Halmashauri ya Mji Kibaha sasa imepanda hadhi na kuwa Manispaa

Halmashauri ya Mji Kibaha sasa imepanda hadhi na kuwa Manispaa

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia Halmashauri ya Mji Kibaha iliyopo Mkoani Pwani kupandishwa hadhi na kuwa Manispaa.

Uamuzi huo umetangazwa leo Januari 27 na Waziri wa Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa wakati akizungumza katika mkutano wa CCM uliofanyika Januari 27 katika viwanja vya stendi ya zamani Mailimoja Kibaha Mkoani Pwani.

Soma Pia: Mohammed Mchengerwa: Rais Samia Ameipandisha Hadhi Geita kuwa Manispaa na Rufiji kuwa Halmashauri ya Mji


Mchengerwa, ametangaza hilo wakati akizungumza na wanachama wa CCM pamoja na Wananchi katika mkutano mkubwa wa kuunga mkono maazimio ya mkutano Mkuu wa CCM Taifa uliomteua Rais Samia kuwa mgombea wa Urais mwaka 2025.
 
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia Halmashauri ya Mji Kibaha iliyopo Mkoani Pwani kupandishwa hadhi na kuwa Manispaa.

Uamuzi huo umetangazwa leo Januari 27 na Waziri wa Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa wakati akizungumza katika mkutano wa CCM uliofanyika Januari 27 katika viwanja vya stendi ya zamani Mailimoja Kibaha Mkoani Pwani.

Soma Pia: Mohammed Mchengerwa: Rais Samia Ameipandisha Hadhi Geita kuwa Manispaa na Rufiji kuwa Halmashauri ya Mji


Mchengerwa, ametangaza hilo wakati akizungumza na wanachama wa CCM pamoja na Wananchi katika mkutano mkubwa wa kuunga mkono maazimio ya mkutano Mkuu wa CCM Taifa uliomteua Rais Samia kuwa mgombea wa Urais mwaka 2025.
Mmaposema wanachama wa CCM na wananchi mnamaanisha nini? Kwamba wanachama wa CCM siyo wananchi?
 
Back
Top Bottom