Halima Mdee: Tusifikirie kimasikini, ndege binafsi sio anasa

Halima Mdee: Tusifikirie kimasikini, ndege binafsi sio anasa

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
1656332511311.png

Mbunge wa Viti Maalum, Halima Mdee ameshauri Serikali kupunguza kodi katika ndege zinazotumika kwa utalii Nchini akisema inatakiwa kushuka na ikiwezekena ifike hatua kumiliki ndege binafsi liwe jambo la kawaida.

“Kamati imesema ndege za kukodi zimepungua kutoka 200 hadi 105, ifike kipindi Waziri Mwigulu (Nchemba), kumiliki ndege sio anasa, tuache kufikiria kimasikini, tushindanisha watu waruke hewani,” anasema Mdee akiwa Bungeni Jijini Dodoma, leo Juni 27, 2022.

Aidha, Mbunge mwingine Hamis Kigwangwalla aliongezea kwa kusema Tanzania inatajwa kuwa ni sehemu yenye gharama kubwa kufanya utalii, hivyo Serikali ishushe gharama za kupunguza kodi ikiwemo gharama za ndege kutua Nchini.
 
Mbunge wa Viti Maalum, Halima Mdee ameshauri Serikali kupunguza kodi katika ndege zinazotumika kwa utalii Nchini akisema inatakiwa kushuka na ikiwezekena ifike hatua kumiliki ndege binafsi liwe jambo la kawaida.

“Kamati imesema ndege za kukodi zimepungua kutoka 200 hadi 105, ifike kipindi Waziri Mwigulu (Nchemba), kumiliki ndege sio anasa, tuache kufikiria kimasikini, tushindanisha watu waruke hewani,” anasema Mdee akiwa Bungeni Jijini Dodoma, leo Juni 27, 2022.

Aidha, Mbunge mwingine Hamis Kigwangwalla aliongezea kwa kusema Tanzania inatajwa kuwa ni sehemu yenye gharama kubwa kufanya utalii, hivyo Serikali ishushe gharama za kupunguza kodi ikiwemo gharama za ndege kutua Nchini.
Michango yote inayo tolewa na Covid Bungeni ninharamu kama walivyo wao.
Na haistahili kuingia kwenye kumbukumbu za bunge.
 
Kigwangala akili imerudi baada ya kukosa uwaziri alishindwa nini kushauri kodi ipunguzwe akiwa waziri
 
Huo uwezo wa watanzania kumiliki ndege binafsi uko wapi?

Kama huo uwezo ungekuwepo, Mdee asingesema hicho alichosema.
 
Serikali yetu ni makini sana kwenye kuongeza bila kufikiri kuwa kupunguza bei/gharama vile vile ni kivutio kwa wengi.Mfano,kama kuingia hifadhini kama ni USD 50 kwa mgeni na ukawapata 100 kila siku lakini ukiwalipisha USD 25 unaweza kuwapata 500.

Hapo unakuwa umepata mzunguko wa watu zaidi na faida lazima iongezeke.Hata Machinga wanafanya hivyo,Sasa unajiuliza hivi Waziri mwenye PhD ya uchumi hafahamu multiplayer effect katika biashara?
 
Serikali yetu ni makini sana kwenye kuongeza bila kufikiri kuwa kupunguza bei/gharama vile vile ni kivutio kwa wengi.Mfano,kama kuingia hifadhini kama ni USD 50 kwa mgeni na ukawapata 100 kila siku lakini ukiwalipisha USD 25 unaweza kuwapata 500.

Hapo unakuwa umepata mzunguko wa watu zaidi na faida lazima iongezeke.Hata Machinga wanafanya hivyo,Sasa unajiuliza hivi Waziri mwenye PhD ya uchumi hafahamu multiplayer effect katika biashara?

Umepatia mkuu!! Yaani inaonekana kabisa sisi ndio kikwazo cha utalii. Hatujui ushindani maana yake ni kupunguza gharama kwa mtalii mtarajiwa. Vivutio tulivyonavyo sio vya kipeke kihiiiiivo!!

Usafiri ndege aghaaali kuja Tz. Mtalii akifanya total cost anakuta ni bora aende kwingine akapate kinacholingana na pesa zake!! Sisi ni kama tunataka watalii matajiri - aliwahi kusema kiongozi mmoja mkubwa.
 
Back
Top Bottom