Kuna mpasuko mkubwa uliopo ndani ya simba hivi sasa. Kuna bomu kubwa sana linakuja kulipuka muda sio mrefu. Hiyo yote ni kwa ajili ya Boss kuuza wachezaji wawili na mpunga bado haujasomeka katika account ya klabu.
Wapo viongozi wenye hofu na wasiwasi kubwa sana juu ya biashara ya usajili ya msimu huu. Pia ndani humo humo wapo viongozi wanapingana mazima na uendeshaji wa klabu.
Ikumbukwe kuwa tangu Mo atangaze kuwa ameweka mpunga wa Bilioni 10, Akaunti ya klabu bado inasoma zero balance.
MASWALI MATANO MUHIMU KWA WANASIMBA WENZANGU
Wadau poleni Sana maana naona mmeamua kujiumiza mioyo..
1. Hivi kwann tunapenda kucheza Muziki wa Utopolo??
2. Hivi mnadhani sisi mashabiki tulio mitandaoni tuna uchungu saaana na Timu kuliko kamati ya Usajiri, bodi ya Wakurugenzi, Mangungu au Mo mwenyewe??
3. Hivi ndugu zangu nyie, siku analetwa Chama, Bwalya, Onyango, Mugalu mlikuwa mnawajua??? Au ndio mlihusika kusema waletwe??
4. Hivi Mnajua madhara ya kumkatalia mchezaji kwenda kwenye ofa nono aliyoipata??
5. Nani aliyewaambia bila Chama na Luis Simba haiwezi??
Aliondoka Okwi, Kotei na Kocha Bora kabisa Pierre Lechantre.. Leo mnalalama kwa Hawa??
Mliwahi kumuona Samatta akiwa Simba?? Aliondoka yeye na Patrick Ochan..
Binafsi nawaza saana Kama ningekuwa Mo pocbly ningechukua maamuz magumu saana kwa niyasomayo mitandaoni..
Hakuna kitu Utopolo watafurahia Kama siku Mo akichoshwa na kelele za wanafiki wachache wa Simba wasio Italia mema Simba.
Nawaza Sana kuwa tunashangilia Lakini hatufatilii masuala ya Soka Duniani..
Mnafahamu kuwa David Becham aliondoka Man U akiwa Mtamu??
Mliwahi kufuatilia Siku CR 7 Anavyoondoka Man U??
Ameondoka Meci pale Barca, mnitajie Ni Nani Kama Meci hapo Simba.
Okwi, Kaseja waliondoka Tena kwenda kwa mahasimu wetu..
Lkn Simba ilikuwepo na ikaimarika zaidi..
Simba tumebahatika mno kupata watu wa Soka ktk uongozi lkn tumekuwa hatuwaheshimu...
Hawa Jamaa kina Magori na Hans Poppe wanajua mno....
Eti sisi vile tu tuna bando tunajiona TUNAJUA.
Mliwahi sikia juu ya mbinu wakizozifanya mpaka Luis akasaini kwetu???
Tuna kila Aina ya mchezaji lkn hatuoni Hilo..
Nawaambieni tu Chikwende, Kagere, HD, Miraji, Ajibu na Ndemla hawakuwa na namba ya uhakika Simba, lkn Hawa woteee wangekuwa Utopolo au Azam Hakuna wa kuwaweka Benchi..na wangekuwa fest Eleven wa kudumu kule...
Wenzetu UTOPOLO wanajua kuwatukuza na kuwashukuru mno Viongozi wao...
Wanaletewa Wachezaji wa Kawaida na wa viwango vya chini lkn wanawatia Moyo Wachezaji wao mpaka wanaonekana wakubwa..
Sisi tumekalia majungu, Uzushi na kumsimanga Tajiri wetu..
Gadem shiiit....
Mo nae Ana Moyo, nae Ni binadamu..
IPO Siku atachoka ndio tutajuta..
Mo Yule mbali ya Utajiri wake lkn Ni shabiki mwenzetu Tena lialia..
Tumepata Dancun Monster Nyoni mchezaji wa Kiwango Cha juu mno, tunae MTU kutoka Mali na huko Senegal Ni watu haswa lkn tupo na msononeko tu.
Tukumbuke sisi Mchango wetu Mkubwa ktk timu Ni HAMASA, tujifunze kuheshimu Viongozi, naamini ktk wakati huu wa Vita vya usajiri Viongozi hawalali wanatutengeneza kilicho Bora zaidi. Lkn sisi badala ya kuwapa Kongole tumebaki tu. Tunalalama...
Sijui tupoje???
Tuwe na Imani, tuwaunge Mkono walau kwa kukumbuka mema na ubunifu wao ktk majukumu yao.
Naomba saana ukipata wasaa unijibu hayo maswali matano sio lazima kwa Sauti au kwa kuandika, hata kimoyo Moyo tu itatosha.
Simba kwanza, MTU baadae!!
Wasaalaamu!!!