Chakaza, Sikuu ya Uhuru iliahirishwa kwa tangazo, Christmas inaweza kuahirishwa kwa mzunguko wa fedha.
Kuna muandishi mmoja alikuwa anaandika kuhusu Uganda siku za utawala wa Idi Amin.
Akasema alivyofika Uganda ya Idi Amin aliona nchi tofauti. Waganda kawaida ni wacheshi, watu wenye furaha, lakini Uganda ya Idi Amin ilikuwa tofauti, imejaa majonzi na woga.
Sasa hivi mzunguko wa fedha mgumu.
Sawa, ndugu zenu tulioondoka hapo tuko nje tukawa tunadunduliza na kutuma hela kusaidia. Ukimtumia mtu dola za Marekani mia moja au mbili muda huu wa sikukuu anaweza kufanya maarifa makubwa ajisikie na yeye anaishi.
Mara paap, Benki Kuu imekata nafasi za kutuma hela moja kwa moja MPesa.
Tumewekewa masharti mapya kutuma pesa mpaka uruke viunzi kibao, utume picha na ID card. Hata maelezo yenyewe hayako clear.
Ili mradi usumbufu tu, hata kwa mtu anayetaka kutoa msaada.
Tanzania kwa sasa unaweza kusema unataka kuleta matrekta ya bure kusaidia wakulima, serikali ikakudai kodi hapo hapo!
Sent using
Jamii Forums mobile app