HansPoppe : Safari hii hatutaki wachezaji wa kuokota kijiweni kama Kiiza

HansPoppe : Safari hii hatutaki wachezaji wa kuokota kijiweni kama Kiiza

Usajili wa kibongo unachekesha, eti straika anamweleza/anampigia simu kiongozi kuwa atapiga goli kila mechi halafu kiongozi asiejua lolote kuhusu mambo ya kiufundi na wala hajawahi kumuona huyo straika anapagaaawa mpaka anamponda Hamis Kiiza 'Diego'.Only in Tanzania.
 
Huyo foward ataekuwa anatupia kila game anatoka dunia gani!!!! Basi kama kweli ana uwezo huo hata Ronaldo na Messi hawamfikii.
Aisee! duniani kuna mengi, asipofunga goli anakatwa 1,000,000Tsh? kiongozi makini nae anasema huyo mchezaji yupo makini wakati huko anakotoka wanamwachia! au huko hawataki anaefunga sana.

Hivi yule jamaa mwenye gali yenye plate namba iliyoandikwa "YANGA 1" ni nani vile.
 
hivi kwa nini hawa viongozi hawajifunzi. walitakiwa waanze na kocha aje na mikakati yake na wachezaji wa aina gani anaowataka kutokana na mifumo yake. then wamtafutie msaidizi ambaye yupo kwenye ligi yetu zaidi ya miaka 3 ili amsaidie kupata majina ya aina ya wachezaji anaowahitaji kwa mifumo yake. kocha na msaidizi wapeleke majina kwenye kamati ya usajili ya aina ya wachezaji wanaowahitaji. lakini cha ajabu kamati ya usajili imeshaanza kusajili mwezi huu wa tano kocha ataletwa mwezi wa saba mwishoni na bado mwezi wa nane mwanzoni wataletwa wachezaji double dobule kwa majaribio maana bado kamati ya usajili itakuwa inaendelea na usajili (sijui huwa wanasajili nini kwa zaidi ya miezi 4)! hapo mwishoni ndio utaona wakina niang, papa ndaw wanapishana airport. mwisho wa siku kocha naye anachanganyikiwa anasajili galasa kama papa ndaw halafu analaumiwa wakati kamati ya usajili ndio inamchanganya pamoja na presha ya kuwahi dirisha la usajili kufungwa. kwa viongozi makini timu inajengwa kwa kuanzia na wachezaji waliopo sio kufukuza wachezaji zaidi ya 15 na kusajili zaidi ya 15 kila mwaka. ukiangalia wachezaji wote waliofukuzwa simba miaka miwili mitatu iliyopita wengi wao ndio wanang'ara kwenye ligi na ndio waliinyima simba ubingwa mwaka huu hili ni somo tosha kwa viongozi. kocha kwanza usajili wa wachezaji baadae vinginevyo mwaka mwingine wa kilio kwa sisi wapenzi wa simba.
Umenena kweli mkui
 
Ningekuwa ndiye Hans Poppe, ningebaki kimya na chezaji langu mfukoni. Pale watu watapoona makali yake ndiyo nianze tambo. Hakumbuki ule wimbo wa enzi zake, 'mtoto wacha kupiga mayowe, wache watu waone wenyewe?'. Sauti ya matendo ni kali kishinda ya maneno.
 
hao wachezaj anawasajili kwa mapendekezo ya kocha au kwa ten percent?kwel matopen kuna vtuko,mayanja analeta wachezaj wake na poppe analeta wake.
 
Akionyesha kiwango, mwaka unafuata anaenda Yanga au Azam. Hawezi kuendelea kukaa feeder club kama wa matopeni!
Viongozi wa Simba hawajifunzi kamwe.. Hivi unasajili wachezaji ndiyo utafute kocha au unapata kocha kwanza aseme wachezaji gani atahitaji?
Dalili za Serunkuma mwingine hizo.
Acha kukariri we, yanga kuna nini zaid ya Wachezaji kubebeshwa sembe?
 
Mkuu, ifike mahali viongozi watafute kwanza kocha ndiye aje afanye usajili. Huu mwendo wa kusajili wachezaji harafu kocha hautafanikiwa. Sawa atakuwa mchezaji mzuri, je atafit kwenye mfumo wa kocha?

Si yupo Mayanja, au?
 
Naona ishara ya kupaniki kwa uongozi wa Simba na baadhi ya mashabiki.

Timu hii iliyomaliza ligi sio mbaya ni nzuri kabisa kwa viwango vyovyote vya Kibongo, inachohitaji ni kuongezewa nguvu kwenye maeneo yaliyopwaya.Simba hii inaweza kutwa ubingwa kama itaongezewa vichwa 3-4 vitakavyoingia moja kwa moja kikosi cha kwanza ktk eneo la ushambuliaji, na beki ya kati. Wachezaji wengine ni wa kutanua kikosi full stop.

Huu utaratibu wa kusajili upya kila mwaka ni wa kipuuzi mno. Kama wanaachwa watu iwe ni kwa sababu ya utovu wa nidhamu sio uwezo mdogo. Mtu kama Juuko Murshid unamwachaje kwa mfano eti kwa sababu ya uwezo?
 
Mchango wa Manji pale Yanga si wa kubeza hata kidogo kama Popo alivyobeza mchango wa Kiiza huko vyura fc. Hata hivyo Manji ana umri mdogo, hata nusu ya umri wa Yanga hafikii. Kabla ya Manji Yanga ilikuwepo, wakati wake Yanga ipo na hata atakapoondoka Yanga itaendelea kuwepo.

Shukrani kwa Manji kwa mchango wake unaoonekana hata kwa vipofu lakini haimaanishi kuwa bila yeye Yanga itakufa, hayo maneno yalisemwa na kocha zaidi ya miaka 7 iliyopita (Tazama tarehe ya gazeti).

Msamehe mkuu amekurupuka huyo,nafikiri hata kocha wa Yanga wa sasa hamfahamu.
Habari inamtaja Dusan Kondic,angekua mzima asingetoa povu kwa hiyo habari
 
Back
Top Bottom