Hakuna wa kumfikia Adson Arantes Dos`Nacimento (Pele)

Hakuna wa kumfikia Adson Arantes Dos`Nacimento (Pele)

ebaeban

JF-Expert Member
Joined
Jan 15, 2012
Posts
2,205
Reaction score
2,697
Mods tafadhali msiunganishe uzi huu na mwingine wa kuhusu PELE`

Jamani hamna wa kulinganishwa na Pele` wa Brazil. Hamna wa kumfikia Adson Arantes Dos`Nacimento(PELE).

Pele wa Brazil ndiyo mchezaji wa mpira wa miguu wa hali ya juu zaidi kuwahi kutokea duniani mpaka sasa, mimi hapa mwenye uzi wachezaji wote mahili duniani nimewaona wakicheza akiwemo king PELE`, nasema PELE` hamna wa kulingana nae, yaani huyo Maraddona hamfikii PELE` hata robo.

Kwanza nitamlinganisha PELE` na Maradona tu.

NOKIGEZOPELE `Maradona
1umriMiaka 82 na zaidiMiaka 60
2Sheria za mpiraPELE` alicheza wakati wa sheria za zamani, rafu, kukatwa kwa nyuma n.kMaradona amecheza mpira wakati sheria zimeboreshwa hasa kuwalinda mastaa
3ViwanjaWakati wa PELE` viwanja havikuwa vizuri mfano kuwekewa nyasi za bandia na maboresho mengineMaradona kacheza mpira wakati viwanja vimeboreshwa, nyasi za bandia na vikorombwezo vingine
4Kunyanyua kombe duniaKing PELE` amelinyanyua mara 3, Jules Ramet cup mpaka Brazil walilitwaa moja kwa mojaMaradona amenyakua kombe la dunia mara moja tu (kombe la sasa FIFA 1974)
5Kadi nyekundu wakati wa mashindano ya kombe la dunia
King PELE` hakuwahi kupewa kadi nyekundu wakati akicheza fainali ya kombe la dunia

Maradona alipewa kadi nyekundu mwaka 1982 fainali zaSpain
6Kucheza fainali (mcezo wa mwisho kombe uwanjani)
King PELE` amecheza fainali 2, 1958 ma 1970 na zote alinyakua ndoo

Maradona amecheza mala moja 1986 Mexico
7Magoli mechi za ushindaniMagoli zaidi ya 1000 King PELE`alifungaMaradona hata 600 hakufikisha
8Aina ya vionjo(style)PELE` ndiye mwanzilishi wa style zote: Tik-tak,byscle kick,scissor kick,scorpion kickMaradona style zote alizokuwa anacheza PELE` Maradona sijamwona akizicheza (wote nimewaona)
9KunyumbulikaKing PELE` alikuwa anatumia miguu yote kulia, kushoto, mpira uje kivyovyote: mbele, nyuma,mgongoni, mabegani uje tu
Maradona alikuwa anatumia mguu mmoja wa kushoto , alikuwa anautumia vizuri sana naomba kukili kwa hilo
10Kufunga magoliKing PELE` alikuwa anafunga kivyovyote: mashuti makali na laini, magoli ya kuplace, kichwa, faulo za kutenga, penati n.kMaradona uwezo huo alikuwa hana,goli la kichwa pekee ni lile la mkona alilowafunga Waingereza.


Kuna vigezo vingiiiii, naona nitawachosha tu, tatizo kuhusu wachazaji hawa nyie kizazi kipya mnaelezewa na akina Eddo Kumwembe ambao hawajui chochote wamewaona akina Rodadinno na akina Maradona tu PELE`hawajomwona zaidi ya kwenye vicrips crips, mimi nimemwona hasaaa uwanjani, na Maradona nimemwona hasaa uwanjani.

Sasa vionjo tu.
  • PELE`hakucheza Ulaya kwa sababu bunge la Brazil liliamua kuwa PELE` ni nyala ya taifa kwa hiyo hauzwi, hakuna mchezaji yoyote duniani aliyefanyiwa hivyo
  • PELE kule Columbia alipoenda na klabu chake cha Santos alifanyiwa rafu naye akalipiza kisasi, Refa akamtoa PELE` kwa kadi nyekundu, uwanja mzima ulipiga kelele PELE` akarudishwa uwanjani refa akatolewa nje, hakuna mchezaji yoyote aliyewahi kufanyiwa hivyo.
  • 1972 Club ya Dar-es Salaam Young African chini ya uongozi wa Mbwambo na Tabu Mangala waliandaa mradi wa kumwalika PELE` na klabu yake ya Santos waje Dar kucheza mchezo wa kirafiki, Walienda Brazil wakafikia makubaliano. Yanga wakajiandaa kabisa kupokea ugeni huo na wakatengeneza kabisa na kanga ziliandikwa “ PELE NA SANTOS WAGENI WA YANGA”. Sasa wakati ulipowadia Mke wa PELE` akajifungua ikabidi Klabu ya Santos ije peke yake bila PELE` Klabu ya Yanga ikafuta mradi huo,ikaona Santos kuja bila PELE` haina maana yoyote. Wakafutilia kwa mbali mwaliko huo ila kanga zipo wakina mama wengine wanazo mpaka leo wameweka ukumbusho.
Kwa hiyo jamani kizazi kipya mkome kabisa kumulinganisha PELE` na wachazaji wengine Maradona, Messi n.k , mnakosa nidhamu hata Edo Kumwembe niliwahi kumwambia kwa sababu kwa kigezo no 2 pekee hapo juu wakina Maradona na Messi wangevunjika vipande vipande na wangeacha kabisa kucheza mpira lakini PELE` alikuwa anacheza.
 
Vivyo hivyo hata hapa bongo Huwezi kumulinganosha Sunday Manala na mchezaji yoyote, Kuwalinganisha King PELE` na Maradona ni sawa eti umlinganishe Sunday Manala na Mbwana Samata semeni wenyewe.
 
Sawa Pele kanyanyua World Cup mara 3 nitajie katika mara tatu hizo ni wapi aliibuka mfungaji bora au hata mchezaji bora wa mashindano? Ukipata jibu nenda kapekue World Cup ya 1986 pale Mexico
 
Sawa Pele kanyanyua World Cup mara 3 nitajie katika mara tatu hizo ni wapi aliibuka mfungaji bora au hata mchezaji bora wa mashindano? Ukipata jibu nenda kapekue World Cup ya 1986 pale Mexico
Rekodi gani hiyo na wewe , hiyo ndiyo imufanye Maradona awe zaidi ya PELE`, Hiyo siwezi wala kwenda kuangalia, ila najua 1970 King PELE` ndiye alikuwa mchezaji bora wa mashindano hayo na kilichofuata kutokana na kukubalika kwake mashindano yaliyofuata huko Munich 1974 PELE` ndiye alikuwa mgeni wa heshima na alifyatua mpira kuashiria kuanza kwa mashindano , hakuna mchezaji yoyote aliyefanyiwa hivyo.
 
Sawa Pele kanyanyua World Cup mara 3 nitajie katika mara tatu hizo ni wapi aliibuka mfungaji bora au hata mchezaji bora wa mashindano? Ukipata jibu nenda kapekue World Cup ya 1986 pale Mexico
Unajua pele kacheza jumla ya michezo mingapi world cupu kafunga goli ngapi na kaasisti ngapi?
 
Humu nishaandika saana kuhusu pele, mpaka naona tabu kurudia rudia.. Kuna uzi humu siikumbuki vizuri, tulimjadili saana huyu kibabu
 
Pele ana ubora wake.
maradona ana ubora wake
messi ana ladha yake
Ronnaldo ana ladha yake
Lewandowski ana ladha yake..
nadhani uzi ufungwe.
 
Humu nishaandika saana kuhusu pele, mpaka naona tabu kurudia rudia.. Kuna uzi humu siikumbuki vizuri, tulimjadili saana huyu kibabu
Huna chochote cha kuniambia wewe, PELE` ulimwona wapi? mimi nilimwona Dakar Senegal mwaka 1965 alimipga chenga kipa mpaka akavua jezi akatupa mwisho wa mpira PELE` alienda kumpa mkono kipa yule alikataa mkono na kudai kwa nini alimwazili vile
 
Kumpata mchezaji Bora wa Karne iliyopita ilibidi FIFA waandae Kura toka kwa mashabiki wa soka kote duniani. Walishindanishwa Pele na Maradona. Kura zikahesabiwa na matokeo Diego Maradona akaibuka pale juu kabisa.

Kwa kuwa FIFA inamtumia Pele Kama chombo chake Cha propaganda wakadai pamoja na Diego kushinda tuzo hiyo lakini alikuwa ni mtovu wa nidhamu na ni MLA madawa ya kulevya. Hivyo wakalazimisha tuzo iende kwa wote wawili. Siku ya kutoa tuzo, inajua Diego alisema Nini? Sikwambii mtafute Gang Chomba atakwambia.

Ndani ya uwanja Pele kacheza na mabeki midebwedo. Alitakiwa akutane na mabeki wenye toho mbaya Kama Nigal de Jong, Frank Lebouf, n alike.
Pili hajacheza soka ulaya. Kwa kifupi Pele alikuwa mchezaji nzuri Kama walivyo kina Messi na cr7. Johonn cruffy na kina van Basten.
Mijadala Kama hii tushaichoka.
 
Kumpata mchezaji Bora wa Karne iliyopita ilibidi FIFA waandae Kura toka kwa mashabiki wa soka kote duniani. Walishindanishwa Pele na Maradona. Kura zikahesabiwa na matokeo Diego Maradona akaibuka pale juu kabisa.

Kwa kuwa FIFA inamtumia Pele Kama chombo chake Cha propaganda wakadai pamoja na Diego kushinda tuzo hiyo lakini alikuwa ni mtovu wa nidhamu na ni MLA madawa ya kulevya. Hivyo wakalazimisha tuzo iende kwa wote wawili. Siku ya kutoa tuzo, inajua Diego alisema Nini? Sikwambii mtafute Gang Chomba atakwambia.

Ndani ya uwanja Pele kacheza na mabeki midebwedo. Alitakiwa akutane na mabeki wenye toho mbaya Kama Nigal de Jong, Frank Lebouf, n alike.
Pili hajacheza soka ulaya. Kwa kifupi Pele alikuwa mchezaji nzuri Kama walivyo kina Messi na cr7. Johonn cruffy na kina van Basten.
Mijadala Kama hii tushaichoka.

Na kwa kumalizia, Pele alizungukwa na mafundi haswa, kazi ikawa rahisi kwake! Diego ilibidi aibebe timu makwapani kwake ili watwae ubingwa! Thats the difference
 
Rekodi gani hiyo na wewe , hiyo ndiyo imufanye Maradona awe zaidi ya PELE`, Hiyo siwezi wala kwenda kuangalia, ila najua 1970 King PELE` ndiye alikuwa mchezaji bora wa mashindano hayo na kilichofuata kutokana na kukubalika kwake mashindano yaliyofuata huko Munich 1974 PELE` ndiye alikuwa mgeni wa heshima na alifyatua mpira kuashiria kuanza kwa mashindano , hakuna mchezaji yoyote aliyefanyiwa hivyo.

Wana michezo hatueleweshani hivyo mkuu utasema tupo kwenye korido za lumumba? Cool down
 
huyo pele ulimuona akicheza??

usiniambie umemwona youtube?alafu sheria za mpira zinawabana sana wachezaji sasa,,kipindi hicho hakukua na sheria za offside kama sasa hivi yan enzi hizo wachezaji walikua wanajenga vibanda mpaka maghorofa

kipindi anacheza pele kulikua hakuna wachezaji wa maana ndo maana akawa anavua yeye tuu
 
alafu hayo magoli 1000 ya pele unayajua wewe,ukiingia google wikipedia ya pele utaona pele akiwa santos amecheza mechi 496 amefunga magoli 504 halafu New York Cosmos amecheza mechi 64 akafunga goli 37

timu ya taifa ya brazil amecheza mechi 92 goli 77

mleta mada naomba utuambie hizo goli 1000 kazifunga akiwa timu gani
 
Mtu mwenyewe alikuwa anafunga hata offside hazikuwepo unafunga tu
 
Back
Top Bottom