DOKEZO Hali ilivyo Shule ya Msingi Kamama (Tabora) inasikitisha, vyoo ni chakavu na vichafu, madarasa ndio usiseme

DOKEZO Hali ilivyo Shule ya Msingi Kamama (Tabora) inasikitisha, vyoo ni chakavu na vichafu, madarasa ndio usiseme

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
Juzi kati nilikuwa Tabora, Kata ya Goweko, Kijiji cha Kamama niliendea kumtembelea ndugu yangu wa karibu pande za Uyui mkoani hapo, kuna kitu ambacho nilikiona na nikajiambia hii sasa ni hatari.

Nimekuta Wanafunzi na shule nzima ya Msingi Kamama iliyopo Wilayani hapo ina changamoto nyingi ambazo kiukweli inasikitisha sana mzingira yaliyopo shuleni hapo.

Baadhi ya changamoto zinazowakabili Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kamama ni mazingira mabovu ya Vyoo na hata vilivyopo mazingira sio rafiki kabisa kabisa.
WhatsApp Image 2024-07-30 at 14.02.42_94fa6584.jpg

WhatsApp Image 2024-07-30 at 13.58.40_0e19a03d.jpg

WhatsApp Image 2024-07-30 at 14.02.26_d599236a.jpg
Shule hiyo ina jengo moja la vyoo ambalo lina matundu kati ya 6 au 8 na yote yakiwa katika hali isiyo faa kiafya, hata kimuonekano yana uchakavu mkubwa.

Hali hiyo inasababisha baadhi ya Wanafunzi kujisaidia porini kulingana na hali ilivyo, kitu kinachoumiza zaidi kuhusu mabinti pindi wanapo kuwa katika siku zao, wanapata wakati mgumu wakati wa kujistili hali hiyo wakiwa Shuleni.
WhatsApp Image 2024-07-30 at 14.02.36_5278ba9e.jpg

WhatsApp Image 2024-07-30 at 14.02.38_384b73d5.jpg

WhatsApp Image 2024-07-30 at 14.02.30_363289a0.jpg
Changamoto ya pili ni uhaba wa vyumba vya madarasa, mpaka sasa kuna baadhi ya Wanafumzi wanasomea kwenye madarasa yaliyojengewa miti na udogo.

Hali ya muonekano wa vyumba hivyo kiukweli sio wa wakati tulio nao, hali hizi zilikuwa kabla ya uhuru enzi za kukalia matofali ndio muonekano wa madarasa hayo.

Japokuwa madawati yapo ila vyumba hivyo sio rafiki kwa Mwanafunzi kupata elimu.

Kipindi cha kiangazi vumbi ni lao, masika mvua na tope ni jambo la kawaida kulingana na hali ilivyo.

Pia soma:
~
Baada ya picha za vyoo vya Shule ya Kamama (Uyui - Tabora) kuziweka hapa JF, nimeona wanajenga vyoo vipya

~ Miundombinu ya Shule ya Msingi Kamama yaboreshwa, Vyoo na madarasa vyajengwa
 
Juzi kati nilikuwa Tabora, niliendea kumtembelea ndugu yangu wa karibu pande za Uyui mkoani hapo, kuna kitu ambacho nilikiona na nikajiambia hii sasa ni hatari.

Nimekuta Wanafunzi na shule nzima ya Msingi Kamama iliyopo Wilayani hapo ina changamoto nyingi ambazo kiukweli inasikitisha sana mzingira yaliyopo shuleni hapo.

Baadhi ya changamoto zinazowakabili Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kamama ni mazingira mabovu ya Vyoo na hata vilivyopo mazingira sio rafiki kabisa kabisa.
Shule hiyo ina jengo moja la vyoo ambalo lina matundu kati ya 6 au 8 na yote yakiwa katika hali isiyo faa kiafya, hata kimuonekano yana uchakavu mkubwa.

Hali hiyo inasababisha baadhi ya Wanafunzi kujisaidia porini kulingana na hali ilivyo, kitu kinachoumiza zaidi kuhusu mabinti pindi wanapo kuwa katika siku zao, wanapata wakati mgumu wakati wa kujistili hali hiyo wakiwa Shuleni.
Changamoto ya pili ni uhaba wa vyumba vya madarasa, mpaka sasa kuna baadhi ya Wanafumzi wanasomea kwenye madarasa yaliyojengewa miti na udogo.

Hali ya muonekano wa vyumba hivyo kiukweli sio wa wakati tulio nao, hali hizi zilikuwa kabla ya uhuru enzi za kukalia matofali ndio muonekano wa madarasa hayo.

Japokuwa madawati yapo ila vyumba hivyo sio rafiki kwa Mwanafunzi kupata elimu.

Kipindi cha kiangazi vumbi ni lao, masika mvua na tope ni jambo la kawaida kulingana na hali ilivyo.
Hapa kuna kosa la serikali na kosa la uongozi wa shule na wazazi. Wameshindwa kupanda miti, ukoka na kuweka bustani? Au maji ndiyo shida? Hapa VX moja likiuzwa litakajenga shule nzuri kabisa. Samia mitano tena!
 
Mbona kina ChoiceVariable na Lucas Mwasha Mbwa kila siku wanademka kwamba mama yao chura kiziwi kaupiga mwingi?
 
Juzi kati nilikuwa Tabora, niliendea kumtembelea ndugu yangu wa karibu pande za Uyui mkoani hapo, kuna kitu ambacho nilikiona na nikajiambia hii sasa ni hatari.

Nimekuta Wanafunzi na shule nzima ya Msingi Kamama iliyopo Wilayani hapo ina changamoto nyingi ambazo kiukweli inasikitisha sana mzingira yaliyopo shuleni hapo.

Baadhi ya changamoto zinazowakabili Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kamama ni mazingira mabovu ya Vyoo na hata vilivyopo mazingira sio rafiki kabisa kabisa.
Shule hiyo ina jengo moja la vyoo ambalo lina matundu kati ya 6 au 8 na yote yakiwa katika hali isiyo faa kiafya, hata kimuonekano yana uchakavu mkubwa.

Hali hiyo inasababisha baadhi ya Wanafunzi kujisaidia porini kulingana na hali ilivyo, kitu kinachoumiza zaidi kuhusu mabinti pindi wanapo kuwa katika siku zao, wanapata wakati mgumu wakati wa kujistili hali hiyo wakiwa Shuleni.
Changamoto ya pili ni uhaba wa vyumba vya madarasa, mpaka sasa kuna baadhi ya Wanafumzi wanasomea kwenye madarasa yaliyojengewa miti na udogo.

Hali ya muonekano wa vyumba hivyo kiukweli sio wa wakati tulio nao, hali hizi zilikuwa kabla ya uhuru enzi za kukalia matofali ndio muonekano wa madarasa hayo.

Japokuwa madawati yapo ila vyumba hivyo sio rafiki kwa Mwanafunzi kupata elimu.

Kipindi cha kiangazi vumbi ni lao, masika mvua na tope ni jambo la kawaida kulingana na hali ilivyo.
Ama kweli shule ni maisha na maisha ni magumu.Halafu yupo anayetumia kodi zetu vabaya.
 
Ni aibu bendera ya Taifa inapepea kwnye eneo kama hilo,af ni taasisi inayotaka kuondoa ujinga... ni aibu aibu.
 
Shida sio Serikali wala CCM hapo, tatizo walimu wa wakuu pesa za kiendeshea shule zimekuwa kama za familia zao, Serikali inatoa fedha kila mwezi kiendeshea shule
 
Back
Top Bottom