Hali ya kujiajiri itakuwaje kwa Sheria za Mitandao zilizopo?

Hali ya kujiajiri itakuwaje kwa Sheria za Mitandao zilizopo?

OLS

JF-Expert Member
Joined
Oct 12, 2019
Posts
426
Reaction score
685
Mmoja kati ya wachumi duniani anasema tupo katika Enzi ya Taarifa ‘Information age’ (O’Connor, 2005) kwa kiasi kikubwa huyu bwana ameonyesha namna ambayo taarifa zinavywaajiri watu. Katika hilo amezungumzia zaidi technolojia na mapinduzi yake tangu mwaka 1946 ilipoanza ENIAC Kwa kiasi kikubwa amezungumzia masuala ya ICT

Ni kwa namna hiyo hiyo (Goodman, 2015) ameelezea namna ambavyo makampuni ya teknolojia na taarifa yanakuwa ni makampuni ya bilions.

Japo anaheshimu uchumi wa viwanda lakini wasomi wameshaona kwa sasa taarifa ndio kitu kinachotengeneza pesa zaidi, thus mitandao kama Facebook nk inatengeneza billions of money, na Apps zikinunulika kwa hela nyingi japo yenyewe inatumiwa bure na watumiaji wake, wanapataje hela? Ni swala la taarifa

Kwa waafrika ambao mchango wetu kwenye tecknolojia ni mdogo hatuko nyuma kwenye kutengeneza pesa kupitia taarifa na maarifa, mfano watu wenye Page za instagram zenye followers wengi wamekuwa wakijipatia pesa kwa kupewa matangazo na baadhi ya watu na wao wakaweza kusukuma siku

Ama kwa hakika dunia ilionyesha mwanga wa kujiajiri kwa vijana ambao wamekuwa wakifundishana kwa makundi ya whatsapp kwa ujira kidogo wa kupata elimu mbalimbali za kutengeneza vitu mbali mbali au techniques za maisha

Hapo hatujazungumzia waliokuwa wanapata hela kidogo kwa kuwa na blogs au youtube channels ambazo zingeweza kuja online Tv na vijana kujipatia ajira nk. Kifupi ni kuwa, Hii zama za taarifa zimekuwa ni chanzo cha ajira kwa waliowengi katika nchi zinazoendelea

Sheria ya mtandao ya mwaka 2018 ilisababisha majanga kwa baadhi ya watu na watu wakajitune kivingine, lakini pia kwa sheria ya makosa ya mtandao ya mwaka 2020 imezidi kuwa mwiba kwa kuwazuia vijana hao kuweza kujiajiri bila gharama kupitia mitandao ambayo inawaruhusu kushare taarifa.

Kwa sheria mpya ni kwamba hata mtu mwenye kundi la whatsapp aliyekuwa anafundisha kutengeneza vipodozi, atashindwa kuendelea kufanya hivyo hadi awe na kibali maalumu. Sijui sheria inalenga nini lakini kwa kiasi kikubwa sheria hizi zimeathiri uwezo wa vijana kujiajiri kwa kuwa mambo yaliyokuwa yanawafanya wajiajiri kwa sasa imekuwa jinai.

NB: Najua kuna mashauri ya kiuchumi yanafanyika kwa serikali mimi niwakumbushe tu kuwa tafiti zinaonyesha kuwa ukizidisha kodi, au ukitaka mapato mengi, mapato hupungua kwa kuwa watu huziepuka kodi zaidi wakiona zinazidi kuwabana (Montiel, 2008).

Sasa kwa kuwa watu wataepuka kodi hizo na kupunguza mapato ya serikali, tutazidi kuwapeleka watu jela au kuendelea kufanya majadiliano na DPP ili kulipa fedha ambazo haziko mikononi mwa watu. Kwa mwendo huo basi aidha shughuli haramu ziongezeke, au unemployment iongezeke kwa kasi.

Matokeo ya ugumu kiuchumi yana impact mbaya kisiasa, sheria huwa haifanyi kazi raia wanapoona wamechoka.

Haya ni maneno yangu kwa serikali yangu tukufu ili waweze kujua kuwa vijana hawataweza kujiajiri kama sheria inawabana kwa kiasi kikubwa namna hii, na ikiwa ajira zilizopo haizendani na idadi ya watu waliopo.

Ninayo mengi ila kwa leo niishie hapo.


Signed

OEDIPUS


References
Goodman, M. (2015). Future Crimes. New York: Doubleday.

Montiel, P.-R. A. (2008). Development Macroeconomics. Princeton: Princeton University Press.

O’Connor, D. E. (2005). The Basics of Economics. London: GREENWOOD PRESS.
 
Hivi unaweza kuzuia website au YouTube channel isionekane bongo kabisa?
Inawezekana, though hawatafanya hivyo..ila kwa watakao tumia kuna uwezekano mkubwa wa kushitakiwa kwa kesi za jinai
 
Umesema jambo la msingi sana lakini nasikitika kusema kua wakati wenzetu nchi za wenye akili wanaangaisha vichwa kurahisisha maisha ya watu wao kwakubuni nakuvumbua teknolojia mbalimbali kama hizo za mawasiliano ya internet sisi uku nchi hizi za dunia ya 3 kazi yetu nikuwekeana vikwazo na sheria mbalimbali zisizotusaidia asilani.

Akili yetu inawazaga kufanya mambo yawe magumu badala ya kuyarahisisha.Kwahiyo usitegemee mabadiliko yoyote kwenye hilo zaidi ya vijana wengi wenye uthubutu kuingia matatani.
 
Huwa nasema kila siku,hawa wabunge tunaowapa dhamana kuingia bungeni na kutunga sheria za kumsaidia mtanzania lakini mwisho wa siku wanaishia kupiga tu makofi na kusifia kila kitu na kuunga mkono kila muswada unaopelekwa bungeni,HAPA NDO TATIZO LINAPOANZIA!,

Huu ni mwanzo tu bado kuna sheria mbovu zitakuja za kumkandamiza mtanzania,tusubiri tuone
 
Kwas asilimia mia moja viongozi, wanasiasa na watu wa zamani (1975s down) hawataki kuona maendeleo, hawataki kuona vijana wakifanikiwa, hawataki umaskini ibaki historia. Wanachuki kubwa sana dhidi ya watu wenye uelewa na wenye potential ya kufanikiwa au kutatua masuala mbalimbali.
 
Wakikutaka hawakosi sababu. Hi nchi Ni ya kise.nge sana
hapo labda uingie kwenye anga zao ,au ukiwa famous
lakini kama ukikomaa na audience ya kwa mabeberu huko halafu unaplay low key mmbona fresh
nataka nijaribu hii
 
Umesema jambo la msingi sana lakini nasikitika kusema kua wakati wenzetu nchi za wenye akili wanaangaisha vichwa kurahisisha maisha ya watu wao kwakubuni nakuvumbua teknolojia mbalimbali kama hizo za mawasiliano ya internet sisi uku nchi hizi za dunia ya 3 kazi yetu nikuwekeana vikwazo na sheria mbalimbali zisizotusaidia asilani.

Akili yetu inawazaga kufanya mambo yawe magumu badala ya kuyarahisisha.Kwahiyo usitegemee mabadiliko yoyote kwenye hilo zaidi ya vijana wengi wenye uthubutu kuingia matatani.
Umeongea vizuri sana mno.....
sisi wenyewe ndio wachawi wa maendeleo yetu..
kupitia masheria yanayozuia ubunifu.....
 
hapo labda uingie kwenye anga zao ,au ukiwa famous
lakini kama ukikomaa na audience ya kwa mabeberu huko halafu unaplay low key mmbona fresh
nataka nijaribu hii
Kwanini tufanye mambo halali kwa kujifichaficha katika nchi huru ?
 
Kwanini tufanye mambo halali kwa kujifichaficha katika nchi huru ?
lishatokea hilo ,lipi bora kufanya kwa kujificha au kufanya kwa uwazi lakini ukumbane na mkono wa sheria
 
lishatokea hilo ,lipi bora kufanya kwa kujificha au kufanya kwa uwazi lakini ukumbane na mkono wa sheria
Vijana tunauwezo wa kuilinda kesho yetu badala ya kuruhusu bunge liendelee kututungia sheria za hovyo zinaua kesho yetu ni heri kwenda kuufunga ukumbi wa bunge.

Vijana wa Burkinafaso waliweza hili kwanini sisi tushindwe ???
 
Back
Top Bottom