Hali inatisha: Waliouliwa Uganda kwenye maandamano ni zaidi ya 60. M7 aondoke tu

Hali inatisha: Waliouliwa Uganda kwenye maandamano ni zaidi ya 60. M7 aondoke tu

kimsboy

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
9,846
Reaction score
20,319
Vyombo vya dola vya Uganda vyamuachia huru Bobi Wine; waliouawa katika ghasia wapindukia 60+SAUTI

Nov 20, 2020 14:27 UTC

PAKUA

Kiongozi wa chama cha upinzani cha National Unity Platform (NUP) ambaye pia na mgombea urais nchini Uganda, Robert Kyagulanyi, maarufu kwa jina la Bobi Wine ameachiwa huru kwa dhamana na mahakama moja ya nchi hiyo. Hii ni baada ya kushtadi maandamano ya ghasia yaliyopelekea makumi ya watu kuuawa kufuatia kukamatwa kwa mwanasiasa huyo chipukizi.

Wine alipandishwa kizimbani leo Ijumaa, na kushtakiwa kwa kosa la kukiuka sheria na taratibu zilizowekwa na Tume ya Uchaguzi Uganda (EC) kwa ajili ya kufanya kampeni wakati huu wa maambukizo ya virusi vya corona.

Bobi Wine alikamatwa juzi Jumatano na polisi ya nchi hiyo, kwa kosa la kujaza wafuasi zaidi ya 200 katika mkutano wake wa kampeni, kinyume na kanuni za Tume ya Uchaguzi.

Mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 38 amechiwa huru kwa dhamana na anatazamiwa kurejeshwa mahakamani Disemba 18 mwaka huu 2020.

Watu wasiopungua 68 wanaripotiwa kuuawa katika maandamano ya fujo yaliyoshuhudiwa katika mji mkuu Kampala tokea juzi baada ya kutiwa mbaroni Bobi Wine.

[https://media]Rais Museveni anayeiongoza Uganda tokea mwaka 1986

Waandamanaji walimiminika katika barabara na mitaa ya Kampala, baada ya polisi kumkamata mgombea huyo wa urais akiwa katika mkutano wa kampeni. Mbali na kuuawa, mamia ya waandamanaji wengine wamejeruhiwa huku wengine miongoni mwao wakitiwa mbaroni.

Wine ambaye kwa sasa ni mbunge wa Kyadondo anatazamiwa kuchuana vikali na Rais Yoweri Museveni (76) ambaye yuko madarakani tokea mwaka 1986, katika uchaguzi wa rais wa mapema mwaka ujao 2021.
Soma zaidi[emoji1313]

 
Kuna viongozi majuha sana Africa. Imagine watu zaidi ya 60 wamekufa kizembe kabisa bila sababu za msingi.

Hakukuwa na haja ya kumshikilia Bobi wine mpaka watu wafe ndio wamuachie. Siku za Mu7 zinahesabika sasa
 
EU imeumizwa zaidi na yaliyotokea Tz kuliko ya Uganda na ya wakati ule kwa Kagame

JPM for life

Ya Tanzania kwani yalikuwa madogo? Si busara za wahanga kuacha kuvutania mtoto tu?

Yetu ni haya hapa:


Mengine ni mbwembwe tu!
 
wapumzike kwa Amani ila n serikali ya Uganda iangalie upande w pili wa2 wanavo farik bila sababu y msingiii
 
Mapolisi wanafanana tabia zao wako radhi kuwauwa waafrika wenzao kulinda tumbo la mtawala ambae nae akipata madaraka awakumbuki kuboresha maisha yao. Ni sawa na mbwa alindae kwa bidii lakini ameachwa ajitegemee
 
Si kweli mkuu. Pamekuwa na matamko madhubiti kabisa dhidi ya Mseveni kama ilivyo kwa jiwe pia.
Kuna haja ya kufabya kazi maana haya matamko ni kama yameshindwa kufikia malengo
 
Vyombo vya dola vya Uganda vyamuachia huru Bobi Wine; waliouawa katika ghasia wapindukia 60+SAUTI

Nov 20, 2020 14:27 UTC

PAKUA

Kiongozi wa chama cha upinzani cha National Unity Platform (NUP) ambaye pia na mgombea urais nchini Uganda, Robert Kyagulanyi, maarufu kwa jina la Bobi Wine ameachiwa huru kwa dhamana na mahakama moja ya nchi hiyo. Hii ni baada ya kushtadi maandamano ya ghasia yaliyopelekea makumi ya watu kuuawa kufuatia kukamatwa kwa mwanasiasa huyo chipukizi.

Wine alipandishwa kizimbani leo Ijumaa, na kushtakiwa kwa kosa la kukiuka sheria na taratibu zilizowekwa na Tume ya Uchaguzi Uganda (EC) kwa ajili ya kufanya kampeni wakati huu wa maambukizo ya virusi vya corona.

Bobi Wine alikamatwa juzi Jumatano na polisi ya nchi hiyo, kwa kosa la kujaza wafuasi zaidi ya 200 katika mkutano wake wa kampeni, kinyume na kanuni za Tume ya Uchaguzi.

Mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 38 amechiwa huru kwa dhamana na anatazamiwa kurejeshwa mahakamani Disemba 18 mwaka huu 2020.

Watu wasiopungua 68 wanaripotiwa kuuawa katika maandamano ya fujo yaliyoshuhudiwa katika mji mkuu Kampala tokea juzi baada ya kutiwa mbaroni Bobi Wine.

[https://media]Rais Museveni anayeiongoza Uganda tokea mwaka 1986

Waandamanaji walimiminika katika barabara na mitaa ya Kampala, baada ya polisi kumkamata mgombea huyo wa urais akiwa katika mkutano wa kampeni. Mbali na kuuawa, mamia ya waandamanaji wengine wamejeruhiwa huku wengine miongoni mwao wakitiwa mbaroni.

Wine ambaye kwa sasa ni mbunge wa Kyadondo anatazamiwa kuchuana vikali na Rais Yoweri Museveni (76) ambaye yuko madarakani tokea mwaka 1986, katika uchaguzi wa rais wa mapema mwaka ujao 2021.
Soma zaidi[emoji1313]

badala ya kufa hata ukitetea dini yako,
kuna Mtu et yupo radhi afe ili wengine wale maisha
 
Kwa hali hii M7 ni kutupwa gereni moja kwa moja sielewi kwa nini baadhi ya viongozi wa bara la afrika wanakuwa namana hii pia naona ipo haja ya UN kuongezewa nguvu zaidi na kupewa jeshi kali sana litakalokuwa na kazi tu ya kuwanyofoa viongozi wa aina hii afrika maana naona ipo haja ya kustaarabishwa kinguvu na hakuna namna nyingine yoyote
 
Vyombo vya dola vya Uganda vyamuachia huru Bobi Wine; waliouawa katika ghasia wapindukia 60+SAUTI

Nov 20, 2020 14:27 UTC

PAKUA

Kiongozi wa chama cha upinzani cha National Unity Platform (NUP) ambaye pia na mgombea urais nchini Uganda, Robert Kyagulanyi, maarufu kwa jina la Bobi Wine ameachiwa huru kwa dhamana na mahakama moja ya nchi hiyo. Hii ni baada ya kushtadi maandamano ya ghasia yaliyopelekea makumi ya watu kuuawa kufuatia kukamatwa kwa mwanasiasa huyo chipukizi.

Wine alipandishwa kizimbani leo Ijumaa, na kushtakiwa kwa kosa la kukiuka sheria na taratibu zilizowekwa na Tume ya Uchaguzi Uganda (EC) kwa ajili ya kufanya kampeni wakati huu wa maambukizo ya virusi vya corona.

Bobi Wine alikamatwa juzi Jumatano na polisi ya nchi hiyo, kwa kosa la kujaza wafuasi zaidi ya 200 katika mkutano wake wa kampeni, kinyume na kanuni za Tume ya Uchaguzi.

Mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 38 amechiwa huru kwa dhamana na anatazamiwa kurejeshwa mahakamani Disemba 18 mwaka huu 2020.

Watu wasiopungua 68 wanaripotiwa kuuawa katika maandamano ya fujo yaliyoshuhudiwa katika mji mkuu Kampala tokea juzi baada ya kutiwa mbaroni Bobi Wine.

[https://media]Rais Museveni anayeiongoza Uganda tokea mwaka 1986

Waandamanaji walimiminika katika barabara na mitaa ya Kampala, baada ya polisi kumkamata mgombea huyo wa urais akiwa katika mkutano wa kampeni. Mbali na kuuawa, mamia ya waandamanaji wengine wamejeruhiwa huku wengine miongoni mwao wakitiwa mbaroni.

Wine ambaye kwa sasa ni mbunge wa Kyadondo anatazamiwa kuchuana vikali na Rais Yoweri Museveni (76) ambaye yuko madarakani tokea mwaka 1986, katika uchaguzi wa rais wa mapema mwaka ujao 2021.
Soma zaidi[emoji1313]

Ukileta upumbavu na ujinga utauawa tu. Tatizo vijana wa siku hizi mmejaa ujinga ujinga sana yaani. Mtaendelea kutangulizwa kufa na kutiwa vilema hadi mpukutike, wapumbavu nyinyi.
 
Back
Top Bottom