Hamjamkomoa Mo Dewji kwa kukosa ubingwa, mmewakomoa na kuwaumiza sana Wanasimba msimu huu

Mwishokambi

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2020
Posts
390
Reaction score
1,425
Simba imevuliwa ubingwa, wale viongozi waliodhani wanamkomoa Mo Dewji wakae wakijua kuwa aliyekomoka sio Mo Dewji, ni sisi wanachama na mashabiki, tunajua viongozi wala hamshtuki kwa sababu haya yalitegemewa.

Msimu huu, mipango na mikakati iliuzwa mapema tu, tunashukuru sana, na yanga wataendelea kuwa mabingwa msimu ujao kwa sababu GSM anajielewa.
 
Hao wataondoka tu, japo itaigharimu Sana Simba lakini tukimalozana na hao basi tutakua levels za waydad
 
Mnafuraha mpaka mnakosa cha kuandika.alafu mnatawazwa kuwa mabingwa hamjaanda mbuzi au ng'ombe tuje tule wajameni,ng'ombe wa Mayele bado yupo au ulikufa?
Yanga si huwa wanakata moto kipindi cha pili?

Leo hii nimekosea tena?
 
Mbumbumbu bwana!
 
Mimi naendelea kulaumu benchi la ufundi la Simba ,Kuna mechi walikua wanadharau yaan tulipoteza mechi kizembe Sana na kutoa draw kisa kuishi kwa mazoea.
Yanga wamefanikiwa sabab kila mechi kwao ilikua fainali hawakudharau hata timu moja.
Simba wangekua serious huu ubingwa ungekuja amuliwa kwa idadi ya magoli Kama sio point moja tu.lakin kwa vile Simba waliishi kwa mazoea ona yanga anatangaza ubingwa huku akiwa na mechi tatu mkonon ,hizi ni dharau ndio zimetuponza kukosa morali na kucheza vikosi vipya kila mechi.

Na msimu ujao nawoana yanga wakitwaa Tena ubingwa km Simba hawataacha dharau za kudharau baadhi ya mechi na kutokua serious kwa kila mechi.

Kuna mechi Simba alipoteza kizembe Sana ,acha yanga abebe ubingwa ili tujifunze kuheshimu opponents wetu tunapokutana nao .hongereni Wana yanga.
 
Yanga si huwa wanakata moto kipindi cha pili?

Leo hii nimekosea tena?
kilichowasaidia ni kwamba mwenye nyumba aliweka mkazo zaidi kazi za nje ya nchi kuhakikisha nchi inapata nafasi nne ndo nyinyi mkapata nafasi ya kubeba ubingwa.ila msimu ujao walai nakuhakikishia nguvu zote azitowekwa kimataifa tu itakua 50/50 nusu ndani nusu nje.
 
hakuna cha kukomoana, simba ni dhaifu.

halafu msiwe mnazungumzia kombe letu, kombe ni kama mke wetu, maswala ya jinsi ya kumg*g*da mtuachie sisi
 
Ndo mana kuna timu nyingi kwajili yakushindania kombe
Msimu huu wamepoteza wajipange kwa msimu mwingine
 
Tulishakubaliana Simba Sc ina kikosi kipana🤣🤣🤣
 
Simba kuna watu wapumbavu sana,unawezaje kumwacha mchezaji kama Morrison na huna hela ya kusajili kushindana na akina Berkane?

Mwaka huu hatutaki ule ujinga wa kutudanganya kwenye usajili kupitia media.
Tena kuna huyu mwenyekiti IQ yake ina mashaka mashaka sana.Club haiwezi kuwa na mwenyekiti mropokaji.Unawezaje kutudanganya eti Simba inaweza kusajili mchezaji yeyote inayemtaka na wakati mmekaa kibahili kiasi hicho?
 
Hongereni watani hakika mlistahili . Ki ukweli mlikuwa mmejipanga kuhakikisha mnatwaa ubingwa wa mwaka huu tofati na sisi wapinzani wenu. HONGERENI SANA!
 



sasa ndugu ulitaka kila mwaka uwe ww bingwa tu.. halafu unatakiwa ujue kitu kimoja.. yanga kuchukua ubingwa msimu huu imeisadia sana Simba hasa katika ndoto zao za kuwania ubingwa wa Africa

sababu ukweli ni kuwa simba kwa kuchukua ubingwa mara nne kuliwafanya warelax kwenye usajili so wakalegeza maana kichwan waliamin they are the best kumbe walikuwa bora kwenye kundi la watu dhaifu.. infact hawakuwa dhaifu na wala hawakuwa bora walikuwa average saaa ukiwa avarage kwenye kundi dhaifu ww ni bora

so hili la kukosa ubingwa litawaamsha usingizin ... na pia yanga wasidhani ni bora kipimo cha ubora wao kiko mashindano ya nje kule ndo benchmark

ukiona team kama Berkane anastragle kucheza club bingwa maana yake juu yake ana team bora kina waydad.. ubora wa waydad na Alahly unachagizwa na ubora wa kina zamalek na wengineo..

kipimo za uzuri wa kitu kinatokana na ubaya wa kitu kingine.. pepo zisingekuwa na sifa kama kusingekuwa na jehanam

fikiria ungeambiwa ukitenda dhambi utabak dunian ila ukitenda mema utaenda mbinguni wangapi wangetaka kwenda mbinguni
 
Ni jambo lililokuwa wazi kuwa Simba hawakuwa na kikosi bora Cha kupambania ubingwa msimu huu timu ilikuwa inacheza tu ilimradi...... imagine unapambaniaje ubingwa na striker kama Mugalu au Boko.....??

Yanga waliteleza mara kadhaa lakini kikosi dhaifu Cha Simba kikashindwa kutumia faida hiyo.......


Ni dhahiri kikosi dhaifu Cha Simba hakikuweza kutoa ushindani wa ukweli kuelekea mbio za ubingwa dhidi ya Yanga........

Hongera mtani kwa kuumaliza ukame wa miaka minne......
 

Mkuu Ulipaswa kuwa EFM, WASAFI, CLoUDs.

Umeandika Point sanaaa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…