Hivi punde
JF-Expert Member
- Apr 1, 2017
- 2,554
- 8,587
Tafsiri murua kabisa kiongoziNi sawa na kulinganisha Mfungwa (hapa Nazi tuu) na mfanyakazi wa kiwandani(kazi na bata).
Wa kiwandani akimaliza kazi anaingia Canteen anashusha na Serengeti lite baridi kisha anaagana na wenzake kwa furaha hadi kesho huku akiwa na fedha kiasi ya kupitia super market kununua zawadi kidogo za nyumbani.
Yule mfungwa Hapakazituu, baada ya kazi ngumu ni ugali usio na mboga ya kueleweka na moja kwa moja kufungiwa SAA 9 hadi kesho yake.
Ndio furaha ya Magu na CCM yake kwetu sisi. Lakini wenyewe Bata Rubondo na mamaa kama kazi.
Wabaki na #HapaKaziTuu yao huko, hatuitaki
Sent using Jamii Forums mobile app
Umeshajipangia malengo yako ya 2020 ? Na vipaumbele vyako ? Hebu tuanzie hapo kwanza.Wanabodi , mwaka mpya 2020 umeanza tena, mbilinge mbilinge na udambwi dambwi haviishi hapa kwetu Tanzania. Msoto mwanzo mwisho.
Tuje kwenye mada:
"Hapa Kazi Tu" maana yake ni kufanya kazi kwa bidii mwanzo mwisho usiku na mchana bila kusimama, bila kupumzika na kwa uzalendo wote.
"Kazi Na Bata" maana yake kufanya kazi na baadae kujipongeza, kupunguza machungu, kula starehe baada ya kuvuja jasho jingi la msoto.
Nini kipaumbele chako ?
Sent using Jamii Forums mobile app