Handeni kuna fursa ya Glocery

Ogopa sana huko Handeni hela huwa zinapotea kimazingara sana [emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Balaa tuliendaga handeni kwanza kuna imani nying za kishirikina,waganga wa kutosha kilichotushangaza ni nyumba nying kuwa za udongo na sio kwamba mmiliki hana uwezo hapana mwenyeji wetu alisema huku ukijenga ya tofal wanajua unapesa wanakumaliza unakuta mtu ana nyumba ya udongo ila kaweka solar [emoji23]
 
Kwidikwazu,chogo, mkata,michungwani,kabuku..... Kuhusu kupigwa zongo kawaida. Sema kabuku pale Kuna kuku wakutosha. Handeni wanaishi wazigua watu wakwenda pale hawapawezi ni wilaya ngumu Sana.
 
Kupitia huu uzi nimejua kwanini watanzania wenye maendeleo ni wachache! Mindset zetu ni changamoto sana! Tuendee kuchangia kwenye ule uzi wa kulana kimasihara wakuu mambo ya fursa tuache sio fani zetu!
 
Idea za sisi Wabongo hizi, huwezi sikia tunawaza Idea za Uzalishaji hata siku 1
 
Kupitia huu uzi nimejua kwanini watanzania wenye maendeleo ni wachache! Mindset zetu ni changamoto sana! Tuendee kuchangia kwenye ule uzi wa kulana kimasihara wakuu mambo ya fursa tuache sio fani zetu!
Kaka kufungua bar handeni ni sawa na kupeleka kitimoto uarabuni. Kwanza washirikina pili kuna watu wa dini.wewe jaribu ujionee
 
Nipo mkata mbweni; barabara ya kwenda halmashauri(1km kasoro ) Kuna bar kama tatu sehem Moja.....na watu wanapiga hela. Na fursa zipo kibao handeni. Uchawi upo Kila sehem ila huku kweli umezidi kidogo ila siyo kikwazo katika utafutaji. Ukiamua unafanya na unafanikiwa tu. Unaeza logwa popote brother.....ukiwa mtaftaji mwamini Mungu ndiye mpaji.
Na guest house zinajengwa sio utani. Karibu Mbweni Mkata.
 

Naomba jina la bar niende nikaondoe uchovu wa siku.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…