Sasa nimeelewa kwa nini tunaongoza kwa kuwa nchi ya watu wasio na furaha.
Kumbe imefikia
Kiranga huko nje ukitaka kumpa furaha ndugu yako kwa vidola kadhaa unakumbana na vikwazo kama unataka kusaidia magaidi?
Mbona nchi kama Nigeria au Kenya RAIA wake walio nje ni moja ya vyanzo vikuu vya kuingiza fedha za kigeni? Hizi sio dalili kuwa serikali hii ya CCM haipendi watu wake? Kwa nini isiwalegezee masharti ya kuleta fedha nyumbani na wanyumbani kufaidika na ndugu zao walio nje?
Sent using
Jamii Forums mobile app
Kuna jamaa mmoja alikuwa naibu waziri wa madini, alikwenda kwenye migodi ya madini huko kati, nafikiri ilikuwa Kahama.
Akawa anawalalamikia wawekezaji wa nje kwenye sekta ya madini, kwamba wanalipa Watanzania mishahara mikubwa sana. Wapunguze mishahara. Mishahara ile si sawa kwa levels za Watanzania.
Wakati ile kampuni hata hiyo mishahara iliyoonekana mikubwa, kwao ingejulikana ingeonekana scandal, kwamba wanawafanyisha watu kazi kwa kutumia mishahara midogo sana, wanatumia cheap labor.
Kuna kipindi serikali inapiga domo kuhusu kuleta maendeleo, kumaliza umasikini, wakati inajua kwamba haitaki kuleta maendeleo ya kweli, haitaki kumaliza umasikini.
Ikimaliza umasikini itakosa kazi. Umasikini ni mtaji wa serikali kuendelea kuwepo.
Serikali ikimaliza umasikini, watu watajua haki zao, watapata elimu, watai challenge, hawatakubali kuibiwa, serikali itaondolewa.
Hivyo, seruikali haipigi vita kuondoa umasikini, inapiga vita vita ya kuondoa umasikini.
Ndiyo maana unaona serikali inabana mzunguko wa fedha, tukija watu wa diaspora tunataka kusaidia, wakiona kuna watu wanatumiwa hela na ndugu zao walio nje, na sisi tunawekewa viunzi kibao tusitume hela.
Wajanja kibao, tunaenda kuchagua gubegube Magufuli liwe rais!
Tunajiwekea umasikini wenyewe kimfumo.