Hakuna ubaguzi wa rangi wala mfumo dume, Democrats wameshindwa kihalali kwasababu wameiharibu mno marekani na wangeharibu zaidi wangeshinda

G Tank

JF-Expert Member
Joined
Feb 9, 2023
Posts
2,297
Reaction score
8,760
Kilichopigiwa kura zaidi ni sera ya kuilinda Marekani, Sera za Democrats zimeiharibu sana Marekani,

Haya ni baadhi ya mambo waliyofanya Bidden na Haris kwenye awamu yao, Trump kashinda kwasababu kaapa anaenda kuyafuta na kuyarekebisha.

Mfumuko wa bei na maisha kuwa juu, vyuma vimekaza Marekani, watu wengi uchumi daraja la chini la kati waliofanya kazi 1 kukidho mahitaji yao lakini awamu hii wanafanya kazi 2, Wamarekani wengi hawakuwa tayari kumpa kura Harris kwasababu angefanya maisha yawe magumu zaidi kiuchumi, Vitu vya muhimu kama chakula, mafuta, umeme, Kodi za nyumba n.k vimepanda mno gharama, Ndio sababu ya wanawake wengi wanaoshinda nyumbani wakiwa na uhakika wa kupokea pesa za matunzo na pesa za malezi ya mtoto wamempigia kura Harris lakini wanaume na wanawake wengi wanaojitafutia pesa wamemchagua Trumo

Ongezeko la kodi na kuwatoza kodi wafanyakazi kwenye Tips na overtime, Kwa marekani ni utamaduni uliozoeleka ukiuhudumiwa na watu kama waiter unatoa tip, hii huwa inapigwa kodi, Overtime masaa ya ziada kazini yanapigwa kodi.

Kuruhusu wanaume kubadili jinsia na kuishi kwenye hostel za wanafunzi wa kike, kuoga nao kwenye mabafu, kwenye michezo, n.k. michezoni wanaume wamevunja rekodi nyingi,

Kuruhusu maharamia milioni 20 kuingia Marekani, Siku ya kwanza Biden kuingia ofisini alifuta sheria nyingi za Trump zilizozuia maharamia kuingia nchini, Matokeo yake mipaka ikawa wazi, magenge ya kihalifu yamesafirisha wanawake na watoto wengi sana kuwatumikisha kwenye biashara ya ngono, wahalifu kuanzia wauaji, wabakaji, majambazi, n.k. wanatoroka nchi zao kwenda Marekani, Uhalifu umezidi mno Marekani, magenge ya Venezuela yameanza kuchukua kimabavu apartments.

Kupunguza support kwa Israel mshrika mkuu wa Marekani, Kamala alionyesha dalili za wazi kuwavumilia waandamaji wa Hamas kwa kuwaruhusu kufunga barabara, kuweka kambi vyuoni, n.k. Netanyahu alihutubia bunge la Marekani bila ya uwepo wa Kamala na Biden licha ya wabunge wa Democrats kuhudhuria, Mipango ya Israel kuishambulia Iran ilivujishwa, n.k.

Kuruhusu watoto kubadili jinsia bila ridhaa ya wazazi, hii ilifanya wazazi kupoteza controll ya watoto wanaoshawishika kirahisi

Kufundisha watoto wadogo elimu ya viungo vya uzazi, ikiwemo sex, masturbation, n.k.

Kuruhusu wanawake kufanya late term abortion, kuharibu mimba iliyofikia miezi 9
 
Trump anasema Marekani maisha ni magumu kutokana na uongozi mbovu wa democrats, uchumi ni mbaya, vyuma vimekaza Marekani kutokana na uongozi mbovu wa democrats.


Pia anasema wahamiaji haramu wanafanya uhalifu na kuchukua ajira za wazawa. Inaonekana Marekani kuna ukosefu wa ajira


Chanzo cha Matatizo yote ni democrats
 
Duh! Ilitakiwa Trump aapishwe usiku huu huu na sio kusubiri hadi January, 2025!

Kama hali ndio hiyo wanastahili kabisa kufuata precedence waliyoacha Kivuitu na Kibaki.
 
Ubaya ni kwamba Democrats wamezikamata Media.

Elon alifanya jambo kubwa sana kuinunua twitter, kaipa dunia uhuru wa kupata habari bila upendeleo
 
Hapo uliposema Marekani kuna ukosefu wa ajira ni Uongo.
 
Hapo uliposema Marekani kuna ukosefu wa ajira ni Uongo.
Trump kasema hivyo.

Pia anasema uchumi wa Marekani umeporomoka na kuharibika. Hali imekuwa ngumu sana Marekani hasa kifedha



Ndio maana Trump kashinda kwa kishindo. Usa hakuna uchawa wala maagizo toka JUU.
Tume ya Uchaguzi ya USA wametoa matokeo halisi ya maamuzi ya wamarekani.
 
Ok! Ngoja tuone..
 
Wewe na wanaokuunga mkono mnasikiliza sana uwongo na propaganda za Trump na watu wake; ni haki yenu mfurahia matokeo.

Trump aliingia madarakani wakati uchumi wa marekani unakua kwa 2.9%, unemployement ilikuwa imeungua kutoka 14% hadi kufikia 4.1% na infalation ilikuwa 1.3%. Aliishi kwa momenmtum ya uchumi huo aliorithi ingawa GDP yake ilikuwa inatelemka. Ilipokuja hali inayotaka uongozi wake, akaboronga na kuanguasha uchumi hadi GDP ikafikia -2.21%, unemployement ikawa 15%. Biden akarithi mzigo ambao ameurekebisha hadi sasa hivi uchumi unakuwa kwa 2.8% tena, uneplyment iko 4.1% na inflation ni 2.4%. lakini Trump amekuwa anajisisfia sana kuwa anajua kuongoza uchumi wakati hakuna kitu.

Sasa hivi Trump anarithi uchumi ulioimarika ahalafu atajisifia sana, na watu kama wewe ambao hawako informed.
watachukua uwongio huo na kuufanya kuwa kweli. Utasikia eti crime is too high because of Biden lakini FBI wanakuambia kuwa mwaka 2019 (wakati wa Trump) violent crimes zilikuwa 1,745,570, lakini mwaka 2023 (wakati wa Biden) violent crimes zilipungua na kufikia 1,343,180. Lakini Trump anapiga uwongo kuwa crime is everywehere kama Marekani sasa hivi ni nchi ya hatari sana, halafu watu kama wewe mnakubaliana naye.

Marekani ina watu wengi ambao hawako informed, hivyo Trump kushinda na halali yake.
 
Huwa nikitafakari wanachofanya Democrats, nawaza, au labda hao ni kikundi cha Wachina waliojipenyeza kwenye mfumo wa Marekani na sasa wanaivugura mithili ya kirusi mwilini bila wao kujua?
 
We ndio mungo Tena mpumbavu wa kitumbikwela
 
Kwa ile idadi ya wahamiaji haramu kujaa Marekani, bila shaka uhalifu lazima uwe juu. Hata Tanzania hatuwezi kufanya upuuzi wa kumruhusu kila mtu ajiingize tu nchini bila kibali wala uhalali.

Trump yuko sahihi, ndiyo maana amerejea Jumba Juepe.
 
Democratic ni kama chama cha mataahira. Wamarekani wamewachoka. Chama kina sera za kiwendawazimu.

Kampeni ya Trump ilikua ni restore common sense in USA, maana yake nchi ilipoteza common sense.

Mara eti watoto wadogo wafundishwa kwmna wamezaliw ana jinsia mbaya, wabadilishe tena bila ruhusa ya mzazi. Mara wanaume kushiriki michezo ya wanawake, mara mtu anaweza kujitambulisha kwa jinsia ama rangi yoyote anayoona inamfaa na mambo mengine ya hovyo.
 
Si wanasemaga marekani inaongozwa na mfumo siyo mtu?? Au huwa ni uongo wa majinga Chadema?

Iweje Trump aongoze kivyake na Biden kivyake?
 
Duh! Ilitakiwa Trump aapishwe usiku huu huu na sio kusubiri hadi January, 2025!

Kama hali ndio hiyo wanastahili kabisa kufuata precedence waliyoacha Kivuitu na Kibaki.
Na hao majamaa walivyo haribu nawaza kama hiyo kuapishwa baada ya miezi anaweza kufikiri kubadili sheria,ili kuzuia wahalifu kuendelea kuharibu hata baada ya kushindwa kwenye chaguzi zijazo.
 
The game was brutal but still fair.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…