Hali ya Uchumi na kupanda kwa bei, Waziri Kijaji asema Bei za bidhaa za ndani ni himilivu. Waziri Mwigulu aahidi kupunguza bei mafuta ya kula na gari

Hali ya Uchumi na kupanda kwa bei, Waziri Kijaji asema Bei za bidhaa za ndani ni himilivu. Waziri Mwigulu aahidi kupunguza bei mafuta ya kula na gari

"Ukuaji wa uchumi kwa Tanzania ulishuka kutoka 7% hadi 4.8% na sasa uchumi umepanda hadi 4.9% huku nchi nyingine uchumi wake ulishuka hadi kufikia hasi, siwezi kuzitaja wka sababu za kidiplomasia
Akili hakuna kabisa, anajiuma na kujipulizia mwenyewe, anajisifia kushuka toka 7 hadi 4.8 na kupanda kwa 0.1
 
Bongo bahati mbaya.
Hii nchi raisi alikuwa Ni MAGUFULI na Nyerere tuu wengine wote ni vibaraka tuu.
 
Mama Samia Suluhu Hassan,atapotoshwa na Waheshimiwa mawaziri.
-Dr Kijaji anatoa takwimu za mahitaji ya bidhaa kwa mwaka ukilinganisha na uzalishaji wa ndani,na kuonyesha deficit.
Lakini haji na mikakati ya muda mfupi,muda wa Kati na muda mrefu kumaliza changamoto hiyo
-Dr Kijaji ana lalamika tu, kuhusu wafanya Biashara kupandisha bei ya bidhaa,bila kusema FCC wanafanya nini kuzuia changamoto hiyo.wakati anazo Mamlaka za udhibiti
-Dr Mwigulu anahimiza Wananchi waendelee na kazi iwe covid-19 au vita ya Russia na Ukraine, suala la kujiuliza ni kama watanzania waliacha uzalishaji kutokana na Covid-19 au vita ya Russia?

Ushauri
1)Waheshimiwa mawazi walipaswa kueleza mipango ya Serikali ya muda wa mfupi,muda wa Kati na muda mrefu.
-Kwa mfano :
-kwa kipindi Cha muda mfupi Serikali itapunguza matumizi yasiyo ya lazima na fedha zitakazopatikana kutoa ruzuku kwa waagiza wa mafuta,au
-Serikali kuhamisha fedha kutoka kwenye mfuko Mkuu (Consolidated Fund) na kutoa ruzuku kwa waagizaji wa mafuta.
2). Serikali kuanzisha block farming na kutoa mikopo kwa vijana, security iwe vyeti vyao
3). Serikali kutafuta wawekezaji kwenye sekta ya gasi,kupanua viwanda vya Mbolea nondo na saruji ili kuondoa deficit
4). Serikali kupunguza VAT na Levy inayotozwa kwenye petrol
5) Serikali kukabidhi mashamba makubwa ya Busutu kwa wawekezaji binafsi au kununua Combine harvestor kukodisha kwa vijana wahitimu wetu wa SUA na vyuo vikuu vingine,ambao watawekwa kwenye CAMPs ili kuleta uzalishaji mkubwa
6) Serikali kutafuta masoko ya mazao
7).Kuanzisha viwanda vidogo vidogo au vya kati kwa ajili ya kuchakata mazao na Wabia
 
Shida Hii Ndiyo Eti Wataalam Na Wajuzi
Ccm Tunayohubiriwa Inaisimamia Serikali Imejaa Tele Kama Chatu Aliyemeza Kitu Kizito
 
Aibu naona mimi kwa ajili ya hawa mawaziri wawili. Naona leo wameamua kutudhihirishia ya kuwa tuna mawaziri VILAZA ambao hawana msaada kwa Watanzania.



Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Chama cha kijana kimeitia unajisi hii nchi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Hapo wanasubiri posho ziingie mifukoni mwao kwa hoja hizo?Sababu nyepesi kwa masuala mazito yanayohusisha maisha ya wananchi wa kawaida wa kipato cha chini.
Hapo ni Dr's wamegundua sababu za bei kuruka?

Huyu Waziri anaposema bei za bidhaa za ndani ni himilivu ana maana gani? Wananchi wanalalamika kwasababu hawazimudu hizo bei kutokana na kipato chao; sasa anatUmía kipimo gani anaposema bei ni himilivu? Bei hizo zingekuwa himilivu wananchi wasingelalamika? Ili bei za hizo bidhaa zilizopanda wananchi waweze kuzimudu aidha mishahara/ mapato yao yaongezeke au mishahara/ mipato yao visiongezeka lakini bei ya hizo bidhaa zipungue!! VINGINEVYO SERIKALI ITAKUWA HAIJAWASAIDIA WANANCHI DHIDI YA MFUMUKO HUU WA BEI!
 
Hawa wapumbavu kwanini hawajapunguza kodi na kuweka bei elekezi kwa bidhaa muhimu kisha waje kutusomea namba tu?
Badala yake wanakuja kutuambia kuwa watapunguza, ni nani anahitaji maneno ?
 
Rais Samia ameagiza timu ya wavhumi wa wizara ya fedha kuangalia namna ya kupunguza kodi kwenye sukari, mbolea, mafuta ya kula na nishati.

Hayo yamesemwa na waziri wa fedha Dr Mwigulu Nchemba

Dkt. Mwigulu Nchemba amesema kwa kuanzia sukari itakayoingia hivi karibuni itapunguziwa kodi kwa zaidi ya 10%.

Chanzo: ITV habari
 
Samia asiishie hapo tu, awakataze watoto wake kufanya starehe za kutumia chopper wakati wananchi wanaumia!! Hiyo Asali wanayolamba mwisho wataharisha bure!!! Serikali haina budi kubana matumizi yake nchi inaelekea kubaya 'THE RECESSION IS IN THE OFFING"
 
Samia asiishie hapo tu, awakataze watoto wake kufanya starehe za kutumia chopper wakati wananchi wanaumia!! Hiyo Asali wanayolamba mwisho wataharisha bure!!! Serikali haina budi kubana matumizi yake nchi inaelekea kubaya 'THE RECESSION IS IN THE OFFING"
Serikali imekusikia!
 
Rais Samia ameagiza timu ya wavhumi wa wizara ya fedha kuangalia namna ya kupunguza kodi kwenye sukari, mbolea, mafuta ya kula na nishati.

Hayo yamesemwa na waziri wa fedha Dr Mwigullu Nchemba

Dr Mwigullu Nchemba amesema kwa kuanzia sukari itakayoingia hivi karibuni itapunguziwa kodi kwa zaidi ya 10%.

Source: ITV habari
Sasa tunajua kwanini ilikuwa nongwa kwa January kupunguza tozo
 
Siyo tena kushusha bei mara moja bila ya kujalisha nguvu ya demand na supply?🐒🐒🐒
AI4SIT.jpeg
 
Back
Top Bottom