Hali ninayokutana nayo katika Biashara inatisha nimefunga biashara 3 nimebakiza moja inayopumulia mipira, Msaada wa kiroho unahitajika

Hali ninayokutana nayo katika Biashara inatisha nimefunga biashara 3 nimebakiza moja inayopumulia mipira, Msaada wa kiroho unahitajika

Wewe kama unataka kupotea nenda kwa waganga! Ila suluhu yako ni kumtafuta Yesu nenda kanisani mpokee Yesu kuwa Bwana na mwokozi wako! Vyitu vyako vyote vitarudishwa! Wewe umerogwa na wachawi na hivyo vyitu vimechukuliwa kichawi mchawi babake yake ni shetani, alafu tena unaenda kwa mganga ambaye baba yake ni shetani! Kitakachofuata hapo ni kupewa masharti na hata kama biashara yako itarudi hutaifurahia lakini pia utakuwa umeyauza maishq yako kwa shetani, meaningi baada ya maisha haya ya duniani moto wa jehannum unakuhusu mpendwa! Maana duniani hakuna cha bure! Unawakataa walokole lakini hao ndio wenye njia ya kweli ya uzima wako mwili na roho( ninaposema walokole sio akina mwaposa, kuhani musa nk wanaotumia mafuta na vitambaa na maji) hao ni matapeli tafuta kanisa lolote la kiroho usiangalie wingi wa watu! Hata kama kanisa lina watu 10 ingia hapo onana na mchungaji atakufanyia maombi bure na biashara zako zitarudi acha kuangaika mpendwa!
 
Wewe kama unataka kupotea nenda kwa waganga! Ila suluhu yako ni kumtafuta Yesu nenda kanisani mpokee Yesu kuwa Bwana na mwokozi wako! Vyitu vyako vyote vitarudishwa! Wewe umerogwa na wachawi na hivyo vyitu vimechukuliwa kichawi mchawi babake yake ni shetani, alafu tena unaenda kwa mganga ambaye baba yake ni shetani! Kitakachofuata hapo ni kupewa masharti na hata kama biashara yako itarudi hutaifurahia lakini pia utakuwa umeyauza maishq yako kwa shetani, meaningi baada ya maisha haya ya duniani moto wa jehannum unakuhusu mpendwa! Maana duniani hakuna cha bure! Unawakataa walokole lakini hao ndio wenye njia ya kweli ya uzima wako mwili na roho( ninaposema walokole sio akina mwaposa, kuhani musa nk wanaotumia mafuta na vitambaa na maji) hao ni matapeli tafuta kanisa lolote la kiroho usiangalie wingi wa watu! Hata kama kanisa lina watu 10 ingia hapo onana na mchungaji atakufanyia maombi bure na biashara zako zitarudi acha kuangaika mpendwa!
Huko kanisani siku hizi ni pabaya zaidi. Akifika tu ataambiwa hatoagi fungu la kumi na kueletewa habari za michango ya kanisa. Hajakaa vizuri ataambiwa atoe sadaka ya ukombozi. Ninamshauri apigane kivyake amwombe Mungu kimyakimya.
 
PM umeipiga LOCK tutakujaje sasa mkuu?

mimi Juzi hapa nilipigwa nyungu ya mawe ilikuwa kidogo nikimbie uchi😂😂😂

yani huo mtungi ulichemka kabisa halafu nikafukizwa, jiwe la moto likadumbukizwa humo aisee ilikua bahati tu kuendelea kuwemo kwenye hio shuka😅😅😅😅View attachment 3092991
0765309523
namba ya huyo mtaalam ni hio
naona PM inajaa mafuriko
Yuko Nyamhongolo Jijini Mwanz
 
Habari Wakuu, Maelezo mengi yatawachosha.

Nilianza Biashara 2019, ya umachinga nikawa nachukua bidhaa mjini napeleka vijijini, Biashara ilikubali nilikuwa napiga profit nzuri sana kwa siku, Biashara yangu haikuwa na ushindani wala haikuwa ya kufikirisha kama kuna faida napata, Ila nilikuwa na uwezo wa kutengeneza faida ya Laki moja hadi 3 kwa siku,

Nikaendelea na Biashara hii kwa muda wa mwaka mmoja nikaamua kununua kiwanja na kujenga nyumba yangu wa kwanza ya kuanzia maisha, nikahamia, nikaendelea kukomaa nikajenga nyumba ya pili ya ndoto zangu...

Kwa bahati nzuri location niliyojenga kwa mbele kuna barabara nikaona sio mbaya nikajiongeze nikajenga Viflemu vya biashara nikapata na wapangaji nikaanza kupokea vikodi. Kiukweli nilianza kuona natimiza ndoto kimasihara sana.

Mwaka juzi nikapambana nikapata kigari nikanunua na baadae nikawaza biashara ya Umachinga sio Biashara ya kudumu, Hivyo nikaona nijiwekeze nikaona ni bora nifungue vitega uchumi vingine ili nitanue biashara..

Nikaamua kufungua Duka la kwanza katika moja ya flem zangu, Mwanzoni biashara ilienda vzuri hadi nikawa najiuliza nilikuwa nachelewa nini.

Baadae nikaona shemeji yenu nae anafaa apate biashara yake ili asinitegemee na yeye nikatafuta location nikamfungulia Cafe ya kuuza misosi napo biashara ikatiki nikaongeza kipato zaidi nikazidi kuinjoy..

Nikaona niongeze ofisi ya tatu, Nikafungua Duka la spea za pikipiki eneo baada ya kuona location inafaa, Biashara zikazidi kupamba moto.

Cha ajabu na cha kushangaza ni ndani ya muda mfupi biashara zote zimesimama hakuna mteja anakuja dukani kwangu, watu wanapita tu na kwenda kununua bidhaa kwingine, cha kusikitisha ni kwamba upepo umenata ofisi zote, Pale kwa wife vyakula vinapikwa vinatupwa, Dukani panya wanashambulia vitu bila huruma, na hakuna mteja, Duka la spea hakuna wateja na mafundi wamehama sina fundi wala bidhaa haziuziki.

Nimeamua kufunga biashara zote maana naona ni hasara tupu, Kwanza nilianza na Mgahawa wa wife, likafuata Duka na hivi juzi nimemalizia kufunga Duka la spea.

Nimeamua kurudia biashara yangu ya awali ya Umachinga ambayo ndio ilinipa msingi.. cha ajabu nayo saizi wateja wangu wanataka kunikopa tu hamna la maana. Natoka nazunguka narudi nyumbani na pesa ya kula tu hamna cha maana.

Cha ajabu hata usiku nikilala naota ndoto za kutisha kama nipo kwetu kijijini, tena saa zingine naota nipo shule ya msingi nasoma na mara zingine naota nimepakazwa kinyesi mwili mzima. Jamani wakuu tusaidiane hapa najinasua vipi.

Kwa upande wangu napendelea kujinasua katika hiki kifungo kupitia wataalam wa jadi ndipo imani yangu inanituma japo sijui ni wapi nitaanzia wala ni wapi nitaishia.

Siwiwi na walokole kuponya tatzo langu, kama yupo ambae alishawahi kukutwa na janga kama hili na akachomoka na kurudi katika hali yake ya kawaida anisaidie Pm Iko wazi jamani. Ndugu tusaidianane, Napitia fedheha kubwa sana, Nimejaribu kushirikisha akili yangu ila imefika ukomo.

Napewa namba za wataalamu wengi ila ukimpigia katika maongezi pyschologically nawastukia ni wapigaji wengi wao wanajisifia ila ukipima maongezi yake unaona kama hayana uhalisia.. Na mwisho wanataka kutumiwa pesa ili wanisaidie.
Unasema hauamini katika masuala ya dini lakini nakusisitiza hakika yanasaidia bila masharti yoyote yale


Muhimu ni kuwa kama ulipata mali kwa halali bila dhulma wala kumuibia mtu zitabaki


Kwenda kwa waganga unajitengenezea mazingira ambayo yatazidi kukuongezea vifungo visivyo na mwisho ni bora uokoke wewe na familia yako

Mrudieni Mungu kisha kwa imani moja salini sana hakika Mwangaza mtauona
 
Piga nyungu kamanda ukirudi mpya kila mtu ana kuchangamkia 😄
Mkuu inanibidi tu hamna namna
kinachonikuta kwenye kutafuta maokoto ni kitu kibaua sana

nisipochangamka ntafilisika.

nikifeli hapa naenda katoro

Bahati nzuri hizi connection napewa na ndugu ambao wameshapita huko
 
Mkuu inanibidi tu hamna namna
kinachonikuta kwenye kutafuta maokoto ni kitu kibaua sana

nisipochangamka ntafilisika.

nikifeli hapa naenda katoro

Bahati nzuri hizi connection napewa na ndugu ambao wameshapita huko
Jamaa uhakika sio 😄
 
Piga nyungu kamanda ukirudi mpya kila mtu ana kuchangamkia 😄
Baada ya kutoka huko Mtu wa kwanza kugombana nae ni jirani yangu...😅😅

Jirani kumbe ana chuma ulete ya kimya kimya kubabake..
nikiacha vihela ndani anadokoa bila mimi kuona
FB_IMG_1726036935638.jpg
 
Wewe hujalogwa wala nini. Tatizo lako ni kama la watanzania wengine la kushangilia ushindi kabla mechi hajaisha. Mwaka 2019 hadi leo ni miaka 5. Kosa lako ni kufanya mambo mengi bila kuacha biashara iwe imara kwanza. Kujenga nyumba kadhaa, frems na kununua gari kisha kugawanyisha mtaji na kufungua biashara tatu ni kosa baya. Mbaya zaidi ukaiacha biashara iliyokuletea mafanikio. Wewe umejivuruga mwenyewe. ACHA KUKURUPUKA PIA PUNGUZA TAMAA. Tatizo lako halihitaji mganga wala mchungaji. Tuliza akili anza upya.
Umemaliza kila kitu,...nina uzoefu na biashara, licha ya kuwa kuna changamoto zingine hazieleki kikawaida, lakini msingi wa tatizo upo kama ulivyonena
 
Cha ajabu na cha kushangaza ni ndani ya muda mfupi biashara zote zimesimama hakuna mteja anakuja dukani kwangu, watu wanapita tu na kwenda kununua bidhaa kwingine, cha kusikitisha ni kwamba upepo umenata ofisi zote, Pale kwa wife vyakula vinapikwa vinatupwa, Dukani panya wanashambulia vitu bila huruma, na hakuna mteja, Duka la spea hakuna wateja na mafundi wamehama sina fundi wala bidhaa haziuziki.
Unahitaji suluhisho la kiroho Ili kutatua hilo, amini hili.

Angalia kulingana na Imani yako ya kidini kipi unaweza kufanya, ila huwa unakumbuka kutoa Sadaka kwa faida unazopata kwenye biashara zako?
 
Cha ajabu hata usiku nikilala naota ndoto za kutisha kama nipo kwetu kijijini, tena saa zingine naota nipo shule ya msingi nasoma na mara zingine naota nimepakazwa kinyesi mwili mzima. Jamani wakuu tusaidiane hapa najinasua vipi.

Kwa upande wangu napendelea kujinasua katika hiki kifungo kupitia wataalam wa jadi ndipo imani yangu inanituma japo sijui ni wapi nitaanzia wala ni wapi nitaishia.
Pole sana, unachokiota ndio sahihi ulichotendewa na wanga.....
 
Nakupa Connection ya pili.

Save hii namba: 0759953006
huyu anaitwa Mzee Bahati.
ni mzee wa makamo tu under 60

Location: Katoro

Gharama yake: 100,000/= minimum

anapiga ramli kwa kuchinja kuku

(hapa unaweza nunua kuku hadi wanne, maana akishatibu lazima achinje tena kuangalia kama mambo yamekaa sawa)

Connection nilipewa na ndugu yangu ambaye ni mfanyabiashara wa mazao, pia huenda kuchukua dawa za Kulimia/kupata mazao mengi/kulinda shamba.
 
Nakupa Connection ya pili.

Save hii namba: 0759953006
huyu anaitwa Mzee Bahati.
ni mzee wa makamo tu under 60

Location: Katoro

Gharama yake: 100,000/= minimum

anapiga ramli kwa kuchinja kuku

(hapa unaweza nunua kuku hadi wanne, maana akishatibu lazima achinje tena kuangalia kama mambo yamekaa sawa)

Connection nilipewa na ndugu yangu ambaye ni mfanyabiashara wa mazao, pia huenda kuchukua dawa za Kulimia/kupata mazao mengi/kulinda shamba.
Ha ha ha dawa za kulimia kupata mazao mengi? Huyo ni bwana shamba au mganga?
 
Back
Top Bottom