HansPoppe : Safari hii hatutaki wachezaji wa kuokota kijiweni kama Kiiza

Usajili wa kibongo unachekesha, eti straika anamweleza/anampigia simu kiongozi kuwa atapiga goli kila mechi halafu kiongozi asiejua lolote kuhusu mambo ya kiufundi na wala hajawahi kumuona huyo straika anapagaaawa mpaka anamponda Hamis Kiiza 'Diego'.Only in Tanzania.
 
Huyo foward ataekuwa anatupia kila game anatoka dunia gani!!!! Basi kama kweli ana uwezo huo hata Ronaldo na Messi hawamfikii.
Aisee! duniani kuna mengi, asipofunga goli anakatwa 1,000,000Tsh? kiongozi makini nae anasema huyo mchezaji yupo makini wakati huko anakotoka wanamwachia! au huko hawataki anaefunga sana.

Hivi yule jamaa mwenye gali yenye plate namba iliyoandikwa "YANGA 1" ni nani vile.
 
Umenena kweli mkui
 
Ningekuwa ndiye Hans Poppe, ningebaki kimya na chezaji langu mfukoni. Pale watu watapoona makali yake ndiyo nianze tambo. Hakumbuki ule wimbo wa enzi zake, 'mtoto wacha kupiga mayowe, wache watu waone wenyewe?'. Sauti ya matendo ni kali kishinda ya maneno.
 
hao wachezaj anawasajili kwa mapendekezo ya kocha au kwa ten percent?kwel matopen kuna vtuko,mayanja analeta wachezaj wake na poppe analeta wake.
 
Acha kukariri we, yanga kuna nini zaid ya Wachezaji kubebeshwa sembe?
 
Mkuu, ifike mahali viongozi watafute kwanza kocha ndiye aje afanye usajili. Huu mwendo wa kusajili wachezaji harafu kocha hautafanikiwa. Sawa atakuwa mchezaji mzuri, je atafit kwenye mfumo wa kocha?

Si yupo Mayanja, au?
 
Naona ishara ya kupaniki kwa uongozi wa Simba na baadhi ya mashabiki.

Timu hii iliyomaliza ligi sio mbaya ni nzuri kabisa kwa viwango vyovyote vya Kibongo, inachohitaji ni kuongezewa nguvu kwenye maeneo yaliyopwaya.Simba hii inaweza kutwa ubingwa kama itaongezewa vichwa 3-4 vitakavyoingia moja kwa moja kikosi cha kwanza ktk eneo la ushambuliaji, na beki ya kati. Wachezaji wengine ni wa kutanua kikosi full stop.

Huu utaratibu wa kusajili upya kila mwaka ni wa kipuuzi mno. Kama wanaachwa watu iwe ni kwa sababu ya utovu wa nidhamu sio uwezo mdogo. Mtu kama Juuko Murshid unamwachaje kwa mfano eti kwa sababu ya uwezo?
 

Msamehe mkuu amekurupuka huyo,nafikiri hata kocha wa Yanga wa sasa hamfahamu.
Habari inamtaja Dusan Kondic,angekua mzima asingetoa povu kwa hiyo habari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…