Hamtaki Sasa? Huu ni ukigeugeu wa baadhi ya Watanzania Wenzetu!

Hamtaki Sasa? Huu ni ukigeugeu wa baadhi ya Watanzania Wenzetu!

Tatizo la wapinzani ni kukubali hata vitu vya kijinga wakati mwingine ili wasionekane wanapinga kila kitu tu kama wanavyoimbiwa! Mchakato wa Katiba ulikuwa na matatizo toka mwanzo lakini busara mbuzi zisizoakisi mahitaji halisi ya wananchi ndio zinatufikisha hapa tunaishia kulalamika.

CCM wanahaki ya kusimamia maslahi yao ikiwemo serikali mbili ambao ni msimamo wao rasmi hivyo mbinu yoyote watayotumia ni sawia kabisa sijui watu wanalalamika nini! Kwa kifupi tunapoteza muda na huu mchakato kibaya zaidi tunazugana huku 2015 ndio hiyo inafika na utafanyika uchaguzi ktk mazingira haya haya!

CCM itashinda tena uchaguzi wa 2015 tena kirahisi kabisa labda kisambaratike kitu ambacho ni kigumu kwa mazingira ya sasa kama haikuwa hivyo mwaka 2005.Tusubiri masihi mpya asimamie ukombozi wa kweli maana inakatisha tamaa.
Mkuu Mtazama, huu unaitwa ukweli mchungu!. Ukweli una tabia moja kuu, "husimama!."

Watu humu waliposikia tuu mchakato wa katiba mpya!, wamehamasishwa kuwa na too great expectations kuwa 2015 things will change!. 2015 ni mambo ni yale yale, watu wale wale, mbinu zile zile na chama kile kile, ila akiwa ni "nanii" hata kama ni chama hicho hicho!, things will change for the better!, otherwise, we are doomed!.
Pasco
 
Wajumbe wa Bunge la Katiba wapo mle kwa makundi na moja ya makundi yaliyomo mle ni vyama vya siasa vikiwakilishwa na wabunge wao.Mjumbe aliyepale kuwakilisha kundi fulani lazima asimamie maslahi ya kikundi hicho hivyo wajumbe walio pale kwa mgongo wa CCM lazima wasimamie maslahi ya CCM.

CCM kwa miaka mingi wanatambua serikali mbili tu hivyo kwenda kinyume na hilo ni kwenda kinyume na chama chako ambacho unakiwakilisha pale.

Hivyo misimamo ya makundi si tatizo ila kilichopaswa kufanyika ni kuwa na mchakato huru toka mwanzo ambao ungetoa wajumbe wanaowakilisha matakwa ya wananchi.Lakini kwa mchakato huu tunadanganyana :nono:
 
Mkuu,

Mie nafikiri kuna watu mnafikiri mnajua kumbe hamjui!
Mkuu, hakuna sehemu niliyosema ninajua, hii hoja unataka kuniwekea kwenye maandishi yangu.

Ni asilimia 61 ya watanzania waliosema wanahitaji serikali tatu kwenye rasimu ya katiba ya Jaji Warioba,hayo ndio maslahi ya taifa!Sasa hayo maoni ya baadhi ya wabunge(wa CCM) wasiofika hata 500 wanaosema wanataka serikali mbili ni kwa maslahi ya nani?
Sasa hao asilimia 61 waliosema wako wapi?. Kwa hiyo hawa 61% walisema tu halafu wakaondoka na kuwaachie wengine wawafanyie kazi ya maslahi ya taifa.

Kama wana wawakilishi kwenye Bunge, kwa nini kila mara wanapiga kelele kuwaambia waangalie maslahi ya Taifa, kwani hawawaamini wawakilishi wao na kama hawaamini, kwa nini waliwapa jukumu la kuandika katiba. Huoni hawa waliowapa jukumu la kuandika katiba ndiyo wana matatizo makubwa sana.

Sisi wananchi ndio waajiri wa wanasiasa tumeshasema tunataka serikali tatu nyinyi waajiriwa mtasemaje mnataka serikali mbili?Kumbukeni katiba ni sheria zilizowekwa na WATAWALIWA zikimuongoza MTAWAWALA jinsi ya kuongoza na si kinyume cha hapo!
Sasa kama ninyi ndiyo waajiri wa wanasiasa, kwa nini basi msikae kimya na kusubili wafanyakazi wenu wafanye kazi mliyowatuma!

Mwajiri makini ni yule anayeajiri pia watu makini na kama huwezi kuajiri watu makini basi wewe ndiyo utakuwa na matatizo na siyo mwajiriwa.

Maslahi ya Taifa yameshasemwa kwenye tume ya warioba,zaidi ya hapo yatakuwa ni maslahi ya watu Fulani!

Acheni kuwafanya watanzania MAFALA!
Kumbe maslahi ya Taifa yanajulikana!.

Sasa kelele za nini tena wakati waajiriwa wanafanya kazi mliyowatuma!.

MAFALA ni wale wanaowatuma watu kuwafanyia jambo wakati hawawaamini katika utendaji wao.
 
Mkuu Mtazama, huu unaitwa ukweli mchungu!. Ukweli una tabia moja kuu, "husimama!."

Watu humu waliposikia tuu mchakato wa katiba mpya!, wamehamasishwa kuwa na too great expectations kuwa 2015 things will change!. 2015 ni mambo ni yale yale, watu wale wale, mbinu zile zile na chama kile kile, ila akiwa ni "nanii" hata kama ni chama hicho hicho!, things will change for the better!, otherwise, we are doomed!. Pasco
Mkuu Pasco, UMENENA! Ni hakika kabisa kwamba watu waliamini na ama bado wanaendelea kuamini kwamba mabadiliko ya katiba ndiyo njia pekee ya kusafisha njia toward 2015...wanasahau kwamba katiba is just sehemu tu ya mchakato mzima! Watu wanasahau kwamba hata katiba ya leo haitoi uhuru wa mtu kuivunja lakini siku zote watu wanaivunja! Labda wapo watakaosema kwamba watu wanaivunja kv katiba hiyo haina pahala inapobana wavunja katiba; kwamba lau kama pangekuwa na kifungu kinachotiliwa mkazo wavunja katiba kuadabishwa pindi wanapoivunja basi pasingekuwa na wa kuivunja!! Wanaamini hivyo huku wakisahau kwamba, kama kuna adabu kubwa iliyoidhinishwa nchi hii basi ni adabu ya kuuawa ikiwa utapatikana na kosa la kuua...lakini kila leo watu wanaua ingawaje adhabu ya kuuawa ipo pale pale! Hadi leo, watu wanabaka ingawaje adhabu kali ya kubaki bado ipo pale pale na inatekelezwa! I am very sorry kwa wale wanaoamini kwamba katiba mpya ndiyo tiketi itakayowaingiza madarakani!
 
Mkuu Mtazama, huu unaitwa ukweli mchungu!. Ukweli una tabia moja kuu, "husimama!."

Watu humu waliposikia tuu mchakato wa katiba mpya!, wamehamasishwa kuwa na too great expectations kuwa 2015 things will change!. 2015 ni mambo ni yale yale, watu wale wale, mbinu zile zile na chama kile kile, ila akiwa ni "nanii" hata kama ni chama hicho hicho!, things will change for the better!, otherwise, we are doomed!.
Pasco

Kinachofanya UKWELI huu kuwa MCHUNGU si kwa sababu tutapata BORA KATIBA na si KATIBA BORA bali tumetumia raslimali pesa kwa kwenda mbele na wakati hopsitali zetu hazina ubora wala vifaa muhimu na madawa.Watanzania wengi wanakufa bila kupata tiba ,wakati wengine tunaponda mali DODOMA na tukija na kibwagiza LISHE tunayopewa ni dnogo as if tunakaa sayari nyingine.
 
Wajumbe wa Bunge la Katiba wapo mle kwa makundi na moja ya makundi yaliyomo mle ni vyama vya siasa vikiwakilishwa na wabunge wao.Mjumbe aliyepale kuwakilisha kundi fulani lazima asimamie maslahi ya kikundi hicho hivyo wajumbe walio pale kwa mgongo wa CCM lazima wasimamie maslahi ya CCM.

CCM kwa miaka mingi wanatambua serikali mbili tu hivyo kwenda kinyume na hilo ni kwenda kinyume na chama chako ambacho unakiwakilisha pale.

Hivyo misimamo ya makundi si tatizo ila kilichopaswa kufanyika na kuwa na mchakato huru toka mwanzo ambao ungetoa wajumbe wanaowakilisha matakwa ya wananchi.Lakini kwa mchakato huu tunadanganyana :nono:
Yes. Ulichoongea ndiyo point katika hoja zote.

Huwezi ukaweka kwenye bunge la katiba wabunge kutoka vyama vyao na unachofanya ni kubadilisha jina tu ukategemea watabadilika hasa katika mazingira ya siasa za Tanzania.

Kama kuna mtu alifikiria kuwa watabadilika basi huyo mtu ndiyo atakuwa ana matatizo kifikra.

Kwanza unaposema MAKUNDI unakuwa tayari umewagawa. Ndiyo maana kwa sasa kinachotafutwa ni maridhiano angalau kama kuna uwezekano katika makubariano lakini kwa jinsi siasa za Tanzania zilivyo, sioni kama kutakuwepo na maridhiano.

Kabla hata ya mchakato kuanza, ajenda kuu ilikuwa ni muungano. Nilitegemea kwanza kungetafutwa maridhiano katika ajenda hii kabla ya mchakato haujaanza ili hata pale mchakato utakapoanza basi haya mataifa mawili yanayoundwa na vyama vikuu vitatu yangekuwa tayari yanafahamu aina ya muungano ndani ya mchakato wa katiba.

Kwenye bunge la katiba kinachofanyika kwa sasa ni kama kutafuta kura katika chaguzi kuu kwa sababu muundo wa serikali ni sera za vyama badala ya muhimili wa nchi bila kujali chama kilichoko madarakani. Muundo wa serikali ungekuwa siyo sera za vyama kwa sasa kama mchakato wa kuingiza muundo wa serikali ungefanyika kabla ya mchakato kuanza.

Kinachofanyika kwa sasa ni kama ndiyo tunaanza mchakato wa katiba.
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji hayo unayoyasema uliyasema kitambo na watu wengine waliyanena kitambo. Lakini kilichotokea kila mtu anakifahamu. Watu walialikwa wakaingia nyumba nyeupe wakanena na kilichonenwa hakikutolewa hadharani mchakato ukaanza. Leo hii wala hawakumbuki kwamba kuna sheria inayoongoza mchakato ambayo ilipita mbele ya macho yao wakiwa macho wazi kabisa.

Huwa hata mimi sielewi ya kwamba watu wameingia Bungeni kupitia makundi yenye dhamira moja kwa mfano wanachama wa CCM lakini tunasema yasiegemee makundi yao! Tunataka kundi la wafanyakazi lisiwasilishe na kutetea wafanyakazi huko kwenye katiba, tunataka wanaharakati wa haki za binadamu wasitetee haki za binadamu. Kama yalivyo hayo makundi ambayo yanatetea maslahi yao basi na CCM inatetea maslahi yake!


Tungetaka uwakilishi wa kweli labda tungechaguana mitaani, vitongojini na vijijini ili kupata uwakilishi sawa wa wananchi badala ya watu kupitia vyama. Ndio maana mwisho wa siku unakuta mtu na mkewe wanawakilisha chama! Hao bila shaka watakuwa wanatetea maslahi ya nyumba yao!

duh!!! kaka umeongea ukweli ambao natamani kila mtu angekuwa anaujua na kuukubali...
na lingine la kuongezea, hivi ni nani anaweza kutueleza hili zimwi''' MASLAHI YA TAIFA "'''' likoje??
 
with CCM Tanzania and Tanzanians are finished. With CCM at the helm GOD is and will not be with us. But CCM should not forget that here is an opportunity to solve these things peacefully. But because of their majority and lack of vision they think they will win.
Its a question of time MY ADVICE TO CCM IS "DON'T WAIT TILL A DAY WHEN THE OPRESSED WILL SAY ENOUGH IS ENOUGH" - AND THAT DAY IS NOT FAR.
 
Ukitaka Taifa liharibikiwe, basi ruhusu siasa itawale
Kibaya zaidi, kuna umati mkubwa sana nimeona hata hapa Jf unaojipambanua kama wajuvi wa siasa lakini hawafahamu hata tofauti ya chama na serikali achilia mbali bunge na chama.
 
Haya ni matokeo ya maamuzi yetu tuliyofanya huko nyuma. Wananchi tunapaswa kujifunza kwamba maamuzi ya wanasiasa yanatawaliwa na mitizamo ya vyama vyao kwanza. Kwa misingi hiyo, tunahitaji kubalansi wawakilishi ili maslahi ya wananchi yapite kwa hoja thabiti na sio mitizamo ya chama. Tusifanye makosa 2015. Ushindani wa nguvu zinazokaribiana usawa kwa kawaida unaleta kilichobora kuliko ‘light weight vs heavy weight'
Kwa suala la muundo wa serikali, kuna mambo watawala hawatuambii ukweli. Tanganyika + Zanzibar= Tanzania Inamaanisha serikali ya Tanganyika+ serikali ya Zanzibar = Serikali ya muungano. In simple logic hizi ni serikali 3, ukiamua kuua serikali za Tanganyika na Zanzibar, inabaki 1 ya muungano. Kwa nini 2? Nilitaraji mvutano wetu uwe serikali 1 au 3. Kama mtizamo ni 2 kwa nini tunainyima haki Tanganyika kuwa na serikali yake?
 
Kibaya zaidi, kuna umati mkubwa sana nimeona hata hapa Jf unaojipambanua kama wajuvi wa siasa lakini hawafahamu hata tofauti ya chama na serikali achilia mbali bunge na chama.

Sidhani kama ni wajuvi wa siasa bali ni wakereketwa wa siasa au wafuasi wa vyama vya siasa.
 
Mkuu,

Mie nafikiri kuna watu mnafikiri mnajua kumbe hamjui!

Ni asilimia 61 ya watanzania waliosema wanahitaji serikali tatu kwenye rasimu ya katiba ya Jaji Warioba,hayo ndio maslahi ya taifa!Sasa hayo maoni ya baadhi ya wabunge(wa CCM) wasiofika hata 500 wanaosema wanataka serikali mbili ni kwa maslahi ya nani?

Sisi wananchi ndio waajiri wa wanasiasa tumeshasema tunataka serikali tatu nyinyi waajiriwa mtasemaje mnataka serikali mbili?Kumbukeni katiba ni sheria zilizowekwa na WATAWALIWA zikimuongoza MTAWAWALA jinsi ya kuongoza na si kinyume cha hapo!

Maslahi ya Taifa yameshasemwa kwenye tume ya warioba,zaidi ya hapo yatakuwa ni maslahi ya watu Fulani!

Acheni kuwafanya watanzania MAFALA!

Ndugu, jaribu kushirikisha ubongo wako! Tume ya warioba ilifikia watanzania wasiozidi laki tatu na hamsini hivi na kati ya hao watanzania kama 47,000 hivi ndio waliozungumzia suala la muungano. Kati ya hao 47,000, 61% ndio waliosema serikali tatu!! kwa maana nyingine watanzania wapatao 28,670 ndio waliopendekeza serikali tatu....je haya mapendekezo ndiyo maslahi ya taifa? kumbuka hawa 61% ni kama 0.067% ya watanzania!!!
 
Ndugu, jaribu kushirikisha ubongo wako! Tume ya warioba ilifikia watanzania wasiozidi laki tatu na hamsini hivi na kati ya hao watanzania kama 47,000 hivi ndio waliozungumzia suala la muungano. Kati ya hao 47,000, 61% ndio waliosema serikali tatu!! kwa maana nyingine watanzania wapatao 28,670 ndio waliopendekeza serikali tatu....je haya mapendekezo ndiyo maslahi ya taifa? kumbuka hawa 61% ni kama 0.067% ya watanzania!!!
Wengi wetu hatujiulizi viswali vichache vifuatavyo:

-CCM waliihitaji KATIBA MPYA? Walimtuma Mwenyekiti wao kuuanzisha mchakato wa Katiba hii?

-WATANZANIA tuliihitaji KATIBA MPYA? Tuliandaliwa kiasi gani kabla ya mchakato kuanza?

-Tulitaka nini hasa kwenye KATIBA MPYA? Tanganyika?

-Kwa kuwa tulianzisha mchakato huu kama maandalizi ya HARUSI, tuko tayari sasa kuanza upya ili tusiendelee kutekeza mapesa ya UMMA.
 
with CCM Tanzania and Tanzanians are finished. With CCM at the helm GOD is and will not be with us. But CCM should not forget that here is an opportunity to solve these things peacefully. But because of their majority and lack of vision they think they will win.
Its a question of time MY ADVICE TO CCM IS "DON'T WAIT TILL A DAY WHEN THE OPRESSED WILL SAY ENOUGH IS ENOUGH" - AND THAT DAY IS NOT FAR.

Who are the oppressed who will say enough is enough? hao unaowasemea wewe ndo waliowachagua wawawakilishe bungeni....na ndo wanaotetea maslahi yao.
 
Mkuu Mwanakijiji, nakushukuru kwa sasa kuliona hili!, naomba tuu kufanya rejea siku ile niliposhauri hivi, Katiba: CHADEMA mlikosea! Kubalini yaishe, Tusonge mbele!, Wewe Mzee Mwanakijiji, ulisimama nao!, kinachotokea sasa ni muendelezo tuu wa ile safari!.


Pasco

Pasco, wakati wewe unazinduka karibu miaka miwili baadaye kuona tatizo la mchakato huu mmi nilishaanisha miezi michache tu baada ya Rais kutangaza nia yake ya kuanzisha mchakato wa Katiba. Mjadala wangu katika mada yako nilikuwa naonesha tu makosa ya kimantiki kwa sababu inaonekana hukuwa umeona tatizo hili mapema zaidi kama sisi wengine.
 
Wengi wetu hatujiulizi viswali vichache vifuatavyo:

-CCM waliihitaji KATIBA MPYA? Walimtuma Mwenyekiti wao kuuanzisha mchakato wa Katiba hii?

-WATANZANIA tuliihitaji KATIBA MPYA? Tuliandaliwa kiasi gani kabla ya mchakato kuanza?

-Tulitaka nini hasa kwenye KATIBA MPYA? Tanganyika?

-Kwa kuwa tulianzisha mchakato huu kama maandalizi ya HARUSI, tuko tayari sasa kuanza upya ili tusiendelee kutekeza mapesa ya UMMA.

Baadhi yetu waliposikia "katiba Mpya" walikuwa kama wamemuona chatu; wamelegea hata kufikiri hawakutaka tena. Nakumbuka watu walitoa pongezi kwa Rais Kikwete kuanzisha mchakato wa Katiba Mpya! Hao hao leo wanamuona mtu wa ndimi mbili..!
 
with CCM Tanzania and Tanzanians are finished. With CCM at the helm GOD is and will not be with us. But CCM should not forget that here is an opportunity to solve these things peacefully. But because of their majority and lack of vision they think they will win.
Its a question of time MY ADVICE TO CCM IS "DON'T WAIT TILL A DAY WHEN THE OPRESSED WILL SAY ENOUGH IS ENOUGH" - AND THAT DAY IS NOT FAR.

Nisingeweza kuliweka sahihi kama ulivyo fanya!

Hata wana CCM wengine hawapo pamoja na kundi linalolazimisha mambo; hili pekee ni la hatari sana.


Naamini evil can never prevail na kwasababu hiyo CCM is destroying itself japo wao hawatambui hilo!
 
Back
Top Bottom