Hapa ni Gbadolite, Kijijini kwa dikiteta Mobutu Sesseko Kuku Wazabanga, nyumba zimegeuka Magofu na mahame

Charity begins at home! Uzuri ni kuwa chato ipo Tanzania! Kama malalamiko yanayoelekezwa kwa Mkuu yanalenga kutuaminisha kuwa Chato hapana hadhi katika Tanzania, ama basi yaliyofanywa huko yalipaswa kufanyika kaskazini tu itakuwa ni kumuonea mkuu.
Charity inaanzia nyumbani kwako kwa kutumia lasilimali zako mwenyewe,na siyo kwa kutumia lasilimali za kutoka nje na nyumbani kwako,huko ni kuwadhulumu wasiyo kuwa na nafasi ya kuweza kuchukua lasilimali kutoka nje na kupeleka nyumbani kwao wakati ndiowatoaji wakile unachokichukua na kukipeleka kuendeleza kwenu.
 
historia hujirudia
 
Atakachokifanya Magufuli ni kuunda Mkoa wa Chato. Lakini hilo halitasaidia Chato isiwe kama Gbadolite kwa sababu watu wa kupanda ndege kwenda Chato hawapo na watumishi wa serikali watakaokuwa huko kipato chao ni kidogo sana kumudu nauli ya ndege.

Ushauri wangu kwake ni yeye aufanye huo uwanja uwe mali ya JWTZ ili wawe wanafanyia mazoezi yao huko
 
Kwa mtu yeyote mwenye akili timamu anafahamu nini kitatokea kule baada ya JIWE kutoka madarakani...
Hata akija mtawala wa CCM baada yake, bado Chato kama ilivyo hii ya Seseseko! Mpaka sasa sijaona faida yoyote ya kiuchumi kwa huu mradi.
 
KWANINI HAPAWI MAKUMBUSHO AU HATA KUJENGWA KACHUO FULANI HATA KA UONGOZI BORA?
CHUKI ZISITUPUMBAZE WAAFRIKA!
 
CHATO kuwa GBadolite nina uhakika wa zaidi ya asilimia 500,sina shaka hata kidogo.

-Traffic lights zitakufa
-Bank zitakufa
-Uwanja wa Ndege utakufa
-Zoo nayo itakakufa wanyama waote waturudishwa walipotolewa
-Miradi yake aliyoanzisha ambayo ana interest(20% zake) nayo itafumuliwa.
 
Usimfananishe Mtukufu Rais na mambo yako yakipumbavu..

Hii ni Tanzania sio kongo wewe kilaza, kama unapapenda kongo hamia huko
 
Charity begins at home! Uzuri ni kuwa chato ipo Tanzania! Kama malalamiko yanayoelekezwa kwa Mkuu yanalenga kutuaminisha kuwa Chato hapana hadhi katika Tanzania, ama basi yaliyofanywa huko yalipaswa kufanyika kaskazini tu itakuwa ni kumuonea mkuu.

Kuna watu wana akili finyu sana
 

Na ili ujue kuwa Jeuri, Nyodo, Dharau na Unyonyaji wa Rasilimali za Wananchi wako zina mwisho Binti yake Marehemu Mobutu ambaye alikuwa anaoga Pesa tena Dola huku akiwa na Ndege yake Binafsi na akicheza na Dhahabu atakavyo aitwae Ngawali sasa hivi amepigika ( amefilisika ) hadi amefikia kuwa Bar Maid ( Baamedi ) katika Hotel Jijini Paris nchini Ufaransa.
 
Chadema ndo huwa nawaona wajinga hapo tu, yaani nyie kila kitu ni kupinga tu...manyumbu nyie bhana ni shida sana..!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…