Hamtaki Sasa? Huu ni ukigeugeu wa baadhi ya Watanzania Wenzetu!

Hamtaki Sasa? Huu ni ukigeugeu wa baadhi ya Watanzania Wenzetu!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Mambo mengine yanashangaza na mengine yanachukiza. Wapo watu miongoni mwetu ambao wanakasarishwa na wengine wanakerwa kwelikweli kuona CCM inatumia wingi wake Bunge la Katiba kushinikiza misimamo yake. Watu wengine wanakasirika kabisa na wanahamaki wakijiuliza "kwani Katiba inayotaka kupitishwa ni ya CCM au ya Taifa?"; na wengine wanashangaa ati kwanini "CCM haiweki maslahi ya taifa mbele?!" Kweli kabisa wapo watu na wengine ni watu wenye heshima na wazoefu katika siasa za nchi yetu nao wanashangaa ati "CCM imeteka mchakato wa Katiba"

Sasa hawa ndugu zetu hawataki CCM kutumia wingi wake kwenye Bunge la Katiba na wanaisihi ati wasiweke "uvyama" kwanza na badala yake waweke dubwasha moja liitwalo "Utaifa kwanza"! Na hawa si watu nje ya Bunge bali wapo wengine ndani ya hilo Bunge ambao nao wanawasihi wana CCM kuweka "maslahi ya Taifa kwanza"

Kwanini? Kwanini watu hawataki CCM ilioteka ajenda ya Katiba Mpya isitumie wingi wake kupitisha maslahi yake? Kwanini watu hawataki CCM ambayo Mwenyekiti wake alianzisha mchakato wa Katiba Mpya na akawateua wana CCM mashuhuri kuusimamia? Kwanini watu hawataki CCM ambayo ilipitisha Sheria ya Mchakato wa Katiba iliyompa Rais ambaye ni Mwenyekiti wao nguvu kubwa katika mchakato huu wasitumie nafasi hiyo kutimiza maslahi yao?

Watu walikubali ile sheria, wakakubali kushiriki kwenye mchakato na wakakubali kuwa sheria ile ya mchakato imewapa wingi mkubwa wana CCM kwenye Bunge la Katiba. Hivi ndugu zetu walikuwa wanafikiria kuwa mchakato umewekwa kuwajaza wana CCM ilikuwa ni kwa bahati mbaya? Kwamba mchakato mzima unamzunguka RAis na utaongozwa na wana CCM hivi wanafikiri iliandaliwa vile kwa sababu hakukuwa na uchaguzi mwingine (another alternative)? Sasa kama kabla ya kuundwa kwa Bunge la Katiba miaka karibu mitatu nyuma waliambiwa kuwa mchakato huu ni wa ki CCM sasa CCM wanataka kutumia nafasi ya nguvu yao kwanini tunawatakalia?

Kama sera ya CCM ni serikali mbili na hilo limethibitishwa jana na wote tunajua ndio msimamo rasmi wa chama tangu miaka ya 1990s sasa kwanini watu wanafikiria kuwa wanafungwa na mapendekezo ya TUme ya Katiba Mpya? Kwani TUme ya Katiba Mpya ilipiga kura ya maoni au ilikusanya maoni tu? Na nchi haiongozwi na mapendekezo ya Tume inaongozwa na sera za chama kilichoko madarakani na tutake tusitake chama kilichoko madarakani ni CCM; sera zake ndizo zinatakelezwa kuanzia kwenye nishati, maji, elimu, umeme na hata mfumo wa utawala?

Sasa kama CCM msimamo wake ni serikali mbili na kinataka kuhakikisha wanachama wake wana 'toe the line' kwa kuhakikisha kuwa kunakuwa na kura ya wazi kwanini tunataka kuwakatlia? Kwani nani kasema serikali tatu ndilo suluhisho pekee - hata kama limependekezwa na TUme ya Warioba?

Ninachosema ni kuwa kama watu walikubali principle kuwa mchakato huu ni halali na kuwa CCM inaweza kujazana huko ndani sasa kwanini wakatae matokeo ya kujazana huko na nguvu yake hiyo kubwa? Au watu walikuwa wanaombea labda CCM itaacha kuwa CCM na itafuata wengine? Kwamba watu walikuwa wanaombea kuwa CCM itabadilika na kufuata misimamo ya wengine ili kuwaridisha wao na siyo kujiridhisha yenyewe?

Wapinzani na wanamageuzi wengine waliokubali kushiriki mchakato huu na kukubali mfumo huu ulioibeba CCM wawe tayari kula kiburi yao! Wavune walichokubali kipandwe! CCM kwa haki kabisa inatumia sheria na mfumo uliokubaliwa kuhakikisha inapitisha mapendekezo yake na kwa haki kabisa wanaweza kuifumua rasimu ya Katiba kuhakikisha kuwa inatengenezwa kukubali serikali mbili na si tatu kama ilivyo sasa!

Tunaweza tusipende, tunaweza kuchukia, tunaweza kuona kuwa CCM wanaweka uchama mbele n.k lakini ukweli unabakia pale pale; wanafanya kilicho ndani ya uwezo wao. Si tulishawakubali in principle? We have to live with the consequences? Au hatutaki kuishi na matokeo ya maamuzi yetu wenyewe?

Binafsi kwa kweli sijashtuka, sijashangazwa wala sijasikitishwa na yanayofanywa na yatakayofanywa na CCM kwenye hilo Bunge lao. Well, waliliandaa hivyo sasa kwanini tushangae? Watu walikubali wapande mbegu, na tulijua wanapanda mbegu gani tena wanapenda vipi na wapi; sasa leo wanataka kuvunja tunataka kuruka; tunataka viote vingine? Well, imekula kwetu - itakuwepo kura ya wazi na inawezekana serikali mbili ikarudi na wapinzani na wengine hata wakikasirika. Yatakuwa ni maamuzi ya kidemokrasia na yanakubalika kisheria wenye kutaka kugoma Bungeni watagoma, wenye kupiga kelele watapiga na wenye kuzungumza kwa uchungu tutawaona lakini ukweli utabakia kuwa ukweli.

Imekula kwao!

Next time, usikubali ngamia aangize kichwa kwenye hema!
MMM
 
Halafu mimi nímekuwa nakereka sana na hii kauli ya kisiasa ya kusema ''kuweka mbele'' maslahi ya taifa

Hivi taifa ni nini kama siyo watu. Sasa hawa watu wamejificha wapi kwenye bunge la katiba?.

Kama wabunge siyo watu au Watanzania basi hata hoja ya kusema kuweka mbele maslahi ya taifa itakuwa valid lakini kama hawa wabunge ni watu na Watanzania basi hata wao ni taifa na chochote kile watakachokipitisha ndiyo kitakuwa kuweka mbele maslahi yao ambayo ndiyo maslahi ya taifa.

Kama mlifahamu kuwa hawa wabunge hawawezi kuweka mbele maslahi ya taifa kwa maana kwamba maslahi yenu basi ninyi mnaowaomba ndiyo hamukuweka mbele maslahi ya taifa kwa sababu kama mngekuwa mmeweka mbele maslahi ya taifa basi msingewaruhusu hawa wabunge kwenda kwenye bunge la katiba kwa maana nyingine, ninyi mnaofahamu maslahi ya taifa ndiyo mngeenda kutengeneza hiyo katiba.

Mpaka pale mtakapopata tiba ya kansa ya kulalamika lalamika, ndiyo siku hiyo mtafahamu athari za kulalamika lalamika tu wakati hata hamjitambui.
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji hayo unayoyasema uliyasema kitambo na watu wengine waliyanena kitambo. Lakini kilichotokea kila mtu anakifahamu. Watu walialikwa wakaingia nyumba nyeupe wakanena na kilichonenwa hakikutolewa hadharani mchakato ukaanza. Leo hii wala hawakumbuki kwamba kuna sheria inayoongoza mchakato ambayo ilipita mbele ya macho yao wakiwa macho wazi kabisa.

Huwa hata mimi sielewi ya kwamba watu wameingia Bungeni kupitia makundi yenye dhamira moja kwa mfano wanachama wa CCM lakini tunasema yasiegemee makundi yao! Tunataka kundi la wafanyakazi lisiwasilishe na kutetea wafanyakazi huko kwenye katiba, tunataka wanaharakati wa haki za binadamu wasitetee haki za binadamu. Kama yalivyo hayo makundi ambayo yanatetea maslahi yao basi na CCM inatetea maslahi yake!


Tungetaka uwakilishi wa kweli labda tungechaguana mitaani, vitongojini na vijijini ili kupata uwakilishi sawa wa wananchi badala ya watu kupitia vyama. Ndio maana mwisho wa siku unakuta mtu na mkewe wanawakilisha chama! Hao bila shaka watakuwa wanatetea maslahi ya nyumba yao!
 
Last edited by a moderator:
Mambo mengine yanashangaza na mengine yanachukiza.
Imekula kwao!
Next time, usikubali ngamia aangize kichwa kwenye hema!
MMM
Mkuu Mwanakijiji, nakushukuru kwa sasa kuliona hili!, naomba tuu kufanya rejea siku ile niliposhauri hivi, Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!, Wewe Mzee Mwanakijiji, ulisimama nao!, kinachotokea sasa ni muendelezo tuu wa ile safari!.

Maji ukiyavulia nguo, huna budi kuyaoga!. Sasa maji yako maliwato na muogaji keshaingia maliwatoni!, huko hakuna kingine, ni ether kukoga or kukogeshwa!. Akikoga mwenyewe, anaweza kujifuta maji huko huko maliwatoni na kutoka mkavu kana kwamba hajakoga!. Asipotaka kukoga mwenyewe, atakogeshwa na hapo atatoka amerowa na kutwetwa maji baada ya kukogeshwa na kuroweshwa!.

"I fear the Greeks, especially when they bring gifts!", baada ya kukubali tule tujizawadi twa chai na juice, now its pay back time!, sasa ni kuendelea tuu na safari! tena ilibidi kwa kutulia tuli kama ananyolewa na wembe wa CCM wenye makali kuwili, ukifurukuta unaweza kukukata!.

Nasisitiza "If you can't get what you want!, just take what you get!. Japo tulihitaji "Katiba Bora!", mchakato huu utatupatia "Bora Katiba!", natoa wito kwa wote tuiunge mkono hiyo bora katiba kwa kuipigia kura ya ndio!, tupate katiba mpya!.
Pasco
 
Sasa kama CCM msimamo wake ni serikali mbili na kinataka kuhakikisha wanachama wake wana 'toe the line' kwa kuhakikisha kuwa kunakuwa na kura ya wazi kwanini tunataka kuwakatlia? Kwani nani kasema serikali tatu ndilo suluhisho pekee - hata kama limependekezwa na TUme ya Warioba?

Ninachosema ni kuwa kama watu walikubali principle kuwa mchakato huu ni halali na kuwa CCM inaweza kujazana huko ndani sasa kwanini wakatae matokeo ya kujazana huko na nguvu yake hiyo kubwa? Au watu walikuwa wanaombea labda CCM itaacha kuwa CCM na itafuata wengine? Kwamba watu walikuwa wanaombea kuwa CCM itabadilika na kufuata misimamo ya wengine ili kuwaridisha wao na siyo kujiridhisha yenyewe?
Sidhani kama kuna sababu za kutengeneza uhusiano kama ulioweka hapo juu kutokana na paragraphs hizo mbili hapo juu. Short and clear, kila mmoja pale bungeni ana HAKI NA WAJIBU wa kutetea anachokiamini bila kujali kwamba hapo kabla kulikuwa na mazingira haya au yale! Binafsi ninachokiona toka kwa wapinzani wa CCM ni ama kukosa ukomavu wa kisiasa au labda kuna ugonjwa mpya; CCMphobia! Kama ulivyosema hapo juu, CCM wana haki ya kutetea msimamo wao wa kutaka serikali mbili kama ambavyo CHADEMA walivyo na haki ya kutetea serikali tatu! Kama ingekua pendekezo ya Tume la serikali tatu ingekuwa ndo final basi mengine yote yaliyopendekezwa na Tume yangekuwa final na pasingekuwa tena na sababu ya kuitisha bunge la katiba na hata hapo baadae kuipigia kura!

Binafsi mathalani, hapo awali nilikuwa naunga mkono serikali tatu kwa sababu moja tu; kwamba hakuna guarantee kwamba no matter what, muungano huu hautakuja kuvunjika hata siku moja daima dumu! Kwa kuzingatia yale ambayo yamepata kutokea kwenye "miungano" mbalimbali duniani tena ambayo ilidumu kwa miongo kadhaa k.v USSR, Yugoslavia, Czechoslovakia, basi utaona hakuna exceptional kwa Tanzania; it's just a matter of time! Nikizingatia kwamba hata leo hii Scotland inafikiria kuachana na UK, nikaona Tanzania we're not that blessed kwamba no matter what, muungano utadumu tu kwa karne kadhaa wa kadhaa! It's all a matter of time; probably very soon especially itakapotokea CHADEMA yenye sura hii ya sasa ikachukua madaraka...siamini kabisa kwamba wanaweza kuiva na Wazanzibar! Kwa kuzingatia kwamba existence ya muungano haijatoa guarantee kwamba hautavunjika basi nikaona Serikali Tatu ndio mfumo pekee utakaoweza kutufanya stuachane kwa usalama bila kuacha mzozo wa madaraka popote itakapotokea muungano umevunjika! Hata hivyo, nilipokuja kuona mfumo wa serikali mbili unaopendekezwa na CCM; nalazimika hatimae kuwaunga mkono! Hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa; kwamba yeyote mwenye hoja yake anatakiwa kuitetea lakini si mbaya kubadilika ukiona ya mwenzako imekugusa! Kwahiyo wana-CHADEMA ni kama wanaonesha ni namna gani wasivyojitambua wanavyoipinga CCM kutetea msimamo wao wa serikali mbili wakati wao wapo kidete kutetea serikali tatu! Hoja kwamba serikali tatu ndiyo imependekezwa ni hoja mfu coz' katiba yote ni mapendekezo so kama ingekuwa ni hoja ya msingi basi isingejadiliwa!
 
Huwa hata mimi sielewi ya kwamba watu wameingia Bungeni kupitia makundi yenye dhamira moja kwa mfano wanachama wa CCM lakini tunasema yasiegemee makundi yao! Tunataka kundi la wafanyakazi lisiwasilishe na kutetea wafanyakazi huko kwenye katiba, tunataka wanaharakati wa haki za binadamu wasitetee haki za binadamu. Kama yalivyo hayo makundi ambayo yanatetea maslahi yao basi na CCM inatetea maslahi yake!
Mkuu Kimbunga, umenena vyema kabisa! Unajua watu tunasahau kwamba wajumbe wote wa bunge la katiba ni ama wanakilisha kundi hili au lile! Imepaswa kupeleka wawakilishi kv isingewezekana watanzania wote 45m+ tuingie mjengoni! So, ikiwa mjumbe X anawakilisha kundi Y, maana yake ni kwamba huyu anatakiwa kutetea kwa nguvu ya hoja maslahi ya kundi Y coz' imeshindikana akina Y wote kwenda huko! Hawa akina Y wapo kundi Y kv wameridhika kwa hiari yao na misingi ya kundi Y ndio maana wakawa pamoja nao! Sasa huyu Mjumbe X analazimika kuitetea misingi ya kundi Y kv, assumption ni kwamba ndicho kilichowavuta akina Y otherwise wangekuwa somewhere else! Hili ndilo ambalo watu wana-miss! Wabunge wa CCM wapo pale, technically kuwakilisha wananchi waliowachagua sio kuwakilisha chama watu wanavyotaka tuamini! Hapa inasimama assumption ile ile kwamba, wananchi waliwachagua wabunge wa CCM kv wananchi hao wameridhika kwa hiari yao misingi ya CCM, misingi ambayo CCM leo hii wanapaswa kuitetea kwa nguvu ya hoja kv tuna-assume ndiyo iliyowafanya wapate kura za wananchi!

Kutokana na ukweli huo, basi ni mtu asiyeelewa tu ndie anaweza kuwapinga CCM kv kutetea mfumo wa serikali mbili basi.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mzee Mwanakijiji hayo unayoyasema uliyasema kitambo na watu wengine waliyanena kitambo. Lakini kilichotokea kila mtu anakifahamu.

Tungetaka uwakilishi wa kweli labda tungechaguana mitaani, vitongojini na vijijini ili kupata uwakilishi sawa wa wananchi badala ya watu kupitia vyama. Ndio maana mwisho wa siku unakuta mtu na mkewe wanawakilisha chama! Hao bila shaka watakuwa wanatetea maslahi ya nyumba yao!
Tuliogopa gharama!.
 
Sidhani kama kuna sababu za kutengeneza uhusiano kama ulioweka hapo juu kutokana na paragraphs hizo mbili hapo juu. Short and clear, kila mmoja pale bungeni ana HAKI NA WAJIBU wa kutetea anachokiamini bila kujali kwamba hapo kabla kulikuwa na mazingira haya au yale! Binafsi ninachokiona toka kwa wapinzani wa CCM ni ama kukosa ukomavu wa kisiasa au labda kuna ugonjwa mpya; CCMphobia! Kama ulivyosema hapo juu, CCM wana haki ya kutetea msimamo wao wa kutaka serikali mbili kama ambavyo CHADEMA walivyo na haki ya kutetea serikali tatu! Kama ingekua pendekezo ya Tume la serikali tatu ingekuwa ndo final basi mengine yote yaliyopendekezwa na Tume yangekuwa final na pasingekuwa tena na sababu ya kuitisha bunge la katiba na hata hapo baadae kuipigia kura!

Binafsi mathalani, hapo awali nilikuwa naunga mkono serikali tatu kwa sababu moja tu; kwamba hakuna guarantee kwamba no matter what, muungano huu hautakuja kuvunjika hata siku moja daima dumu! Kwa kuzingatia yale ambayo yamepata kutokea kwenye "miungano" mbalimbali duniani tena ambayo ilidumu kwa miongo kadhaa k.v USSR, Yugoslavia, Czechoslovakia, basi utaona hakuna exceptional kwa Tanzania; it's just a matter of time! Nikizingatia kwamba hata leo hii Scotland inafikiria kuachana na UK, nikaona Tanzania we're not that blessed kwamba no matter what, muungano utadumu tu kwa karne kadhaa wa kadhaa! It's all a matter of time; probably very soon especially itakapotokea CHADEMA yenye sura hii ya sasa ikachukua madaraka...siamini kabisa kwamba wanaweza kuiva na Wazanzibar! Kwa kuzingatia kwamba existence ya muungano haijatoa guarantee kwamba hautavunjika basi nikaona Serikali Tatu ndio mfumo pekee utakaoweza kutufanya stuachane kwa usalama bila kuacha mzozo wa madaraka popote itakapotokea muungano umevunjika! Hata hivyo, nilipokuja kuona mfumo wa serikali mbili unaopendekezwa na CCM; nalazimika hatimae kuwaunga mkono! Hivi ndivyo inavyotakiwa kuwa; kwamba yeyote mwenye hoja yake anatakiwa kuitetea lakini si mbaya kubadilika ukiona ya mwenzako imekugusa! Kwahiyo wana-CHADEMA ni kama wanaonesha ni namna gani wasivyojitambua wanavyoipinga CCM kutetea msimamo wao wa serikali mbili wakati wao wapo kidete kutetea serikali tatu! Hoja kwamba serikali tatu ndiyo imependekezwa ni hoja mfu coz' katiba yote ni mapendekezo so kama ingekuwa ni hoja ya msingi basi isingejadiliwa!
Mkuu NasDaz, nimeguswa na objectivity yako na uwasilishaji hoja zako!, nadhani you were "born teacher" kufundisha, darasa hili ni darasa tosha!.
Thanks!.
Pasco
 
Mambo mengine yanashangaza na mengine yanachukiza. Wapo watu miongoni mwetu ambao wanakasarishwa na wengine wanakerwa kwelikweli kuona CCM inatumia wingi wake Bunge la Katiba kushinikiza misimamo yake. Watu wengine wanakasirika kabisa na wanahamaki wakijiuliza "kwani Katiba inayotaka kupitishwa ni ya CCM au ya Taifa?"; na wengine wanashangaa ati kwanini "CCM haiweki maslahi ya taifa mbele?!" Kweli kabisa wapo watu na wengine ni watu wenye heshima na wazoefu katika siasa za nchi yetu nao wanashangaa ati "CCM imeteka mchakato wa Katiba"

Sasa hawa ndugu zetu hawataki CCM kutumia wingi wake kwenye Bunge la Katiba na wanaisihi ati wasiweke "uvyama" kwanza na badala yake waweke dubwasha moja liitwalo "Utaifa kwanza"! Na hawa si watu nje ya Bunge bali wapo wengine ndani ya hilo Bunge ambao nao wanawasihi wana CCM kuweka "maslahi ya Taifa kwanza"

Kwanini? Kwanini watu hawataki CCM ilioteka ajenda ya Katiba Mpya isitumie wingi wake kupitisha maslahi yake? Kwanini watu hawataki CCM ambayo Mwenyekiti wake alianzisha mchakato wa Katiba Mpya na akawateua wana CCM mashuhuri kuusimamia? Kwanini watu hawataki CCM ambayo ilipitisha Sheria ya Mchakato wa Katiba iliyompa Rais ambaye ni Mwenyekiti wao nguvu kubwa katika mchakato huu wasitumie nafasi hiyo kutimiza maslahi yao?

Watu walikubali ile sheria, wakakubali kushiriki kwenye mchakato na wakakubali kuwa sheria ile ya mchakato imewapa wingi mkubwa wana CCM kwenye Bunge la Katiba. Hivi ndugu zetu walikuwa wanafikiria kuwa mchakato umewekwa kuwajaza wana CCM ilikuwa ni kwa bahati mbaya? Kwamba mchakato mzima unamzunguka RAis na utaongozwa na wana CCM hivi wanafikiri iliandaliwa vile kwa sababu hakukuwa na uchaguzi mwingine (another alternative)? Sasa kama kabla ya kuundwa kwa Bunge la Katiba miaka karibu mitatu nyuma waliambiwa kuwa mchakato huu ni wa ki CCM sasa CCM wanataka kutumia nafasi ya nguvu yao kwanini tunawatakalia?

Kama sera ya CCM ni serikali mbili na hilo limethibitishwa jana na wote tunajua ndio msimamo rasmi wa chama tangu miaka ya 1990s sasa kwanini watu wanafikiria kuwa wanafungwa na mapendekezo ya TUme ya Katiba Mpya? Kwani TUme ya Katiba Mpya ilipiga kura ya maoni au ilikusanya maoni tu? Na nchi haiongozwi na mapendekezo ya Tume inaongozwa na sera za chama kilichoko madarakani na tutake tusitake chama kilichoko madarakani ni CCM; sera zake ndizo zinatakelezwa kuanzia kwenye nishati, maji, elimu, umeme na hata mfumo wa utawala?

Sasa kama CCM msimamo wake ni serikali mbili na kinataka kuhakikisha wanachama wake wana 'toe the line' kwa kuhakikisha kuwa kunakuwa na kura ya wazi kwanini tunataka kuwakatlia? Kwani nani kasema serikali tatu ndilo suluhisho pekee - hata kama limependekezwa na TUme ya Warioba?

Ninachosema ni kuwa kama watu walikubali principle kuwa mchakato huu ni halali na kuwa CCM inaweza kujazana huko ndani sasa kwanini wakatae matokeo ya kujazana huko na nguvu yake hiyo kubwa? Au watu walikuwa wanaombea labda CCM itaacha kuwa CCM na itafuata wengine? Kwamba watu walikuwa wanaombea kuwa CCM itabadilika na kufuata misimamo ya wengine ili kuwaridisha wao na siyo kujiridhisha yenyewe?

Wapinzani na wanamageuzi wengine waliokubali kushiriki mchakato huu na kukubali mfumo huu ulioibeba CCM wawe tayari kula kiburi yao! Wavune walichokubali kipandwe! CCM kwa haki kabisa inatumia sheria na mfumo uliokubaliwa kuhakikisha inapitisha mapendekezo yake na kwa haki kabisa wanaweza kuifumua rasimu ya Katiba kuhakikisha kuwa inatengenezwa kukubali serikali mbili na si tatu kama ilivyo sasa!

Tunaweza tusipende, tunaweza kuchukia, tunaweza kuona kuwa CCM wanaweka uchama mbele n.k lakini ukweli unabakia pale pale; wanafanya kilicho ndani ya uwezo wao. Si tulishawakubali in principle? We have to live with the consequences? Au hatutaki kuishi na matokeo ya maamuzi yetu wenyewe?

Binafsi kwa kweli sijashtuka, sijashangazwa wala sijasikitishwa na yanayofanywa na yatakayofanywa na CCM kwenye hilo Bunge lao. Well, waliliandaa hivyo sasa kwanini tushangae? Watu walikubali wapande mbegu, na tulijua wanapanda mbegu gani tena wanapenda vipi na wapi; sasa leo wanataka kuvunja tunataka kuruka; tunataka viote vingine? Well, imekula kwetu - itakuwepo kura ya wazi na inawezekana serikali mbili ikarudi na wapinzani na wengine hata wakikasirika. Yatakuwa ni maamuzi ya kidemokrasia na yanakubalika kisheria wenye kutaka kugoma Bungeni watagoma, wenye kupiga kelele watapiga na wenye kuzungumza kwa uchungu tutawaona lakini ukweli utabakia kuwa ukweli.

Imekula kwao!

Next time, usikubali ngamia aangize kichwa kwenye hema!
MMM

Nakubalia na wewe 100%!!! hata hao wanaolalamika wangekuwa leo watawala na wakawa wengi wangefanya hivyo hivyo. Leo hii tunaona ufinyu wa demokrasia ndani ya vyama vya upinzani vikishamiri, itakuwaje wakishika nchi? Ni ukweli usiopingika kwamba majority (ambao ndiyo wananchi waliwapa mandate ya kutawala) ku-dictate mchakato wanaoutaka. Ndiyo demokrasia hiyo.
 
walishasahau kwamba walitaka kuandamana lakini walipoitwa pale magogoni na kupata hiyo juice na picha kede kede huku wakipeana mikono na kukenua kwa tabasamu.....wakubali kwamba kwa sasa imekula kwao big time otherwise hawakujua wanachofanya kitu ambacho ni aibu pia
 
Bado napingana na CCM inapowatishia wanachama wake(wajumbe)
 
Tatizo la wapinzani ni kukubali hata vitu vya kijinga wakati mwingine ili wasionekane wanapinga kila kitu tu kama wanavyoimbiwa! Mchakato wa Katiba ulikuwa na matatizo toka mwanzo lakini busara mbuzi zisizoakisi mahitaji halisi ya wananchi ndio zinatufikisha hapa tunaishia kulalamika.

CCM wanahaki ya kusimamia maslahi yao ikiwemo serikali mbili ambao ni msimamo wao rasmi hivyo mbinu yoyote watayotumia ni sawia kabisa sijui watu wanalalamika nini! Kwa kifupi tunapoteza muda na huu mchakato kibaya zaidi tunazugana huku 2015 ndio hiyo inafika na utafanyika uchaguzi ktk mazingira haya haya!

CCM itashinda tena uchaguzi wa 2015 tena kirahisi kabisa labda kisambaratike kitu ambacho ni kigumu kwa mazingira ya sasa kama haikuwa hivyo mwaka 2005.Tusubiri masihi mpya asimamie ukombozi wa kweli maana inakatisha tamaa.
 
Mkuu Kimbunga, umenena vyema kabisa! Unajua watu tunasahau kwamba wajumbe wote wa bunge la katiba ni ama wanakilisha kundi hili au lile! Imepaswa kupeleka wawakilishi kv isingewezekana watanzania wote 45m+ tuingie mjengoni! So, ikiwa mjumbe X anawakilisha kundi Y, maana yake ni kwamba huyu anatakiwa kutetea kwa nguvu ya hoja maslahi ya kundi Y coz' imeshindikana akina Y wote kwenda huko ! Hawa akina Y wapo kundi Y kv wameridhika kwa hiari yao na misingi ya kundi Y ndio maana wakawa pamoja nao! Sasa huyu Mjumbe X analazimika kuitetea misingi ya kundi Y kv, assumption ni kwamba ndicho kilichowavuta akina Y otherwise wangekuwa somewhere else! Hili ndilo ambalo watu wana-miss! Wabunge wa CCM wapo pale, technically kuwakilisha wananchi waliowachagua sio kuwakilisha chama watu wanavyotaka tuamini! Hapa inasimama assumption ile ile kwamba, wananchi waliwachagua wabunge wa CCM kv wananchi hao wameridhika kwa hiari yao misingi ya CCM, misingi ambayo CCM leo hii wanapaswa kuitetea kwa nguvu ya hoja kv tuna-assume ndiyo iliyowafanya wapate kura za wananchi!

Kutokana na ukweli huo, basi ni mtu asiyeelewa tu ndie anaweza kuwapinga CCM kv kutetea mfumo wa serikali mbili basi.

Hapo kwenye Bold......Ukweli huu ambao NasDaz umeuweka hapa ningelikuwa na uwezo ningempelekea manyerere na wengine wauweke kwenye vyombo vyao vya kupasha habari ili watu waelewe maana ya makundi kuwakilisha misimamo na maslahi ya makundi yao.....
 
Katiba mpya, achilia mbali serikali tatu, haijawahi kuwa ajenda ya CCM, siyo sera ya CCM, na haitakaa kamwe iwe sera ya CCM kwa muda wote ambao kitakuwa madarakani. Sababu ni rahisi - mfumo wa kikatiba uliopo unaihakikishia CCM fursa ya kutawala milele. CCM kubadilisha katiba iliyoweka mfumo unawahakikishia utawala ni sawa na kukata tawi la mti walioukalia. Vyama vya upinzani kutegemea CCM ibadili mfumo uliowaweka na kuwadumisha madarakani ni sawa na kumtegemea simba wa mwituni aongoke na kuacha kula nyumbu kwa sababu tu ni jambo jema.
 
Halafu mimi nímekuwa nakereka sana na hii kauli ya kisiasa ya kusema ''kuweka mbele'' maslahi ya taifa

Hivi taifa ni nini kama siyo watu. Sasa hawa watu wamejificha wapi kwenye bunge la katiba?.

Kama wabunge siyo watu au Watanzania basi hata hoja ya kusema kuweka mbele maslahi ya taifa itakuwa valid lakini kama hawa wabunge ni watu na Watanzania basi hata wao ni taifa na chochote kile watakachokipitisha ndiyo kitakuwa kuweka mbele maslahi yao ambayo ndiyo maslahi ya taifa.

Kama mlifahamu kuwa hawa wabunge hawawezi kuweka mbele maslahi ya taifa kwa maana kwamba maslahi yenu basi ninyi mnaowaomba ndiyo hamukuweka mbele maslahi ya taifa kwa sababu kama mngekuwa mmeweka mbele maslahi ya taifa basi msingewaruhusu hawa wabunge kwenda kwenye bunge la katiba kwa maana nyingine, ninyi mnaofahamu maslahi ya taifa ndiyo mngeenda kutengeneza hiyo katiba.

Mpaka pale mtakapopata tiba ya kansa ya kulalamika lalamika, ndiyo siku hiyo mtafahamu athari za kulalamika lalamika tu wakati hata hamjitambui.

Mkuu,

Mie nafikiri kuna watu mnafikiri mnajua kumbe hamjui!

Ni asilimia 61 ya watanzania waliosema wanahitaji serikali tatu kwenye rasimu ya katiba ya Jaji Warioba,hayo ndio maslahi ya taifa!Sasa hayo maoni ya baadhi ya wabunge(wa CCM) wasiofika hata 500 wanaosema wanataka serikali mbili ni kwa maslahi ya nani?

Sisi wananchi ndio waajiri wa wanasiasa tumeshasema tunataka serikali tatu nyinyi waajiriwa mtasemaje mnataka serikali mbili?Kumbukeni katiba ni sheria zilizowekwa na WATAWALIWA zikimuongoza MTAWAWALA jinsi ya kuongoza na si kinyume cha hapo!

Maslahi ya Taifa yameshasemwa kwenye tume ya warioba,zaidi ya hapo yatakuwa ni maslahi ya watu Fulani!

Acheni kuwafanya watanzania MAFALA!
 
Mambo mengine yanashangaza na mengine yanachukiza. Wapo watu miongoni mwetu ambao wanakasarishwa na wengine wanakerwa kwelikweli kuona CCM inatumia wingi wake Bunge la Katiba kushinikiza misimamo yake. Watu wengine wanakasirika kabisa na wanahamaki wakijiuliza "kwani Katiba inayotaka kupitishwa ni ya CCM au ya Taifa?"; na wengine wanashangaa ati kwanini "CCM haiweki maslahi ya taifa mbele?!" Kweli kabisa wapo watu na wengine ni watu wenye heshima na wazoefu katika siasa za nchi yetu nao wanashangaa ati "CCM imeteka mchakato wa Katiba"

Sasa hawa ndugu zetu hawataki CCM kutumia wingi wake kwenye Bunge la Katiba na wanaisihi ati wasiweke "uvyama" kwanza na badala yake waweke dubwasha moja liitwalo "Utaifa kwanza"! Na hawa si watu nje ya Bunge bali wapo wengine ndani ya hilo Bunge ambao nao wanawasihi wana CCM kuweka "maslahi ya Taifa kwanza"

Kwanini? Kwanini watu hawataki CCM ilioteka ajenda ya Katiba Mpya isitumie wingi wake kupitisha maslahi yake? Kwanini watu hawataki CCM ambayo Mwenyekiti wake alianzisha mchakato wa Katiba Mpya na akawateua wana CCM mashuhuri kuusimamia? Kwanini watu hawataki CCM ambayo ilipitisha Sheria ya Mchakato wa Katiba iliyompa Rais ambaye ni Mwenyekiti wao nguvu kubwa katika mchakato huu wasitumie nafasi hiyo kutimiza maslahi yao?

Watu walikubali ile sheria, wakakubali kushiriki kwenye mchakato na wakakubali kuwa sheria ile ya mchakato imewapa wingi mkubwa wana CCM kwenye Bunge la Katiba. Hivi ndugu zetu walikuwa wanafikiria kuwa mchakato umewekwa kuwajaza wana CCM ilikuwa ni kwa bahati mbaya? Kwamba mchakato mzima unamzunguka RAis na utaongozwa na wana CCM hivi wanafikiri iliandaliwa vile kwa sababu hakukuwa na uchaguzi mwingine (another alternative)? Sasa kama kabla ya kuundwa kwa Bunge la Katiba miaka karibu mitatu nyuma waliambiwa kuwa mchakato huu ni wa ki CCM sasa CCM wanataka kutumia nafasi ya nguvu yao kwanini tunawatakalia?

Kama sera ya CCM ni serikali mbili na hilo limethibitishwa jana na wote tunajua ndio msimamo rasmi wa chama tangu miaka ya 1990s sasa kwanini watu wanafikiria kuwa wanafungwa na mapendekezo ya TUme ya Katiba Mpya? Kwani TUme ya Katiba Mpya ilipiga kura ya maoni au ilikusanya maoni tu? Na nchi haiongozwi na mapendekezo ya Tume inaongozwa na sera za chama kilichoko madarakani na tutake tusitake chama kilichoko madarakani ni CCM; sera zake ndizo zinatakelezwa kuanzia kwenye nishati, maji, elimu, umeme na hata mfumo wa utawala?

Sasa kama CCM msimamo wake ni serikali mbili na kinataka kuhakikisha wanachama wake wana 'toe the line' kwa kuhakikisha kuwa kunakuwa na kura ya wazi kwanini tunataka kuwakatlia? Kwani nani kasema serikali tatu ndilo suluhisho pekee - hata kama limependekezwa na TUme ya Warioba?

Ninachosema ni kuwa kama watu walikubali principle kuwa mchakato huu ni halali na kuwa CCM inaweza kujazana huko ndani sasa kwanini wakatae matokeo ya kujazana huko na nguvu yake hiyo kubwa? Au watu walikuwa wanaombea labda CCM itaacha kuwa CCM na itafuata wengine? Kwamba watu walikuwa wanaombea kuwa CCM itabadilika na kufuata misimamo ya wengine ili kuwaridisha wao na siyo kujiridhisha yenyewe?

Wapinzani na wanamageuzi wengine waliokubali kushiriki mchakato huu na kukubali mfumo huu ulioibeba CCM wawe tayari kula kiburi yao! Wavune walichokubali kipandwe! CCM kwa haki kabisa inatumia sheria na mfumo uliokubaliwa kuhakikisha inapitisha mapendekezo yake na kwa haki kabisa wanaweza kuifumua rasimu ya Katiba kuhakikisha kuwa inatengenezwa kukubali serikali mbili na si tatu kama ilivyo sasa!

Tunaweza tusipende, tunaweza kuchukia, tunaweza kuona kuwa CCM wanaweka uchama mbele n.k lakini ukweli unabakia pale pale; wanafanya kilicho ndani ya uwezo wao. Si tulishawakubali in principle? We have to live with the consequences? Au hatutaki kuishi na matokeo ya maamuzi yetu wenyewe?

Binafsi kwa kweli sijashtuka, sijashangazwa wala sijasikitishwa na yanayofanywa na yatakayofanywa na CCM kwenye hilo Bunge lao. Well, waliliandaa hivyo sasa kwanini tushangae? Watu walikubali wapande mbegu, na tulijua wanapanda mbegu gani tena wanapenda vipi na wapi; sasa leo wanataka kuvunja tunataka kuruka; tunataka viote vingine? Well, imekula kwetu - itakuwepo kura ya wazi na inawezekana serikali mbili ikarudi na wapinzani na wengine hata wakikasirika. Yatakuwa ni maamuzi ya kidemokrasia na yanakubalika kisheria wenye kutaka kugoma Bungeni watagoma, wenye kupiga kelele watapiga na wenye kuzungumza kwa uchungu tutawaona lakini ukweli utabakia kuwa ukweli.

Imekula kwao!

Next time, usikubali ngamia aangize kichwa kwenye hema!
MMM

Aisee!
Kwaiyo raia wakubali tu?
You can't be serious!
 
Bado napingana na CCM inapowatishia wanachama wake(wajumbe)
Hapa nita-assume kwamba hoja yako kwamba CCM inawatisha wanachama wake inatokana na suala zima la ama kura za siri au ya wazi! kama ndivyo, hivi ni CCM inawatishia wanachama wake au ni hisia zetu tu kwamba kv wanataka kura ya wazi ndio tunaamini CCM ina lengo la kuwabana wanachama wake? By the way, kwa kuangalia huu muktadha, hivi wale wanaosimama pale bungeni kutetea kura ya wazi tunaweza kuwaita CCM, kwa maana ya uongozi wa CCM, au hao ni wanachama wa CCM tunaosema wanatishiwa? Ikiwa CCM inataka kuwatisha wanachama wake inakuwaje tena wanachama hao hao wasimame kutetea kutishiwa? Kwani alikuja Pius Mangula pale au Kinana au Nape kutetea suala la kura ya wazi?

Turudi kwenye ama kura ya wazi au ya siri; binafsi wala hayaniumizi kichwa haya mambo. Lakini nichukue upande wa watetezi wa kura ya wazi. Katika historia yetu tangu tuanze mfumo wa vyama vingi, haijapata hata mara moja wanasiasa kutoka upinzani kukiri kwamba wameshindwa kwa haki...mara zote wamekuwa wakidai kura kuchakachuliwa! Leo hii, tunatetea kura ya siri; kura ile ile ambayo ni rahisi kuchakachuliwa! Lakini hata kama isipochakachuliwa, hayatakuja madai yale yale ya miaka nenda rudi kwamba kura zimechakachuliwa? Hivi huoni kwamba ni doa kubwa sana kusema kwamba Katiba X imechakachuliwa pengine ile kuamini kwamba uchaguzi mkuu Y matokeo yake yalichakachuliwa? Ikiwa watu walishapata kutamka hadharani kwamba hawamtambui Rais kwavile matokeo yalichakachuliwa; what kwa vitu sensitive kama katiba? Why should I follow and respect katiba ninayoamini kwamba imechakachuliwa? Hivi leo hii Mkatoliki nini hasa kitamchoma kati ya kumwambia uchaguzi wa Papa ulichakachuliwa au Bible ilichakachuliwa? Kwa sababu Mkatoliki anaweza kuwa Mkatoliki asiye na doa hata kama uteuzi wa Papa ulikuwa na mizengwe lakini Ukatoliki wake utakuwa na madoa endapo itaaminika kwamba Bible imechakachuliwa! Katiba is like Bible wakati Papa is like President! Ndio maana tunasema katiba ni sheria mama na wala sio Rais! Sasa kwanini tusione kwamba, hata kama CCM walifanya hayo kwa ajili ya kuwabana wanachama wake, lakini hiyo ndiyo muafaka kuifanya katiba yetu isiwe ni ile ya kutiliwa shaka?
 
Mkuu,

Mie nafikiri kuna watu mnafikiri mnajua kumbe hamjui!

Ni asilimia 61 ya watanzania waliosema wanahitaji serikali tatu kwenye rasimu ya katiba ya Jaji Warioba,hayo ndio maslahi ya taifa!Sasa hayo maoni ya baadhi ya wabunge(wa CCM) wasiofika hata 500 wanaosema wanataka serikali mbili ni kwa maslahi ya nani?

Sisi wananchi ndio waajiri wa wanasiasa tumeshasema tunataka serikali tatu nyinyi waajiriwa mtasemaje mnataka serikali mbili?Kumbukeni katiba ni sheria zilizowekwa na WATAWALIWA zikimuongoza MTAWAWALA jinsi ya kuongoza na si kinyume cha hapo!

Maslahi ya Taifa yameshasemwa kwenye tume ya warioba,zaidi ya hapo yatakuwa ni maslahi ya watu Fulani!

Acheni kuwafanya watanzania MAFALA!
Je, maoni mengine yaliyopo kwenye mapendekezo ya Tume sio ya Watanzania? Je, haya nayo ni lazima tufuate kile kilichopendekezwa na Tume kwavile ni ndiyo yalipata asilimia nyingi? By the way, ikiwa kila kilichoandikwa ama kupendekezwa na Tume kutokana na idadi ya wale waliokuwa wametoa maoni, kuna maana gani basi kuleta hayo mapendekezo kujadiliwa? Kwanini isiwepo tu timu ya wataalmu waka-structure katiba rasmi kutokana na mapendekezo yaliyopo bila ya kuwa na sababu ya kupeleka tena bungeni?

Kama unaamini kila kilichosemwa na Tume ya Warioba ndiyo maslahi ya taifa basi hakuna tena sababu ya bunge la katiba na hatimae kurudi tena kwa wananchi. Huwezi kuunda bunge la katiba litakalotumia billions of tsh kwa ajili tu ya kwenda kufanya endorsement...kama ni endorsement ya kile ambacho kimeandikwa na Tume Ya Warioba, basi wiki moja ingetosha sana badaya ya hizo 70-90 days!
 
Back
Top Bottom