SoC04 Halmashauri zitumie vyanzo hivi vipya kupata kodi endelevu kwa maendeleo ya nchi

SoC04 Halmashauri zitumie vyanzo hivi vipya kupata kodi endelevu kwa maendeleo ya nchi

Tanzania Tuitakayo competition threads

Xpertz

Member
Joined
May 3, 2024
Posts
13
Reaction score
10
UTANGULIZI
Halmashauri nyingi nchini zimekua zikitumia vyanzo vya mapato vile vile miaka yote, hakuna ubunifu wa vyanzo vipya, halmashauri nyingine zimekua mizigo kwa Serikali kwa kutegemea fedha nyingi kutoka Serikali kuu ili kujiendesha huku zikiwa na vyanzo vingi vya mapato ambavyo havitumiki. Nashauri MAENEO yafuatayo yaguswe kupata mapato zaidi ya Serikali :

1. Biashara ya Nyumba za kupanga za makazi irasimishwe
Nashauri biashara ya nyumba za kupanga nchini kote irasimishwe na wapangishaji wote wawe na leseni pia serikali itoze angalau asilimia 20% ya kodi pia wapangaji wawe wanalipia kodi kwa utaratibu rasmi wapewe na risiti na MIKATABA yao ikaguliwe
(Anuani za makazi tayari zitakua zimesaidia kurahisisha zoezi hili kwa kutambua nyumba zinazofanya biashara ya kupangisha, ANGALIZO: kodi hii iwe ni maalumu kwa nyumba zinazopangishwa kwa ajili ya makazi na biashara tu).

Humu kwenye nyumba za kupanga za makazi Serikali inapoteza mabilion ya pesa kila mwezi mfano mimi ninapoishi nmepanga nalipia Tshs. 150,000/= kila mwezi(vyumba viwili na sebule) ila serikali haipati hata mia mbovu kwenye pesa hiyo. Wapo watu wanalipia kodi mpaka 1,000,000 kwa mwezi mmoja ila Serikali haipati kitu. Hii ni biashara lazima Serikali ikusanye na ifanyike kwenye nyumba za kibiashara pia maarufu kama fremu.

Kodi hizi za nyumba za kibiashara na za kupangisha baada ya wapangishaji kukaguliwa mikataba yao, watendaji wa kata watumike kukusanya mapato hayo ya halmashauri kwa njia za kielekroniki(wapewe mashine za EFD) na pia iwapo mpangaji akiwa anataka kuhama au anahama mpangishaji atoe taarifa hiyo kabla ya mwisho wa mwezi (kwa. Mujibu wa mkataba wa mpangaji) unaofuata toka kuhama mpangaji na afisa wa halmashauri ngazi ya kata athibitishe na kuripoti nakala kwa mwajiri wake(halmashauri).

Pia iwe ni kosa kisheria kupangisha nyumba kwa ajili ya makazi au biashara bila kuwa na leseni, faini isipungue shilingi za kitanzania milioni moja.

2. Halmashauri ziwekeze kwenye miradi ya kimkakati ya biashara maeneo yenye uhitaji.
Serikali bado inakosa fedha nyingi kwa kukosa maono, kuna maeneo mengi mfano Kuna uhaba wa Kumbi za sherehe, magari ya abiria, vituo vya mafuta, wakala wa kifedha, nyumba za kulala wageni nk Serikali inaweza kujenga au kuwekeza huko na kupata mapato makubwa mno. Mfano uhitaji wa nyumba za kulala wageni kwenye miji ya kimkakati kama Dodoma mjini, Dar, Arusha na jirani na stendi karibu zote za kimkakati hakuna za gesti za Serikali kwanini?

3. Kuta za uzio za mashule, vyuo na baadhi ya maofisi yaliyo katikati ya miji zitumike kibiasharara.
Mfano shule ya sekondari Uhuru (ya Serikali) iliyopo Shinyanga mjini imezungushiwa ukuta wenye eneo zuri mno la kujenga vyumba vya biashara zaidi ya 200 lakini hautumiki cha kusikitisha kwenye shule hiyo hata chaki zikiisha Serikali inanunua.

4. Halmashauri zikodishe mitambo na vifaa vya kitaalamu kuongeza mapato.
Kwenye halmashauri nyingi nchini ujenzi unaendelea wa miradi mingi na majumba binafsi lakini halmashauri hazinufaiki moja kwa moja na ukuaji wa shughuli hizo kwa kushiriki kiufundi kuchochea upatikanaji wa vitendea kazi kwa kuvikodisha na kupata mapato mengi. Hili ni tatizo karibu halmashauri zote nchini

5. Maeneo ya wazi ya Serikali yaliyotengwa kwa matumizi fulani ya baadae kama matumizi halisi mda wa utekelezaji bado sana yawekewe mipango ya matumizi ya dharura kuchochea shughuli za kiuchumi na kuongeza mapato kwa Serikali. Mfano maeneo mengi ya hifadhi ya reli na barabara ambayo hayatarajiwi kuendelezwa leo wala kesho yaliyo maeneo ya mijini yatumike kukodishia wajasiriamali wadowadogo kwa biashara ndogo ndogo kodi zikusanywe.

6. Serikali iwe ya kwanza kuvuna rasilimali za nchi.
Hapa ni kwenye rasilimali za kimkakati kama madini, halmashauri zetu ziunde kampuni mfano za uchimbaji (ndogo au kubwa) kwa kutumia wataalamu wa ndani walioajiriwa na halmashauri hizo ili halmashauri ziwe za kwanza kuchangamkia fursa mbalimbali ambapo itasaidia kuzalishia halmashauri husika mapato makubwa mno. Kwa mfano kwenye sekta ya madini kwa sasa halmashauri zetu zinachoambulia ni fedha ya fadhila kwa jamii (CSR) pekee huku makampuni ya uchimbaji ambayo mengi ni kutoka nje yakivuna utajiri mkubwa kwenye halmashauri hizo kwa mfano halmashauri ya Kishapu ulipo mgodi wa Mwadui na El Hilal kunakochimbwa almasi halmashauri hiyo ni moja kati ya halmashauri zenye uchumi dhaifu zaidi nchini wakati ina utajiri mkubwa wa madini.
 
Upvote 3
Humu kwenye nyumba za kupanga za makazi Serikali inapoteza mabilion ya pesa kila mwezi mfano mimi ninapoishi nmepanga nalipia Tshs. 150,000/= kila mwezi(vyumba viwili na sebule) ila serikali haipati hata mia mbovu kwenye pesa hiyo. Wapo watu wanalipia kodi mpaka 1,000,000 kwa mwezi mmoja ila Serikali haipati kitu. Hii ni biashara lazima Serikali ikusanye na ifanyike kwenye nyumba za kibiashara pia maarufu kama fremu.
Kuna ule mpango wa kuchukua kodi zao kila mtu anaponunua umeme, je? Bado unahisi serikali haipati kodi zake stahiki?

Halmashauri ziwekeze kwenye miradi ya kimkakati ya biashara maeneo yenye uhitaji.
Serikali bado inakosa fedha nyingi kwa kukosa maono, kuna maeneo mengi mfano Kuna uhaba wa Kumbi za sherehe, magari ya abiria, vituo vya mafuta, wakala wa kifedha, nyumba za kulala wageni nk Serikali inaweza kujenga au kuwekeza huko na kupata mapato makubwa mno. Mfano uhitaji wa nyumba za kulala wageni kwenye miji ya kimkakati kama Dodoma mjini, Dar, Arusha na jirani na stendi karibu zote za kimkakati hakuna za gesti za Serikali kwanini?
Hapa patamu, maana serikali kwa uwezo wa kimtaji ilionao, ina uwezo wa kujenga na kuendesha miradi mikubwa mno ili kujipatia kipato badala ya kuweka mzigo wote katika kodi.
Tena hii uliyoongea ni midogo wanaweza (kuwaachia watu binafsi) ukilinganisha na miradi ambayo serikali iko na uwezo nayo.
Kuta za uzio za mashule, vyuo na baadhi ya maofisi yaliyo katikati ya miji zitumike kibiasharara.
Mfano shule ya sekondari Uhuru (ya Serikali) iliyopo Shinyanga mjini imezungushiwa ukuta wenye eneo zuri mno la kujenga vyumba vya biashara zaidi ya 200 lakini hautumiki cha kusikitisha kwenye shule hiyo hata chaki zikiisha Serikali inanunua.
Wazo zuri sana hili. Rasilimali zinazowezabkusaidiabkuendesha taasisi zisikae bure🙅‍♂️. Zifanyiwe kazi bhana. Ahsante.

Halmashauri zikodishe mitambo na vifaa vya kitaalamu kuongeza mapato.
Saaafi, na hii itegemee tu eneo lina uhitaji wa nini? Mfano eneo watu wanalima sana serikali ya eneo lao inaweza kumiliki matrekta ya kukodisha. Kama tu tunavyoona majosho ya serikali - maeneo yenye wafugaji au magari makubwa ya uzoaji taka na majitaka. Tanzania tuitakayo inawezekana sana tu
 
Kuna ule mpango wa kuchukua kodi zao kila mtu anaponunua umeme, je? Bado unahisi serikali haipati kodi zake stahiki?


Hapa patamu, maana serikali kwa uwezo wa kimtaji ilionao, ina uwezo wa kujenga na kuendesha miradi mikubwa mno ili kujipatia kipato badala ya kuweka mzigo wote katika kodi.
Tena hii uliyoongea ni midogo wanaweza (kuwaachia watu binafsi) ukilinganisha na miradi ambayo serikali iko na uwezo nayo.

Wazo zuri sana hili. Rasilimali zinazowezabkusaidiabkuendesha taasisi zisikae bure🙅‍♂️. Zifanyiwe kazi bhana. Ahsante.


Saaafi, na hii itegemee tu eneo lina uhitaji wa nini? Mfano eneo watu wanalima sana serikali ya eneo lao inaweza kumiliki matrekta ya kukodisha. Kama tu tunavyoona majosho ya serikali - maeneo yenye wafugaji au magari makubwa ya uzoaji taka na majitaka. Tanzania tuitakayo inawezekana sana tu
Kabisa mkuu
 
Umeshauri vizuri sana Mkuu, ila hapo kwenye Kodi za majengo mbona tunalipia kupitia malipo ya Umeme?

Hata hivyo ukiona nyumba imejengwa ujue wakati wote wa Ujenzi, Serikali imepata Kodi kupitia 18% ya VAT.

Hata hivyo haipendezi mtu umetumia shilingi 100,000,000 kujenga nyumba yako ya Kupangisha, hata fedha zako ulizotumia kuwekeza hazijarudi eti Serikali ichukue Kodi tena?

Labda ungeshauri wachukue Kodi Kwa MaDalali ambao hulipwa Mwezi mmoja Kwa Kila mpangaji anayemleta kwenye nyumba yangu.

Mathalani kama mteja wangu analipa Kodi ya shilingi 120,000 Kwa Mwezi, basi dalali aliyemleta huyo mteja kwenye nyumba yangu ili apange, basi atapewa kiasi cha shilingi 120,000 kutoka Kwa mteja
 
Umeshauri vizuri sana Mkuu, ila hapo kwenye Kodi za majengo mbona tunalipia kupitia malipo ya Umeme?

Hata hivyo ukiona nyumba imejengwa ujue wakati wote wa Ujenzi, Serikali imepata Kodi kupitia 18% ya VAT.

Hata hivyo haipendezi mtu umetumia shilingi 100,000,000 kujenga nyumba yako ya Kupangisha, hata fedha zako ulizotumia kuwekeza hazijarudi eti Serikali ichukue Kodi tena?

Labda ungeshauri wachukue Kodi Kwa MaDalali ambao hulipwa Mwezi mmoja Kwa Kila mpangaji anayemleta kwenye nyumba yangu.

Mathalani kama mteja wangu analipa Kodi ya shilingi 120,000 Kwa Mwezi, basi dalali aliyemleta huyo mteja kwenye nyumba yangu ili apange, basi atapewa kiasi cha shilingi 120,000 kutoka Kwa mteja
Ile inayokatwa kwenye umeme ibaki kuwa ya ardhi pekee (pango) na ifanyike kwa nyumba zote(za makazi binafsi na za Kupangisha /biashara) ila za kibiashara zote za Kupangisha za makazi na biashara zikatwe hii ya kufanya biashara

Point yangu ni kwamba biashara ya upangishaji sio sahihi kukatwa kodi sawa na kodi ya pango ya makazi binafsi ya kawaida ya makazi
Umeshauri vizuri sana Mkuu, ila hapo kwenye Kodi za majengo mbona tunalipia kupitia malipo ya Umeme?

Hata hivyo ukiona nyumba imejengwa ujue wakati wote wa Ujenzi, Serikali imepata Kodi kupitia 18% ya VAT.

Hata hivyo haipendezi mtu umetumia shilingi 100,000,000 kujenga nyumba yako ya Kupangisha, hata fedha zako ulizotumia kuwekeza hazijarudi eti Serikali ichukue Kodi tena?

Labda ungeshauri wachukue Kodi Kwa MaDalali ambao hulipwa Mwezi mmoja Kwa Kila mpangaji anayemleta kwenye nyumba yangu.

Mathalani kama mteja wangu analipa Kodi ya shilingi 120,000 Kwa Mwezi, basi dalali aliyemleta huyo mteja kwenye nyumba yangu ili apange, basi atapewa kiasi cha shilingi 120,000 kutoka Kwa mteja
 
Back
Top Bottom