Jackbauer
JF-Expert Member
- Oct 28, 2010
- 6,053
- 2,207
Halmashauri ya jiji la Arusha chini ya mkurugenzi mpya imeamua kuichukua timu ya AFC ambayo kwa sasa iko ligi daraja la pili.Manispaa ya jiji imeamua kuichukua timu hiyo iliyokuwa ikiwakilisha Arusha katika ramani ya michezo au mpira wa miguu kwa miaka mingi kabla ya kufulia.
Inasemekana hili ni wazo la mkurugenzi mpya wa jiji ambaye ana historia ya kuiibua timu ya Mbeya city alipokuwa mkurugenzi wa manispaa ya mbeya.
kwa sasa AFC itajulikana kama ACFC ...ARUSHA CITY FOOTBAL CLUB!
Kila la kheri mkurugenzi.
=====================
=====================
Mkurugenzi wa jiji la Arusha, Juma Iddi (mwenye suti nyeusi).
Mkurugenzi wa jiji la Arusha, Juma Iddi amepania kuipandisha ligi timu ya Arusha FC inayoshiriki ligi daraja la pili msimu huu, huku akiwataka viongozi wa sasa wa timu hiyo kuwa kama kamati na jiji hilo kuhakikisha swala hilo linafanikiwa.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mapema ofisini kwake alisema kuwa kwa kuwa tayari usajili umekwisha fanyika kwa sasa wanatafuta kocha mwenye ujuzi na uwezo wa kimataifa wa kuwanoa vijana hao ili kuweza kumudu mikiki ya ligi daraja la pili bila kuwa na woga.
"Kiukweli mimi napenda michezo na niko hapa halmashauri ambapo kazi kubwa ni pamoja na kuitangaza michezo na kuonyesha mfano hivyo kwa kuanzia tumeipa nguvu ya kushiriki michuano hiyo kwa vifaa vyote walivyohitaji vya michezo lengo wasianze kulalama na vifaa".
"Na baada ya vifaa sasa tutahakikisha inakuwa mikononi mwetu mapema mwezi ujao baraza la madiwani litakapokaa na kuridhia na baadhi ya watendaji wa halmashauri hii watakuwa miongozi mwa viongozi watakaochaguliwa kuiongoza lengo ni kuileta karibu na kujua mahitaji yao" alisema Juma Iddi.
Alitumia fursa hiyo kuwataka wananchi wa Arusha kuhakikisha wanakuwa karibu zaidi na timu hiyo na ilete chachu ya soka mkoani hapa kwa kuishangilia na mawazo pia maoni yao.
"Sisi kama halmashauri kuimiliki timu hii siyo kuwaweka mbali wananchi bali ni kuweza kuwajulisha kuwa pia kuwa timu hiyo ni yao kwani itakuwa inatangaza jiji pia kodi zao ndio zitatumika na wajue kuwa pia hatutachukua moja kwa moja bali kwa mda ili tu kuipandisha"
Alitumia fursa hiyo kuwataka mashabiki wa soka wa mkoani hapa pamoja na benchi la ufundi na wachezaji kuwa kitu kimoja na wasiruhusu migogoro kati yao kwani kufanya hivyo kutakatisha matumaini ya kupanda ligi bali wawe kitu kimoja kuhakikisha lengo linafanikiwa.
DewjiBlog
Inasemekana hili ni wazo la mkurugenzi mpya wa jiji ambaye ana historia ya kuiibua timu ya Mbeya city alipokuwa mkurugenzi wa manispaa ya mbeya.
kwa sasa AFC itajulikana kama ACFC ...ARUSHA CITY FOOTBAL CLUB!
Kila la kheri mkurugenzi.
=====================
=====================
Mkurugenzi wa jiji la Arusha, Juma Iddi (mwenye suti nyeusi).
Mkurugenzi wa jiji la Arusha, Juma Iddi amepania kuipandisha ligi timu ya Arusha FC inayoshiriki ligi daraja la pili msimu huu, huku akiwataka viongozi wa sasa wa timu hiyo kuwa kama kamati na jiji hilo kuhakikisha swala hilo linafanikiwa.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mapema ofisini kwake alisema kuwa kwa kuwa tayari usajili umekwisha fanyika kwa sasa wanatafuta kocha mwenye ujuzi na uwezo wa kimataifa wa kuwanoa vijana hao ili kuweza kumudu mikiki ya ligi daraja la pili bila kuwa na woga.
"Kiukweli mimi napenda michezo na niko hapa halmashauri ambapo kazi kubwa ni pamoja na kuitangaza michezo na kuonyesha mfano hivyo kwa kuanzia tumeipa nguvu ya kushiriki michuano hiyo kwa vifaa vyote walivyohitaji vya michezo lengo wasianze kulalama na vifaa".
"Na baada ya vifaa sasa tutahakikisha inakuwa mikononi mwetu mapema mwezi ujao baraza la madiwani litakapokaa na kuridhia na baadhi ya watendaji wa halmashauri hii watakuwa miongozi mwa viongozi watakaochaguliwa kuiongoza lengo ni kuileta karibu na kujua mahitaji yao" alisema Juma Iddi.
Alitumia fursa hiyo kuwataka wananchi wa Arusha kuhakikisha wanakuwa karibu zaidi na timu hiyo na ilete chachu ya soka mkoani hapa kwa kuishangilia na mawazo pia maoni yao.
"Sisi kama halmashauri kuimiliki timu hii siyo kuwaweka mbali wananchi bali ni kuweza kuwajulisha kuwa pia kuwa timu hiyo ni yao kwani itakuwa inatangaza jiji pia kodi zao ndio zitatumika na wajue kuwa pia hatutachukua moja kwa moja bali kwa mda ili tu kuipandisha"
Alitumia fursa hiyo kuwataka mashabiki wa soka wa mkoani hapa pamoja na benchi la ufundi na wachezaji kuwa kitu kimoja na wasiruhusu migogoro kati yao kwani kufanya hivyo kutakatisha matumaini ya kupanda ligi bali wawe kitu kimoja kuhakikisha lengo linafanikiwa.
DewjiBlog