Elections 2010 Hali ngumu CCM nyanda za juu kusini

Acha watu wajue ukweli kwanza..............maamuzi baadaye watakapokubali kukataa pilau na pombe za kienyeji za ccm...
ni lazima maovu ya ccm yaanikwe ili watu wajue kuwa hakifai, ili wapate sababu ya kukiacha chama hiki kinachokumbatia mafisadi. Wananchi wana haki ya kujua uchafu wa ccm ili wafanye uchaguzi uliokwenda shule!
 
Sera za sisiem ni kutoa ahadi? kila anapopita huyu mkwere anasema nitawajengea daraja, mara ooh...nitajenga kituo cha afya.......hizo ndio sera za sisiem? THINK.........
 

labda sijaelewe
hivi hii habari ina uhusiano gani na nyanda za juu kusini?
 

Msingi mkuu wa kuanguka kwa taifa la TZ ni CCM kwa sababu zifuatazo:

1. Chama ambacho ndicho kinachoongoza nchi hakina political will kupambana na wizi wa mali ya uma. CCM yenyewe inaiba kutoka katika mapato ya nchi kwa ajili ya kufanikisha mambo yake ya uchaguzi niambie leo watapata wapi ubavu wa kuwazuia wananchi wengine.

2.CCM imechagua makada wake kuongoza taasisi nyeti nchini na kuzifanya zisiwe independent. Kwa mfano TAKUKURU, Tume ya Uchaguzi, n.k
Msingi mkuu wa hili ni kutokuwa na katiba inayo vifanya vyombo au taasisi hizi ziwe independent.

Na kwa kujua kuwa mfumo huu unawanufaisha wao hawana interest ya kubadilisha katiba, imagine hiyo haipo hata kwenye ilani yao ya uchaguzi.

Kwa hiyo si kweli kwamba matatizo yetu ni zaidi ya CCM bali matatizo yetu ni CCM na pale tutakapoamua kuwaondoa na kuwaweka watu ambao wameamua kubadili katiba mbovu hii tutaanza kuona mwanga wa tumaini jipya kwa nchi yetu.

Namalizia kwa kusema kuwa kwa mtazamo wangu CCM wanatumia mwamvuli wa chama kutuhadaa tu watanzania. Hiki ni kikundi cha MAFIA ambao ajenda yao kuu ni kushika dola ili waweze kujinufaisha wao na familia zao. Namna wanavyooperate ni kama a political party but it's actually not, ila bahati mbaya watz wengi hawalijui hili. Ni kundi la watu wezi ambao kwa kushirikiana na manyang'au wa nje wanaitafuna nchi kama mbwa mwitu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…