Halotel ni wezi, wakimbieni!

Halotel ni wezi, wakimbieni!

Kuna mwenzio jana alileta malalamiko kama yako. Alipopiga simu akaambiwa amejiunga na huduma ya "Hadithi ya Kaundime"😂

Hebu angalia na wewe usije ukawa ni mteja wa Hadithi ya Kaundime.

Teteteeee ...nacheka kwa huzuni
 
hakuna bando linaloisha kwa 'haraka' bila kutumia kwa 'haraka'
Ficha upumbavu wako nimefanya kazi mtandao mmoja wa simu kitengo flani kwa mwaka mmoja najua wizi unaofanyika

Ushawah jiuliza kuna menu unaingia unakuta 1Gb kwa tsh 1000 na lain hio hio unaenda menu ingne unakuta 1Gb kwa buku jero 😁 kwann? Huoni kuna moja imesetiwa haiesabu real 1GB
 
Nilikuwa mtumiaji mzuri sana wa mtandao wa Vodacom. Baadae wakaja kupandisha bei za vifurushi vyao kwa kiwango kikubwa.
Niliendelea kutumia Vodacom kwa matumizi yangu makubwa na kidogo laini ya Halotel.

Baadae nikaja kushtuka Vodacom ukiwa mteja mzuri wanakupandishia bei,vifurushi vyako vinakuwa vya gharama zaidi kuliko wanaotumia kwa kusua sua. Nikaacha au kupunguza sana kuweka vocha na kununua bando kwenye Vodacom.

Nikahamia Halotel,vifurushi vyao havikuwa na gharama sana kama Vodacom,ila speed yao ya Intanet haikuwa na uwezo mkubwa kama Vodaocom,lakini ilitosha. Karibuni hapa nao wamepandisha bei za vifurushi,nikaona wote ni wale wale. Kilichokuja kunishtua ni bando la halotel kuanza kuisha kwa haraka sana. Bando la wiki halimalizi siku moja. Gb 1 inaisha ndani ya muda mfupi mno kwa matumizi ya kawaida,nikaona kuna kitu hakipo sawa.

Nikasema ngoja nianze kutumia tena Vodacom,kuanzia juzi najiunga mabando ya Vodacom tu. Huwa nanunua vocha kutoka App ya NMB,bila intanet hununui vocha kwenye app.....Kwa kuwa sasa nimeseti matumizi yangu yote kwenda laini ya vodacom,nikanunua vocha ya 1000 kwenye laini ya halotel ikae standby,ili bando likikata kwenye voda,nitumie hii buku kununulia vocha kwenye App ya NMB. BILA MATUMIZI YEYOTE NILIYOFANYA KWENYE HALOTEL,ASUBUHI HII WAMEKATA 200 kwenye ile buku niliyoweka standby,nakuta kuna Tsh 800 tu.
Mitandao imebuni njia nyingi za kuibia wateja wao mojawapo ni kukuunga na malipo ya Huduma pasipo kujua ,mfano halotel wana mtindo wa kukutumia meseji umejiunga na huduma flani siku moja ni bure, baada ya hapo utakatwa shilingi 125 kwa siku kama huitaji huduma hii tuma neno ondoa kwa herufi kubwa .
Kwa vile wengi wetu huwa hatusomi jumbe hizi hujikuta tumeungwa na huduma hizi pasipo hiari na kujikuta tunakatwa pasipo kujua. kwa maana hiyo kama kuna watanzania milioni moja kwenye mtandao kama huu wanakatwa kiasi hicho ni pesa nyingi sana kwa mwezi na ukiwapigia wanakwambia utakua umejiuga bila kujua wakati si kweli, ni vema kusoma meseji zote zinazoingia kwenye simu.
 
Mimi nimeshahama kwa Sasa niko TTCL nibora upewe Gb chache lakini wasikuibie kwenye matumizi sasa unanunua gb 1 kwenye matumizi nikama unatumia mb 200 tu bando linaisha
 
Huna pa kukimbilia. Hao wote huwa wanakaa vikao ili wawanyonye kwa pamoja ili isije ikatokea mmoja wao akajifanya mwema sana akawaharibia wengine biashara.
Kila utakapokwenda wembe ni ule ule
 
Ttcl sijui inataka kujifia?
Maana kutopatikana kwa network Kwa masaa mengi limekuwa ni jambo la kawaida siku hizi [emoji848][emoji848]

Inauma sana.

Imagine mtu anataka huduma labda ya Bolt/Uber taxi aende hospitali lakini TTCL wamekata mtandao na hakuna mbadala wa usafiri mwingine si ni mtihani mkubwa huo?!

TTCL mnakwaza sana [emoji57][emoji57][emoji18]
Dharura ni nyingi sana,hii mitandao tunaipa dhamana kubwa lakini inatufelisha..
 
Kuna mwenzio jana alileta malalamiko kama yako. Alipopiga simu akaambiwa amejiunga na huduma ya "Hadithi ya Kaundime"😂

Hebu angalia na wewe usije ukawa ni mteja wa Hadithi ya Kaundime.

Hizo huduma huwa wanakuunga kiujanja ujanja,unapewa maelezo ya mtego ili ujiunge bila kujua kuwa utakatwa hela.
 
Hauko Serious mzee, natumia Zantel mwaka wa 4 na sasa kwa kurahisisha huduma wameunganisha na Tigopesa.

Yani nikitumiwa hela Zantel naenda kuitoa kwa Till ya Tigopesa mda wowote.
Bando zao ziko mkuu .kwa mfano ya buku mb ngapi
 
Hauko Serious mzee, natumia Zantel mwaka wa 4 na sasa kwa kurahisisha huduma wameunganisha na Tigopesa.

Yani nikitumiwa hela Zantel naenda kuitoa kwa Till ya Tigopesa mda wowote.
Zantel mikoan wapo kweli? Mana hata dar penyewa huwa nawaonaga pale mikochen wamepaki hiace zao kama zpo yard vile
 
najua mkuu,nikitumia kwa haraka najua,na nikitumia kawaida najua...
Dawa yake ni very simple, hakikisha kwamba hiyo buku yako unaiweka kama MPESA au HaloPesa na kamwe usiiache kama vocha maana lazima wataipiga panga. Hiyo laini yako ya Halotel hata ikibaki na zero vocha fresh tuu ila cha muhimu buku iko kwenye HALOPESA.. Ukitaka kununua vocha au kifurushi unanunua direct kutoka kwenye HALOPESA... Mimi sikumbuki ni lini niliwahi kuacha salio la vocha kwenye laini, kwanza nimeshasahau... Hata kununua vocha za kukwangua nimesahau kabisa... Yaani nikivuta salio kutoka HALOPESA au airtel money saa hiyo hiyo najiunga na kifurushi husika na hakuna vocha inabaki.
 
Ttcl sijui inataka kujifia?
Maana kutopatikana kwa network Kwa masaa mengi limekuwa ni jambo la kawaida siku hizi [emoji848][emoji848]

Inauma sana.

Imagine mtu anataka huduma labda ya Bolt/Uber taxi aende hospitali lakini TTCL wamekata mtandao na hakuna mbadala wa usafiri mwingine si ni mtihani mkubwa huo?!

TTCL mnakwaza sana [emoji57][emoji57][emoji18]
Imeshajifia hiii kilichobaki ni slogan ya rudi nyumbani eti kumenoga... Hawa badala ya kukabiliana na ushindani wa soko wao wakawekeza kwenye kufanya lobbying serikalini ili wabebwe hasa kipindi cha serikali ya awamu ya tano... [emoji23] [emoji23]
 
Wewe umeiweka inazagaa zagaa wao walipopita wakajua labda umeangusha wakapita nayo...siku nyingine hifandhi pesa M pawa au Air tel money hawakati kule.
Exactly [emoji1666] [emoji1666] [emoji1666]
 
Back
Top Bottom