Hali ya umeme yawa ya matumaini baada ya juhudi za Serikali pamoja na mvua kuanza kunyesha maeneo mbalimbali nchini

Hali ya umeme yawa ya matumaini baada ya juhudi za Serikali pamoja na mvua kuanza kunyesha maeneo mbalimbali nchini

Mvua isiponyesha ni matatizo ya ukame
ila ikinyesha ni juhudi za serikali
 
Katika miradi yote inavyotekelezwa na serikali yetu hakuna mtu yeyote atakayebakia salama ikiwa itabainika kuwa kafuja fedha za umma
Lile daraja la 7b kibiti linafanana na thamani ya fedha? Hatua gani zinachukuliwa?

Mmeishia kuwatumbua waliokuwa watumishi katika serikali ya magufuli ili muweke watu wenu waendeleze upigaji.

Kuna uozo mkubwa sana kwenye miradi ya serikali. Hakuna hatua zinazochukuliwa. Unatuambia nini?
 
Mvua isiponyesha ni matatizo ya ukame
ila ikinyesha ni juhudi za serikali
Juhudi za Serikali zimeonekana kipindi chote Cha ukame kilichotokea hapa nchini,Kama siyo juhudi za serikali hali ingekuwa mbaya zaidi kwa jinsi ukame ilivyokuwa mkubwa mwaka huu
 
Lile daraja la 7b kibiti linafanana na thamani ya fedha? Hatua gani zinachukuliwa?

Mmeishia kuwatumbua waliokuwa watumishi katika serikali ya magufuli ili muweke watu wenu waendeleze upigaji.

Kuna uozo mkubwa sana kwenye miradi ya serikali. Hakuna hatua zinazochukuliwa. Unatuambia nini?
Hakuna Atakaye pona ikiwa atabainika kugusa pesa za umma.Tuwe na Imani na serikali yetu
 
Hakuna Atakaye pona ikiwa atabainika kugusa pesa za umma.Tuwe na Imani na serikali yetu
Nimeelewa wewe ni nani.
Lakini iko siku mtakufa tu kama ambavyo watanzania tunakufa kwa stress za ugumu wa maisha na kukosa huduma katika taasisi za serikali.

Shule za serikali elimu imeporonoka mbaya. Ukienda private ada zimepaa mbaya mwaka huu.

Maji ni shida na umeme sisemi.

Mko kwenye kiyoyozi mnasema eti kila kitu kiko sawa.
 
Ndugu zangu kwa Sasa Hali ya umeme inarejea katika Hali yake ya kawaida,kwa Sasa shughuli za kiuchumi zinazotegemea umeme zinakwenda vyema, Mioyo ya wananchi wajasiriamali na wafanyabiashara imeanza kuwa
na Tabasamu na matumaini ya kufanya kazi muda wote,Taa ya Matumaini inawaka mioyoni mwa watu Sasa, Giza linazidi kusogezwa mbali,mitaa inazidi kuwa na mwanga na kuchangamka muda wote, sauti za manung'uniko ya umeme zinapungua na Kuisha.

Sasa Ni pongezi kwa serikali ya mh Rais Wetu mpendwa Dr Samia kwa juhudi zake kubwa za kukabiliana na tatizo hili pamoja Na shukurani kwa Mwenyezi Mungu kwa kutushushia Neema Na Baraka za Mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mengi, ambapo hata hapa napoandika mvua kubwa inaendelea kunyesha huku niliko mkoani kwangu. Hakika serikali yetu imepambana,imejitahidi kwa nguvu zake zote, kwa nyenzo zote katika wakati wote ambao tulikuwa tunapitia katika kipindi Cha ukame wa mvua kulikopelekea kupungua kwa kina Cha maji katika mabwawa yetu ya kuzalisha umeme.

Hongera kwetu watanzania kwa mioyo yetu ya Subira uvumilivu na usikivu kwa serikali yetu kwa kipindi chote Cha changamoto hii ya umeme,kwa namna ambavyo tuliungana na kuielewa serikali yetu juu ya chanzo Cha changamoto hiyo ya umeme iliyokuwa imetokana na ukame mkubwa uliokuwa umeikumba nchi yetu.

Hata hivyo Inawezekana Kuna maeneo kukawa na kukatika kwa muda mfupi kwa umeme Jambo ambalo naamini haiwezi ikawa Kama awali,hivyo Tuwe wenye Subira na uvumilivu Kama awali huku tukiendelea kuiamini serikali yetu, maana Tumeona namna inavyo pambana pamoja na juhudi zake katika katika kukabiliana na changamoto ya aina yoyote inayojitokeza mbele yetu Kama Taifa.

Watanzania Hatuna budi Kuendelea kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa upendo wake kwetu watanzania kwa kutupatia Baraka na Neema ya mvua katika kipindi hiki, zitakazo saidia kumaliza changamoto hii ya umeme,Hakika Mwenyezi Mungu anatupenda Sana watanzania, Tuendelee kumwomba Mwenyezi Mungu aendelee kulilinda Taifa letu na Wala Tusikubali mtu yeyote akatugawa kwa misingi ya udini,ukabila au ukanda. Tuwe wamoja na Tumuunge mkono Rais wetu mpendwa Dr Mama Samia Suluhu Hassan na serikali yake katika kututumikia watanzania.

Kazi iendeleee,mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu: 0742-676627
Nani kakutuma wewe. Umeona hali imetengemaa au umetumwa? Kipindi hiki kuacha kuumia shughuli zetu hata kombe la dunia watu wameshindwa kufustilia kwa uzuri
 
Nimeelewa wewe ni nani.
Lakini iko siku mtakufa tu kama ambavyo watanzania tunakufa kwa stress za ugumu wa maisha na kukosa huduma katika taasisi za serikali.

Shule za serikali elimu imeporonoka mbaya. Ukienda private ada zimepaa mbaya mwaka huu.

Maji ni shida na umeme sisemi.

Mko kwenye kiyoyozi mnasema eti kila kitu kiko sawa.
Mimi Ni mkulima na nimeona juhudi za serikali katika kutukwamua kiuchumi watanzania,Tumeona namna serikali ilivyojengwa miradi mimgi inayogusa maisha yetu,Tumeona namna uliyoleta mapinduzi makubwa katika secta karibu zote,mfano katika Afya Tumeona namna vituo vya Afya vilivyojengwa nchini kwote mfano majuzi hapa kumejengwa vituo vya Afya 234 ,lakini pia madarasa zaidi ya elfu nane nchini yamejengwa.

Ukienda katika kilimo nako Ni mapinduzi makubwa ambapo bajeti tu imeongezeka na kufikia billioni Mia Tisa na point na kutolewa kwa Ruzuku ya mabillioni ya pesa karibu billion Mia moja hamsini na kupelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni mfano mbolea ya DAP msimu uliopita ilikuwa inauzwa shillingi laki moja na 40 lakini msimu huu inapatikana kwa Elfu 70 tu
 
Nani kakutuma wewe. Umeona hali imetengemaa au umetumwa? Kipindi hiki kuacha kuumia shughuli zetu hata kombe la dunia watu wameshindwa kufustilia kwa uzuri
Inawezekana ulikoko lakini niliko Hali imekuwa njema Sana katika suala Zima la umeme
 
Mimi Ni mkulima na nimeona juhudi za serikali katika kutukwamua kiuchumi watanzania,Tumeona namna serikali ilivyojengwa miradi mimgi inayogusa maisha yetu,Tumeona namna uliyoleta mapinduzi makubwa katika secta karibu zote,mfano katika Afya Tumeona namna vituo vya Afya vilivyojengwa nchini kwote mfano majuzi hapa kumejengwa vituo vya Afya 234 ,lakini pia madarasa zaidi ya elfu nane nchini yamejengwa.

Ukienda katika kilimo nako Ni mapinduzi makubwa ambapo bajeti tu imeongezeka na kufikia billioni Mia Tisa na point na kutolewa kwa Ruzuku ya mabillioni ya pesa karibu billion Mia moja hamsini na kupelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni mfano mbolea ya DAP msimu uliopita ilikuwa inauzwa shillingi laki moja na 40 lakini msimu huu inapatikana kwa Elfu 70 tu
Umeshiba keki ya taifa. Andika tu baba. Andika hadi usinzie kwa raha zako.
 
Mimi Ni mkulima na nimeona juhudi za serikali katika kutukwamua kiuchumi watanzania,Tumeona namna serikali ilivyojengwa miradi mimgi inayogusa maisha yetu,Tumeona namna uliyoleta mapinduzi makubwa katika secta karibu zote,mfano katika Afya Tumeona namna vituo vya Afya vilivyojengwa nchini kwote mfano majuzi hapa kumejengwa vituo vya Afya 234 ,lakini pia madarasa zaidi ya elfu nane nchini yamejengwa.

Ukienda katika kilimo nako Ni mapinduzi makubwa ambapo bajeti tu imeongezeka na kufikia billioni Mia Tisa na point na kutolewa kwa Ruzuku ya mabillioni ya pesa karibu billion Mia moja hamsini na kupelekea kushuka kwa Bei ya mbolea sokoni mfano mbolea ya DAP msimu uliopita ilikuwa inauzwa shillingi laki moja na 40 lakini msimu huu inapatikana kwa Elfu 70 tu
DAP sh 70, 000 wapi?

Hivi mmetuona watanzania hatunazo kiasi hicho?

Kama kweli mmeshusha bei ya mbolea basi ondoeni kodi kwenye miamala na umeme.

Yaani tunanunua mbolea kwa bei ileile halafu mnasema imepungua bei.
 
Mimi nipo Mkoa wa Songwe wilaya moja wapo ambapo nakuhakikishia kuwa umeme katika wiki lots haujasumbua hata kidogo hata napoandika umeme upo
Mkoa wa Songwe Wilaya ipi umeme sio wa mgao labda Ileje maana sijafika huko lakini hapa Tunduma hapa sio mgao ni kero maana umeme unakatika hovyo hovyo Kyela,Rujewa, Chunya,Ubaruku kote mgao mkali
Labda upo Saza kwenye migodi huko sijui hali ikoje lakini Mikoa ninayotembelea kote nakutana na mgao mkali

Tena ningependa kukwambia huko Mkoa wa Songwe,Rukwa,Katavi huko mvua zinanyesha vizuri lakini Mkoa wa Iringa na Dodoma mvua bado ya kusuasua

Kwa hiyo mpaka sasa akuna sehemu yoyote yenye unafuu wa mgao kote kuna mgao mkali wala asikudanganye mtu ndugu yangu
 
Tukiwa na vichwa kama vyako maendeleo yatabaki kuwa ndoto
Uko kwako ndio unaona uo umeme au ngoma
Mbona suala la umeme tulikwisha sahau ila limerudi Tena? Tena kwa kasi ya ajabu? Unasifia Nini tatizo wanaleta wanajidai kutatua?
Tuwe serious na maisha asee
 
Mkoa wa Songwe Wilaya ipi umeme sio wa mgao labda Ileje maana sijafika huko lakini hapa Tunduma hapa sio mgao ni kero maana umeme unakatika hovyo hovyo Kyela,Rujewa, Chunya,Ubaruku kote mgao mkali
Labda upo Saza kwenye migodi huko sijui hali ikoje lakini Mikoa ninayotembelea kote nakutana na mgao mkali

Tena ningependa kukwambia huko Mkoa wa Songwe,Rukwa,Katavi huko mvua zinanyesha vizuri lakini Mkoa wa Iringa na Dodoma mvua bado ya kusuasua

Kwa hiyo mpaka sasa akuna sehemu yoyote yenye unafuu wa mgao kote kuna mgao mkali wala asikudanganye mtu ndugu yangu
Nakukaribisha Mbozi ambako hata muda huu umeme upo na wiki lote hili umeme haujasumbua,niambie Ni sehemu gani kwa Sasa ndani ya wilaya ya Mbozi ambako umeme u asumbua iwe Ni Rwanda mahenje mlowo Vwawa au hata ihanda.
 
Tukiwa na vichwa kama vyako maendeleo yatabaki kuwa ndoto
Uko kwako ndio unaona uo umeme au ngoma
Mbona suala la umeme tulikwisha sahau ila limerudi Tena? Tena kwa kasi ya ajabu? Unasifia Nini tatizo wanaleta wanajidai kutatua?
Tuwe serious na maisha asee
Tatizo la umeme halikuletwa na mtu maana sote ni.mashahidi wa namna mwaka huu ukame ulivyo kuwa nchini kwetu
 
DAP sh 70, 000 wapi?

Hivi mmetuona watanzania hatunazo kiasi hicho?

Kama kweli mmeshusha bei ya mbolea basi ondoeni kodi kwenye miamala na umeme.

Yaani tunanunua mbolea kwa bei ileile halafu mnasema imepungua bei.
Mbolea zote za Ruzuku kwa mbolea aina ya DAP no shilingi elfu 70 katika maduka yote yenye kuuza mbolea za Ruzuku ukienda na sms yako ambayo uliletewa baada ya zoezi lile la awali la usajili unapewa mbolea bila shida
 
Mbolea zote za Ruzuku kwa mbolea aina ya DAP no shilingi elfu 70 katika maduka yote yenye kuuza mbolea za Ruzuku ukienda na sms yako ambayo uliletewa baada ya zoezi lile la awali la usajili unapewa mbolea bila shida
Hiyo ruzuku umetoa wewe au ni kodi yangu?
 
Hiyo ruzuku umetoa wewe au ni kodi yangu?
Sasa hapa tunabishana Nini mkuu? Wewe si ulikuwa unapinga kuwa mbolea ya DAP ya Ruzuku haiuzwi kwa elfu 70? Mimi nimekupa utaratibu ambao wakulima tulikuwa tunaufuata kuipata mbolea hiyo na nimegundua wewe hata kilimo huelewi kikoje na mambo yapoje katika secta hii,ndio maana unakuwa mbishi bila sababu ilimradi tu uonekane umepinga
 
Back
Top Bottom