Halmashauri ziache kuwalazimisha Watumishi kuchangia Mwenge

Walimu ndio punching bag zao..wanatumikishwa sana hawa watu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Acha uongo, hakuna makubaliano yoyote yanayofanyika zaid ya kulazimishana tu
 
Wewe ni muongo na mnafiki, hicho kikao huwa wanakaa nani wakakubaliana?
 
Upuuzi huu sasa ifikie mahali ukome
 
Wadau Nawasalimu.Najua MWENGE wa UHURU upo Chini ya Serikali kipitia WIZARA husika.Wizara husika ktk Makadirio yake iliomba Fedha za Kuendesha Shughuli nzima za MWENGE wa UHURU. Wizara husika inapaswa izipeleke Sehemu ya Fedha hizo ktk Halmashauri zote ambazo MWENGE wa UHURU utakimbizwa.Kinachoonekana kwa sasa ni HALMASHAURI kuwachangisha WATUMISHI kwa KUWAKATA kwenye MISHAHARA yao MIDOGO ili Kufanikisha MBIO za MWENGE.Ukweli hiyo Sio HAKI hata KIDOGO
Tunaiomba WIZARA husika na MWENGE itumie FEDHA ilizotengewa na BUNGE kwa Kuzipeleka WILAYANI badala ya WAKURUGENZI kuwachangisha Watumishi.USHAHIDI wa WATUMISHI kuchangishwa huo hapo CHINI.Na kama SERIKALI haina FEDHA za kuendesha SHUGHULI za MWENGE wa UHURU iachane Nao.
 
Yaani kama huwa kuna vitu havitakiwi hata kujadiliwa, kukimbiza mwenge ni kimojawapo. Sijui bado tuko karne ya ngapi sisi jamani.
 
Hao ni Walimu sio Watumishi.
Walimu acheni kujichanganya na watumishi wengine, hio kazi yenu ni laana.
 
Hivi mwalimu akikataa kuchanga watamfanyaje?
Swali zuri. Hawamfanyi kitu. Ila wanahamasishwa kuchangia Ili kumpokea na kumkirimu mgeni. Asipochangia mmoja au wawili, wengine watachangia na mambo yataenda.

Ushauri wangu. Tusipende kuamini kuwa kila jambo ni baya tu kisa wewe hulipendi.
 
Swali zuri. Hawamfanyi kitu. Ila wanahamasishwa kuchangia Ili kumpokea na kumkirimu mgeni. Asipochangia mmoja au wawili, wengine watachangia na mambo yataenda.

Ushauri wangu. Tusipende kuamini kuwa kila jambo ni baya tu kisa wewe hulipendi.
Kama ni hiari sidhani kama kuna tatizo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…