✓Migogoro ya kifamilia
✓Ukosefu wa pesa
Ndivyo vilivyonipelekea kuwa na msongo mzito wa mawazo kufikia hatua ya kutaka niwe kipeke yangu tu! Hivi sasa nimeshazoea, sihitaji kuwa na marafiki wazungumzaji sana, sehemu yenye makelele ya muziki, kujichanganya na watu hata kuwa kwenye mahusiano sioni umuhimu!
Napenda kuwa peke yangu tu! Unawaza kila muda kuwa hata kama utakuwa kwenye mahusiano, huyo binti utampa nini? Hapo hisia zote zinakata unabaki kuangalia jinsi ambavyo nguvu zako za kiume zinamwagika chini bila huruma!
Kuwa karibu na marafiki unaona ni aina fulani ya unafiki, wenzako wakiwa bar wanaagiza, mwenzangu na mie unaona hata aibu kuongozana nao, utaagiza nini!!?
Inaanza kama mawazo, depression ya nguvu, lakini mwisho wa siku unajikuta unaishi ishi tu ili mradi siku zisogee ufe tu!!