Halmashauri ya Bukombe walipeni watumishi madeni yao ili tupate matokeo chanya

Halmashauri ya Bukombe walipeni watumishi madeni yao ili tupate matokeo chanya

Johnson Alex Otieno

Senior Member
Joined
Mar 14, 2013
Posts
172
Reaction score
57
Salaam wana jukwaa,

Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa uzima na afya njema, pia niwashukuru watumishi wote nchini Tanzania kwa kuendelea kujenga Taifa letu bila kujali kadhia mnazokumbana nazo toka kwa wakuu wenu wa vitengo na wengine wengi waliopewa mamlaka ya kusimamia maslahi na haki zenu.

Nijikite kwenye mada, Kwa wa sio fahamu Bukombe ni moja ya wilaya za Mkoa wa Geita.

Ndani ya halmashauri ya Bukombe kuna mambo mengi yanayokatisha tamaa na shauku ya watumishi kufanya kazi kwa bidii na kutumia talanta/vipaji vyako kikamilifu.
Mambo hayo ni kama yafutayo:

1). Kucheleweshwa kwa malipo ya uhamisho na wakati mwingine kutokulipwa kabisa.

Imekuwa ni kawaida kwa watumishi wa kada ya elimu(walimu) kuhamishwa bila kufata taratibu na kanuni za kazi.
Mfano mwezi Machi shule nyingi mpya zimefunguliwa na walimu walihamishwa toka eneo moja la kazi na kupelekwa km nyingi bila kukamilisha malipo yao.

Jambo hili limeathiri utendaji wao, kwa ni huko walikopelekwa hakuna nyumba za watumishi hivyo watumishi hawa walazimika kusafiri umbali mrefu ili kutimiza takwa la kazi.

Naomba wakuu walipeni watumishi fedha za uhamisho mapema ili wapate unafuu wa maisha na wakidhi gharama za nauli, mathalani mwalimu mmoja hutumia elfu tano kwa siku ili kufika kituo cha kazi, wengine huendesha baiskeli kwa zaidi ya km 36 kwa siku kwenda kituo chake cha kazi kwa kazi.

Ifike wakati jibu la mchakato unaendelea lisitamkwe.
Wapeni fedha ili wafanye kazi, uhamisho sio adhabu.

2) Fedha za kujikimu kwa watumishi wapya/ajira mpya.

Imekuwa ni kawaida kwa halmashauri ya bukombe kuchelewesha fedha za kujikimu kwa watumishi wapya, hali hii imefanya watumishi wengi washindwe kufanya kazi kwa ufanisi na kufikia lengo.

Mara nyingi halmashauri inasubiri watumishi wafike ofisi ya mkurugenzi kumsumbua kwa kushinikiza malipo yao, nje ya utaratibu wa kushinikiza malipo yao, majibu huwa mchakato unaendelea na kuambiwa barua zimekosewa.

Kuna maelekezo mengine, punguzeni michakato tafadhari. Lipeni watumishi madai yao kwa wakati, watumishi hawa ni binadamu, wana mahitaji na wana familia zinawategemea.

Ijumaa kareem
 
Salaam wana jukwaa,

Awali ya yote napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa uzima na afya njema, pia niwashukuru watumishi wote nchini Tanzania kwa kuendelea kujenga Taifa letu bila kujali kadhia mnazokumbana nazo toka kwa wakuu wenu wa vitengo na wengine wengi waliopewa mamlaka ya kusimamia maslahi na haki zenu.

Nijikite kwenye mada, Kwa wa sio fahamu Bukombe ni moja ya wilaya za Mkoa wa Geita.

Ndani ya halmashauri ya Bukombe kuna mambo mengi yanayokatisha tamaa na shauku ya watumishi kufanya kazi kwa bidii na kutumia talanta/vipaji vyako kikamilifu.
Mambo hayo ni kama yafutayo:

1). Kucheleweshwa kwa malipo ya uhamisho na wakati mwingine kutokulipwa kabisa.

Imekuwa ni kawaida kwa watumishi wa kada ya elimu(walimu) kuhamishwa bila kufata taratibu na kanuni za kazi.
Mfano mwezi Machi shule nyingi mpya zimefunguliwa na walimu walihamishwa toka eneo moja la kazi na kupelekwa km nyingi bila kukamilisha malipo yao.

Jambo hili limeathiri utendaji wao, kwa ni huko walikopelekwa hakuna nyumba za watumishi hivyo watumishi hawa walazimika kusafiri umbali mrefu ili kutimiza takwa la kazi.

Naomba wakuu walipeni watumishi fedha za uhamisho mapema ili wapate unafuu wa maisha na wakidhi gharama za nauli, mathalani mwalimu mmoja hutumia elfu tano kwa siku ili kufika kituo cha kazi, wengine huendesha baiskeli kwa zaidi ya km 36 kwa siku kwenda kituo chake cha kazi kwa kazi.

Ifike wakati jibu la mchakato unaendelea lisitamkwe.
Wapeni fedha ili wafanye kazi, uhamisho sio adhabu.

2) Fedha za kujikimu kwa watumishi wapya/ajira mpya.

Imekuwa ni kawaida kwa halmashauri ya bukombe kuchelewesha fedha za kujikimu kwa watumishi wapya, hali hii imefanya watumishi wengi washindwe kufanya kazi kwa ufanisi na kufikia lengo.

Mara nyingi halmashauri inasubiri watumishi wafike ofisi ya mkurugenzi kumsumbua kwa kushinikiza malipo yao, nje ya utaratibu wa kushinikiza malipo yao, majibu huwa mchakato unaendelea na kuambiwa barua zimekosewa.

Kuna maelekezo mengine, punguzeni michakato tafadhari. Lipeni watumishi madai yao kwa wakati, watumishi hawa ni binadamu, wana mahitaji na wana familia zinawategemea.

Ijumaa kareem
Poleni
 
Hilo tatizo ni la nchi nzima watumishi kibao hawalipwi arrears zao kwa zaidi ya miaka 5 mfano huku wilaya ya sumbawanga watu mpaka wamekata tamaa
 
huwezi amini hapo hapo bukombe watu waliopanda madaraja 2019 mis hahara yao ya miezi kadhaa hawajalipwa,wanalipwa kimafungu,unakuta unafanya nae kazi kituo kimoja ,mmepanda mwezi mmoja,yeye analipwa ww unaachwa,hiyo ndio bukombe ya waziri doto biteko,hata CWT yenywewe haina meno,
•mbaya zaidi umehamishwa bila malipo tena umbali mkubwa ikiacha kwenda au ukichelewa unagongwa barua ya kujieleza na mkuu wa shule,
 
Teach as you earn, mwanao peleka padre pio runzewe.

Do passive reaction hadi umma utambue mwl sio tatzo bali gavoo.
 
Kuna mtumishi alienda kujiendeleza alimaliza chuo Leo mwaka wa 9.kabla ya kwenda chuo alipanda Daraja 2013 mara ya mwisho Kichekesho tangu amalize chuo ofisi ya utumishi wamekuwa wakimpa barua za Categorization bila promotion Kwa kipindi chote hicho cha miaka 9, anazo barua 4 za categorization
 
Back
Top Bottom