Hali halisi ya pato halisi (GDP) la Tanzania

Hali halisi ya pato halisi (GDP) la Tanzania

mahunduhamza

Member
Joined
Aug 25, 2021
Posts
19
Reaction score
46
Katika kipindi cha mwaka 2001-2010 pato halisi la Tanzania(GDP) limeonyesha kiwango cha wastani wa kukua cha 7%. Ukuaji ulishuka mwaka 2009 na kuwa 6.0%, hasa kutokana na kudorora sana kwa ukuaji wa uchumi duniani.

Hata hivyo ulirudia kwenye 7% mwaka 2010. Sekta zilizoonyesha viwango vya ukuaji vya zaidi ya 10% katika mwaka 2010 ni mawasiliano,(22.1%), ikifuatiwa na Ujenzi, Umeme na Gesi (10.2%) na Taasisi za Fedha(10.1%).

Mwaka 2010, Sekta zilizokuwa na mchango mkubwa kwenye ukuaji wa GDP ni Biashara na Matengenezo, Kilimo, Utengenezaji Bidhaa na Milki/Majengo na Huduma za Biashara.

Zaidi ya hayo, uchumi unategemea zaidi kilimo, ambacho ni zaidi ya robo ya GDP, kinatoa 85% ya mauzo ya nje, na kuajiri kiasi cha 75% ya wafanyakazi.
 
Back
Top Bottom