma inayotokana na tradition tu na inafaa kuachwa.
Na kuna watu kibao wanajivunia kuwa katika "common law marriage", kwao wanaona kwamba kuamua wao wenyewe kuwa pamoja bila ya kufungwa na kanisa au serikali kunaonyesha kwamba wametaka kuwa pamoja kikweli na hawajalazimika kuwa hivyo kwa sababu ya tradition.
Kwa hiyo there is a case to be made here kwamba wale unaosema hawana sababu kubwa sana za kujivunia "ndoa" zao (common law marriage) actually ndio wenye sababu kubwa sana ya kujivunia ndoa zao. Hawajamchangisha mtu mchango wa harusi na kufanya harusi ya gharama na hivyo kuhofia kuwa disappoint watu wakiachana, lakini hawaamui kuachana.
Kiujumla, watu wanaangalia traditions nyingi wanakuta ziko overrated. Kwa mfano ndoa, kitu ambacho kimsingi ni makubaliano ya watu wawili, imeenda kufanywa kuwa a pompous circus yenye migharama ya ajabu na spectacle ya kushangaza. Kuna wengine wanaona bughudha hii ya nini wakati mambo ni ya wawili? Ndiyo maana unaona common law marriage zinazidi.
Zamani harusi watu wakipika wenyewe, kinamama kuchambua mchele etc. Siku hizi mpaka matarumbeta, catering services sijui, suti za Savile Row na habari za kushindana misafara. Wengine wanaona hatuwezi haya, bora tufanye kivyetuvyetu.
Kwangu mie bora mapenzi. Kati ya ndoa unazoziita "rasmi" kuna nyingi tu zina matatizo mengi na kati ya hizo unazoziona si "rasmi" kuna nyingi tu za mapenzi ya kweli.
Tukiacha ubaguzi wa ndoa "rasmi" na zisizo "rasmi" tukatambua zote kama ndoa, na kuelekeza juhudi kwenye kuongeza mapenzi ya kweli, tutakuwa tunafanya la maana zaidi.
Na hesabu zetu za ndoa pengine hazitaona mabadiliko uliyoyaona.